Uchaguzi 2020 Ni kwanini upinzani utashindwa vibaya na CCM Itashinda kwa kishindo?

Uchaguzi 2020 Ni kwanini upinzani utashindwa vibaya na CCM Itashinda kwa kishindo?

Amani Msumari

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2016
Posts
1,830
Reaction score
972
Awali ya yote, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza ndugu Bernard Camilius Membe na ndugu wakili msomi Tundu Antipas Lissu kwa kuaminiwa na kuteuliwa kupeperusha bendera za vyama vyao katika kinyang'anyiro cha urais wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, 2020. Ni rasmi sasa watachuana na Rais Magufuli.

Uchaguzi ni uchaguzi na hakuna uchaguzi rahisi. Hatahivyo, Rais Magufuli na CCM kwa ujumla watashinda kwa kishindo. Twende pamoja:

1. Rais Magufuli na chama chake, CCM wana ajenda mahususi za uchaguzi mkuu. CCM chini ya Magufuli wanataka kukamilisha kazi kubwa waliyoianza. Hapa hapatakuwa na matumizi ya nguvu bali nguvu ya hoja. CCM wataonesha walichokifanya ndani ya miaka 5 na watawaomba watanzania waendelee kuwaamini kwa miaka 5 ijayo. Kwavile kazi imefanyika kweli na watanzania wameona, basi hakutakuwa na tabu. Upande wa pili, wapinzani hawana hoja wanayoisimamia kwa Sasa.

Naomba niwakumbushe kuwa katika nchi zinazoendelea Kama Tanzania, ajenda kubwa huwa ni maendeleo, na CCM chini ya Magufuli wamefanikiwa kwenye ajenda hii. Wapinzani wataleta ajenda ipi? Huko kupinga kila kitu? Watanzania wameamka.

2. Uimara wa vyama. CCM ni chama imara chenye mizizi mpaka ngazi ya shina. Vyama vingine vipo mijini tuu. Pamoja na rekodi yake nzuri, mgombea wa CCM ambaye ni ndugu Magufuli atabebwa na ukubwa wa chama chake, mapenzi ya wananchi walio wengi kwa CCM na ile hali ya ukweli kuwa imekita mizizi mpaka ngazi za chini.

3. Kushindwa kwa wapinzani kuungana. Kwanza niweke wazi, hata wapinzani wakiungana, bado kura zao hazitaweza kufikia kura za Rais Magufuli lakini angalau wangepata kura kadhaa. Kitendo cha kutoungana kinaonesha hawaaminiani hivyo watachafuana wenyewe kwa wenyewe na watadhoofishana kabla ya kufikia sanduku la kura. Inashangaza eti inakuwa jambo kubwa kwa mpinzani kuhamia upinzani. Yaani huu ndio ule mchezo wa sifuri kugeuza O. Wajifunze kwa mataifa yaliyoendelea. Wanahitaji wawe na chama kimoja cha upinzani chenye nguvu. Ni dhahiri ujio wa Membe utapunguza kura za CHADEMA

4. Wananchi wengi kupoteza imani yao kwa vyama vya Upinzani. Pamoja na ukweli kuwa kuunga mkono jitihada za mh Rais ni jambo jema lakini wananchi waliowachagua madiwani na wabunge wa upinzani na kuwaacha CCM walihuzunika sana kuona viongozi hao wakitimkia CCM. Sasa wengi wao wanaona bora tuu nao waunge juhudi kwa kura zao na wale wachache wanaobaki wanasema hatupigii tena upinzani kwani hawaaminiki na hatuipigii CCM vilevile. Hawa ni rahisi kuwashawishi wakaipigia CCM na ikitokea hawakupiga basi wapinzani ndio wanaopata hasara kwani wapiga kura wa CCM hawajabadilika zaidi sana wameongezeka

5. Watu wengi wanaounga mkono upinzani walisusa kujiandikisha/kuhakiki taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura. Hawa hawataweza kuwachagua viongozi wao. CCM ilifanya vizuri kwa kuhakikisha wananchama wake wamejiandikisha.

#tukutaneoktoba

Amani
 
Halafu bado naendelea kujiuliza, naomba mwenye jibu ajitokeze. Ukiishadadia CHADEMA wee mzalendo Ila ukiisemea mema CCM we unajipendekeza. Hii Ni dhambi ya ubaguzi. Hatahivyo, hapa kwangu mtasema mpaka mtabloo mafigo, katu sitaacha kuyasema mema ya Rais, serikali yake. Mimi Sina nchi nyingine. Mimi ni mtanzania halisi
 
CCM itashinda kwa asilimia zaidi ya 90. Hili halina ubishi.

