Ni kwanini watu wenye pesa wakiwa na shida huwa kimbilio lao kwa masikini na kuwasumbua?

Ni kwanini watu wenye pesa wakiwa na shida huwa kimbilio lao kwa masikini na kuwasumbua?

Bata batani

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2011
Posts
3,217
Reaction score
3,694
Kuna vitu huwa najiuliza watu wengi wakiwa na pesa hujitenga sana na watu masikini tena hawa masikini hata wakiwatafutaga huwa simu zao hazipokelewi lakini sasa inapotokea watu wenye pesa wana shida basi kimbilio lao la kwanza ni kwa watu masikini.

Yaani unashanga mtu kipindi ana pesa alikuwa hana muda na wewe masikini ila leo hii baada kuwa na shida ndio anakukumbuka anaanza usumbufu mara ohooo muda wote anataka muwe mnaongozana, mara kila ukikutana anakusimulia matatizo yake, mara anataka umsindikize mahakamani sijui ana kesi na kampuni, mara aanze kukulamikia kuhusu kutegwa na watu wake wa karibu sababu ana shida yaani mambo kibao na matatizo kibao anakuletea wewe masikini.

Sasa ndipo najiuliza why wanakimbilia kwa watu masikini hao wenye pesa wenzake wako wapi waliokuwa wakila na kula bata pamoja asiwashushie mashida yake kuwaelezea.
 
Mi huwa hata salam siwapi...kama walivyokuwa wanakausha
 
Kuna vitu huwa najiuliza watu wengi wakiwa na pesa hujitenga sana na watu masikini tena hawa masikini hata wakiwatafutaga huwa simu zao hazipokelewi lakini sasa inapotokea watu wenye pesa wana shida basi kimbilio lao la kwanza ni kwa watu masikini

Yaani unashanga mtu kipindi ana pesa alikuwa hana muda na wewe masikini ila leo hii baada kuwa na shida ndio anakukumbuka anaanza usumbufu mara ohooo muda wote anataka muwe mnaongozana , mara kila ukikutana anakusimulia matatizo yake,mara anataka umsindikize mahakamani sijui ana kesi na kampuni, mara aanze kukulamikia kuhusu kutegwa na watu wake wa karibu sababu ana shida yaani mambo kibao na matatizo kibao anakuletea wewe masikini

Sasa ndipo najiuliza why wanakimbilia kwa watu masikini hao wenye pesa wenzake wako wapi waliokuwa wakila na kula bata pamoja asiwashushie mashida yake kuwaelezea
Yule mheshimiwa sana wa nchi alisemaga akili zako changanya na za kuambiwa.Tajiri akifiwa hata kama ana hela hawezi chimba kaburi au basi hata akisema akodi watu wamchimbie hataweza kuzika mwenyewe na hata akikodi watu wakuzika kwenye matanga atakaa na nani lazima amuhitaji masikini amsaidie kulia.Tajiri ana kila kitu lakini ukimuambia sindano ya kushonea nguo lazima atakwenda kumuomba masikini.Tajiri akiona amefilisika wenzake walicho nacho watamkimbia kumuogopa asiwapige mizinga lakini kimbilio lake ni masikini hawezi mnyanyasa atamfariji.
Nenda kwa tajiri unaweza kuta hana hata jembe anajua jirani yake masikini hawezi kukosa au basi hata kibanio cha kubania mkaa baada ya umeme kukatika mkewe akaamua kupikia jiko la mkaa.Tajiri gari lake likizimika kwenye dimbwi la maji atamuhitaji masikini amsaidie kulisukuma maana suti yake itachafuka.Hii inaitwa symbiosis yaani kufaana.Gari likiwa chafu tajiri anaoshewa na masikini tajiri anafarijika na masikini anapata hela yake.Mfano yule ndege anayekaa juu ya mgongo wa mnyama nyati anafaidi kula kupe wa juu ya mgongo wa nyati nyati naye anafaidika kutolewa kero ya wadudu.Hali kadhalika mamba huwa hatafuni anapokula meno yake yanakuwa na mabaki ya nyama anapanua mdomo kuna kindege kinakuja kinaingia hadi mdomoni kumsaidia kutoa nyama zilizonata kwenye meno ajabu mamba huwa hamdhuru hata siku moja
Duniani tunategemeana ndivyo mungu alivyotuumba
 
Duniani tunategemeana Kama ilivyo ecosystem.
 
Back
Top Bottom