Ni kwanini serikali imeshindwa kuwaajiri wahitimu wa fani za mafuta na gesi pamoja na uchache wao?

Ni kwanini serikali imeshindwa kuwaajiri wahitimu wa fani za mafuta na gesi pamoja na uchache wao?

Serikali haikutakiwa kuwa muajiri mkuu kwa hao vijana, service companies, drilling contractors na operators hilo ndio jukumu lao. Serikali waharakishe kusaini mkataba wa LNG, ili operators waendelee na uchimbaji wa gesi Mtwara.
 
Nimependa hiyo phrase "dira ya Taifa".

Wenyewe wana kauli yao eti kila Kitabu na zama zake, wakimaanisha kwamba kila Kiongozi wa nchi anakuja na mipango yake, hii siyo sawa hasa kwa Taifa linaloendelea kama Tanzania.

Hata hii Katiba mpya inayopigiwa kelele inaweza isiwe mwarobaini wa haya mambo ya hovyo yanayotokea nchini.

Mwl Nyerere akizungumzia ubovu wa Katiba tuliyonayo na umuhimu wa kuwa na Katiba mpya aliwahi kutoa angalizo kwamba bila DIRA ya Taifa hata tukiwa na Katiba mpya nzuri kiasi gani, uozo utakuwa ni uleule, akatolea mfano wa Germany kwa Adolf Hitler by then, kumbe kwa kipindi kile Germany ndiyo ilikuwa na Katiba bora kabisa duniani ila Hitler akapenyeza Udikteta, Hitler alifanikiwa kwasababu Germany haikuwa na dira ya Taifa pamoja na kuwa na Katiba bora.

All in all, muda ndiyo mwamuzi mzuri. Ngoja iendelee kunyesha tuone panapovuja.
Nyerere pamoja na akili zake zote alishindwa kuacha Katiba nzuri.

Cha kushangaza akasema kwa Katiba hii akioatikana kiongozi kichwa ngumu anaweza kuwa dikteta, sasa kwanini aliamua tuwe na Katiba ya namna hii?
 
Kuna jamaa mmoja pia kapiga hiyo course pale UDSM, lakini mpaka leo kaishia kuwa mwalimu wa tuition pale Mwanza.


Jamaa ni mjuzi sana ila ndohivyo, bongo nyosso.
Dah! Na kuna siku atakamatwa na Mratibu Elimu Kata na kumuhoji kama anayo taaluma ya Ualimu.

Walimu huwa wanaringia taaluma yao sema wahuni town wanapeta na Tuit kama pale Mchikichini, mapambano, Buguruni n.k watu wanakula Namba kama mizimu vile!
 
Kuna kozi bongo sio za kusoma.

Unasoma kozi za mafuta kwani Tanzania ina mafuta ama inachimba mafuta? Hizo fani ni dili sana huko uarabuni ila bongo ni kupoteza muda wako.

Unasoma unakuja kusubiri uajiriwe na serikali.

Ilikua kidogo niuvae ama niingie cha kike kusoma kozi za kisiasa.

Shemeji yangu aliuvaa mkenge wa kisiasa akasoma kozi inaitwa law enforcement pale UD, hadi sasa anauza juice ya miwa mtaani maana sio mwanasheria sio nani.

Kozi kama hizo za kisiasa na procurement sio za kusoma tena sasa ulimwengu huu.

Tuhamie kwenye IT, Finance(sio accounting) Investment, Projects, Electronics, Electrical, Civil engineering, Architect, Law, Computer nk.

Mimi kwa sasa simshauri mtu kusoma kozi nje ya hizo.
 
Fani za mafuta na gesi zilianza kufundishwa Tanzania mwaka 2013.

Mara serikali ikaanzisha shahada ya kwanza ya kemia ya petroli (BSc. Petroleum Chemistry) (wanafunzi 25), Shahada ya kwanza ya uhandisi wa petroli (BSc. Petroleum Engineering) (Wanafunzi 25) na Shahada ya kwanza ya jiolojia ya petroli (BSc. Petroleum Geology) (wanafunzi 15).

Mwaka 2017, wanafunzi wa kwanza wanahitimu. Lakini serikali inashindwa kuwaajiri pamoja na uchache wao.

Ajira zinatoka TPDC na PURA. Zinaajiri wahitimu wasiozidi sita kwa mwaka. Sasa najiuliza maswali ni jambo gani linazuia kuwaajiri wahitimu wote waliosomea fani hizo.