LAKINI watachaguliwa (watapigiwa kura) na watu wasiozidi asilimia 10

Sababu za Ushindi

1. NEC ya kwao
2. Polisi wa kwao
3. Wakurugenzi wa kwao
4. Watendaji wa kata wa kwao
5. Ushamba wa muheshimiwa
 
CCM itashinda kwa asilimia zaidi ya 90. Hili halina ubishi.

LAKINI watachaguliwa (watapigiwa kura) na watu wasiozidi asilimia 10

Sababu za Ushindi

1. NEC ya kwao
2. Polisi wa kwao
3. Wakurugenzi wa kwao
4. Watendaji wa kata wa kwao
5. Ushamba wa muheshimiwa
Basi sawa
 
Mimi mkazi wa mkoa wa shinyanga naomba nitajiwe mambo makubwa mawili aliyoifanyia shy ili kura yangu nisimpe tundu lissu
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee
 
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee
1. Elimu bure kwa kweli ipo kwenye makaratasi tu, hili ili lieleweke vizuri lingisemwa hivi magufuli karuhusu watoto wa wanyonge kwenda kuzurura na kushinda bure ktk majengo ya serekali yanayoitwa shule, wazazi wanahaha kuzibua vyoo na kuchoma mahindi ili wapeleke watoto shule za private wakapate elimu ya kweli
 
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee
2. Ujenzi wa barabara kwa kungwangua kwa magreda na kuyaacha hivyo hivyo kwa hilo nampongeza kajitahidi ila wanashy nasisi tunataka barabara kama chato
 
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee
3. Majengo yanayoitwa zahanati kwa kweli yapo tangia utawala wa kikwete na hayana madaktari wala wauguzi ngazi za manesi kama ni huduma za kutalii majengo ya zahanati pongezi nazipeleka kwa kikwete ila kwa upande wa quality zile zahanati ni majengo bila huduma
 
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee
4. Usambazaji umeme hizi credit kwa kweli ziende tu kwa mkwele asilimia 90 ya umeme shy kasambaza kikwete so kwa porojo zako hizi sisi wanashinyanga kwa pamoja kura zetu tunampa tundu lissu
 
Sera za Chadema.. ni vitukwo..
1. Wahujumu uchumi.. na mafisadi.. wasisote jela.. 😃😃😃
2. Wagonjwa watibiwe.. walipe bili.. wakipata fedha.. na 😃.. hata ikiwa miaka 10 baada..
3. Kila ukanda utakuwa.. waziri mfano wa Pamba.. Ndizi.. Kahawa.. Samaki.. 😃😃😃 sio Waziri wa Kilimo.. wa nchi nzima.. yeye ajue kila kitu.. 😃😃😃..
Nchi itakuwa.. na mawaziri hata 100.. wote wale.. matumbo kwanza..
4. Hawata kuuliza wananchi tena.. katika ya Warioba.. itatumika.. 😃😃😃 hawa mabomu hawajui.. dunia haisimami.. wavivu kudandia ya CCM.. miaka ile.. siwo ya sasa..
5. Watafita sheria zote zilizopo.. maelfu kwa maelfu..
6. Ati uchumi haupandi sasa.. wao wamesaidiaje.. kubadili.. wabunge walikuwa nao Bungeni..

Chadema muna ndoto za ajabu.. hamutafanya lolote munalisema.. hamuna uwezo.. munataka kwanza muongoze wengi.. mule mule tu..
😃😃😃kwa kweli.. muvizie tu kura za huruma.. za wasiojitambua..

Magufuli 2020
 
1.Elimu bure kwa watoto wetu kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha 4.
2. Ujenzi wa barabara

Bonus points
3. Ujenzi wa vituo vya afya
4. Uimarishaji wa usambazaji wa umeme vijijini

Naomba watu wa Shytown wamuongezee

Yamefanywa na utawala wa Magufuli.
 
Chadema.. hawana vya dijitali.. eti wataqeka ya wananchi wanunue hisa.. kiganjani.. hata wa vijijini.. uchumi ukue..😃😃😃😃 vituko vya kuwemo.. ndani ya futi sita.. ndotooooo
 
Kuna mshenzi mmoja na chama chake nasikia wanataka kuingia barabarani
 
Back
Top Bottom