Ulikua ni mpango wa serikali wa kuandaa wataalamu wa fani hizo katika taifa letu. Tuweke ubinafsi pembeni tuwaajiri wahitimu wote mimi sidhani kama inashindikana. Sio halali mwanafunzi anapata division one ya 5 form six combination ya PCM, na chuo kikuu GPA ya 4.4 taifa linashindwa kumtumia anaamua kuwa auditor kwenye mambo ya uhasibu. Na kwa inavyoonekana ni wengi wala sio mmoja. Tunapaswa kuweka mikakati kama kuna sehemu tumefail tusisite kurudi nyuma na kuanza upya.

Lakini pamoja na kuajiriwa swala la kujiajiri kwa wahitimu wa fani yoyote ni la lazima na hicho ndio kipimo pekee cha kujua kama muhitimu alielewa darasani.

Huu ndio ukweli mhitimu ambaye hawezi kujiajiri maana yake hakuelewa darasani pengine alikua anakalili maarifa bila kuelewa.

Lakini kujiajiri kwa muhitimu kusiwe kisingizio chakutotengeneza ajira katika taifa letu. Bado sisi kama watanzania tunakazi ya kuhakikisha tunatengeneza ajira. Hicho ni kipimo cha ukuaji wa sekta yoyote. Sekta isiyoweza kutengeneza ajira maana yake imesimama kukua.

Hitimisho langu: Sekta ya mafuta na gesi imeshindwa kutimiza malengo iliyojiwekea. Imeshindwa kutengeneza ajira hasa za wahitimu wa gesi na mafuta. Waliokalia viti kwenye sekta ya mafuta na gesi bado hawajafanya kazi vya kutosha. Wanapaswa kuangalia walipoyumba na kufanya marekebisho.

Mwaka 2012 hadi 2013 makampuni ya mafuta na gesi yalijaa Tanzania na yalikua yanajaa vyuoni kuajiri wanafunzi hata kabla hawajamalza vyuo.
Kuna haja ya kubadili uongozi kwenye sekta ya mafuta na gesi ili kurudisha kasi ya kipindi cha nyuma.

Hizi ni baadhi ya hoja ambazo bunge letu lilipaswa kuzizungumzia bungeni na kuwahoji wakuu wa taasisi zinazohusika na mnyororo mzima wa sekta hii. Bunge halipaswi kukaa kimya na kukubali matokeo kasi ya sekta inapokua inashuka.
Mkuu hii mada umekua ukiianzisha kila mara, haipiti miezi 6 hujarudia hii mada naamini wewe ni mhanga mmoja wao ambae umepotezewa muda na wanasiasa. Pole sana.
 
Mkuu hii mada umekua ukiianzisha kila mara, haipiti miezi 6 hujarudia hii mada naamini wewe ni mhanga mmoja wao ambae umepotezewa muda na wanasiasa. Pole sana.
Hapana boss ni mwanasiasa chipukizi nikijianda kupeperusha bendera 2025; hili ni moja la tatizo nililolichagua kulitatua katika taifa letu either kwa uwezo wangu mwenyewe au kwa uwezo wa uongozi kama nitafanikiwa kuchaguliwa kuingia kwenye majengo ya hapa Dodoma.
 
Fani za mafuta na gesi zilianza kufundishwa Tanzania mwaka 2013.

Mara serikali ikaanzisha shahada ya kwanza ya kemia ya petroli (BSc. Petroleum Chemistry) (wanafunzi 25), Shahada ya kwanza ya uhandisi wa petroli (BSc. Petroleum Engineering) (Wanafunzi 25) na Shahada ya kwanza ya jiolojia ya petroli (BSc. Petroleum Geology) (wanafunzi 15).

Mwaka 2017, wanafunzi wa kwanza wanahitimu. Lakini serikali inashindwa kuwaajiri pamoja na uchache wao.

Ajira zinatoka TPDC na PURA. Zinaajiri wahitimu wasiozidi sita kwa mwaka. Sasa najiuliza maswali ni jambo gani linazuia kuwaajiri wahitimu wote waliosomea fani hizo.

Ulikua ni mpango wa serikali wa kuandaa wataalamu wa fani hizo katika taifa letu. Tuweke ubinafsi pembeni tuwaajiri wahitimu wote mimi sidhani kama inashindikana. Sio halali mwanafunzi anapata division one ya 5 form six combination ya PCM, na chuo kikuu GPA ya 4.4 taifa linashindwa kumtumia anaamua kuwa auditor kwenye mambo ya uhasibu. Na kwa inavyoonekana ni wengi wala sio mmoja. Tunapaswa kuweka mikakati kama kuna sehemu tumefail tusisite kurudi nyuma na kuanza upya.

Lakini pamoja na kuajiriwa swala la kujiajiri kwa wahitimu wa fani yoyote ni la lazima na hicho ndio kipimo pekee cha kujua kama muhitimu alielewa darasani.

Huu ndio ukweli mhitimu ambaye hawezi kujiajiri maana yake hakuelewa darasani pengine alikua anakalili maarifa bila kuelewa.

Lakini kujiajiri kwa muhitimu kusiwe kisingizio chakutotengeneza ajira katika taifa letu. Bado sisi kama watanzania tunakazi ya kuhakikisha tunatengeneza ajira. Hicho ni kipimo cha ukuaji wa sekta yoyote. Sekta isiyoweza kutengeneza ajira maana yake imesimama kukua.

Hitimisho langu: Sekta ya mafuta na gesi imeshindwa kutimiza malengo iliyojiwekea. Imeshindwa kutengeneza ajira hasa za wahitimu wa gesi na mafuta. Waliokalia viti kwenye sekta ya mafuta na gesi bado hawajafanya kazi vya kutosha. Wanapaswa kuangalia walipoyumba na kufanya marekebisho.

Mwaka 2012 hadi 2013 makampuni ya mafuta na gesi yalijaa Tanzania na yalikua yanajaa vyuoni kuajiri wanafunzi hata kabla hawajamalza vyuo.
Kuna haja ya kubadili uongozi kwenye sekta ya mafuta na gesi ili kurudisha kasi ya kipindi cha nyuma.

Hizi ni baadhi ya hoja ambazo bunge letu lilipaswa kuzizungumzia bungeni na kuwahoji wakuu wa taasisi zinazohusika na mnyororo mzima wa sekta hii. Bunge halipaswi kukaa kimya na kukubali matokeo kasi ya sekta inapokua inashuka.
Ina maana Einstein alijiajiri kwanza?
Kujiajiri ni kipaji na pia inatokana na mipango na malezi ya wazazi.
Don't expect mtu ambaye hajui maana ya biashara ila Yuko vizuri sana kwenye engineering akajiajiri, kwanza vifaa tu ni bei kubwa sana, alaf pili, nchi yetu haina teknolojia inayoruhusu baadhi ya kozi kujiajiri.
That's the reality.
Kushindwa kujiajiri is not a measure of intelligence.
 
Biashara ya mafuta na gas iko kwenye mikono ya mabeberu na mabepari Ulaya na America huko, Sera zao ndio huamua upatikanaji au kutopatikana kwa ajira dunia ya tatu huku.

Makampuni ya mabeberu ndio mhimili wa hii biashara na ndio watengenezaji wa ajira na walipaji wa mishahara mikubwa.

Kabla ya awamu ya tano, makampuni mengi ya mabeberu yalimiminika Tanzania na kuanza kuchangamkia biashara ya vitalu pamoja na kutengeneza ajira nyingi na kulipa mishahara minono, Awamu ya Tano ya JPM ilikuja na sera iliyowaogopesha mabeberu na kuamua kufunga biashara wengi wao na kuondoka, hapa ajira za oil and gas zikafa.

USHAURI: Oil and gas inaajira nyingi sana uarabuni, Saudia, Oman, UAE, Kuwait, Qatar nk, kinachotakiwa ni vijana wetu kuzamia huko na kuzisaka fursa kwa kukubali kutaabika kwa muda ili watengeneze future kubwa binafsi, kuendelea kuwategemea wanasiasa watanzania walioshiba kuamua future yako ni kupoteza muda tu.
 
Biashara ya mafuta na gas iko kwenye mikono ya mabeberu na mabepari Ulaya na America huko, Sera zao ndio huamua upatikanaji au kutopatikana kwa ajira dunia ya tatu huku.

Makampuni ya mabeberu ndio mhimili wa hii biashara na ndio watengenezaji wa ajira na walipaji wa mishahara mikubwa.

Kabla ya awamu ya tano, makampuni mengi ya mabeberu yalimiminika Tanzania na kuanza kuchangamkia biashara ya vitalu pamoja na kutengeneza ajira nyingi na kulipa mishahara minono, Awamu ya Tano ya JPM ilikuja na sera iliyowaogopesha mabeberu na kuamua kufunga biashara wengi wao na kuondoka, hapa ajira za oil and gas zikafa.

USHAURI: Oil and gas inaajira nyingi sana uarabuni, Saudia, Oman, UAE, Kuwait, Qatar nk, kinachotakiwa ni vijana wetu kuzamia huko na kuzisaka fursa kwa kukubali kutaabika kwa muda ili watengeneze future kubwa binafsi, kuendelea kuwategemea wanasiasa watanzania walioshiba kuamua future yako ni kupoteza muda tu.
Mbona mnaruka sehemu muhimu ya mada. Nikuulize ukipata nafasi ya kushika usukani kwenye sekta ya mafuta na gesi utayajibu maswali kwa mtindo huo?
 
Acha dharau usidhani mimi navyo andika hivi nina njaa. Nipo hapa kwaajili ya kuandika na kujenga hoja. Najifunza. Kama upo hapa kwaajili ya ushabiki pole sana. Kuna siku utakuja kupiga magoti ofisini kwangu wewe nakusihi acha dharau. Soma nyuzi usifuatilie maisha yangu wala maisha ya watu wa jamii forum. Hili ni jukwaa huru. Kama huwezi kuandika kaa kimya sisi tutaandika nyuzi. Bahati yako saivi nimekua mpole. Ingekua zamani saivi tungekua tunazungumza lugha moja. Shame on you. Kalili hili jina la "Meneja wa Makampuni".
Narudia Tena, njaa itakuua
 
Nakumbuka miaka hiyo wanasiasa waliwaambia mabaharia wa kitanzania watapata ajira kwenye uchimbaji mafuta huku wakijua hakuna kozi za Offshore Practical Training nchini. Katibu mkuu ilibidi awaambie ukweli kama hujasoma kozi hizo huwezi kupata kazi, na vyuo vilikuwa South Africa
 
Nakumbuka miaka hiyo wanasiasa waliwaambia mabaharia wa kitanzania watapata ajira kwenye uchimbaji mafuta huku wakijua hakuna kozi za Offshore Practical Training nchini. Katibu mkuu ilibidi awaambie ukweli kama hujasoma kozi hizo huwezi kupata kazi, na vyuo vilikuwa South Africa

kuna kipindi wanasiasa na hata watalaam wa kitanzania huwa tunapotoshana sana.

unakuta mtu ni AB ana cheti cha STCW95 pale DMI anadanganywa atapata kazi kwenye Drill ship, jackup rig au hata hizi za exporation na kwenye operation za ROV..
Kazi nyingi kwenye Oil and gas ni proffessional's zinazohitaji proffesionals personnel wenye either experience na oil and gas operations au wenye uzoefu na kazi zenye kufanana na hizo kama watu waliofanya kazi kwenye mining field, au uchukue fresh graduates wa oil and gas, mining engineering, geologists, mechanical engineers, electrical engineers, electromechanical engineers, nk then uwatrain wafit kwenye kitu unachotaka.

Hata meli za kisasa zinataka mtu proffessional kwanza then uingie uchaguliwe kwenye area ambayo wewe unautalaam nalo, sio kama zamani unaweza kuokota mtu yeyote ukamfanya kuwa "Oiler" AB nk... dunia yasasa inataka watu proffesional zaidi kwenye marine industry na sio waogeleaji..

Hizi field kwasasa zimejaza sana Cheap labor kutoka ufilipino, India na Indonesia ambako wako wengi na ni very cheap, wachapakazi, waaminifu na wanajua kiingereza tofauti na manpower kutoka Africa ambayo inachangamoto kidogo.
 
Nakumbuka miaka hiyo wanasiasa waliwaambia mabaharia wa kitanzania watapata ajira kwenye uchimbaji mafuta huku wakijua hakuna kozi za Offshore Practical Training nchini. Katibu mkuu ilibidi awaambie ukweli kama hujasoma kozi hizo huwezi kupata kazi, na vyuo vilikuwa South Africa
Unazungumzia kozi za offshore kama zipi
 
Back
Top Bottom