Ni kweli Cleopatra, mwanamke mrembo kuliko wote duniani alikuwa wa Misri?

Ni kweli Cleopatra, mwanamke mrembo kuliko wote duniani alikuwa wa Misri?

Baadhi ya picha zinazosadikika za Cleopatra!
Sakayo Numbisa Gentries @kagadala1 Sky Eclat
ancient-beauty-secrets.jpg
 
Mwanaume mzuri kuliko wote ni nabii yusuph.
Mwanamke mzuri kuliko wote ni mjukuu wake nabii yusuph.jina lake rahma kama ntakuwa sijakosea.
 
mjingamimi mkuu yaweza kuwa,ila mimi nimeelezea katika mlengo wa kibiblia,kama hautojali ebu zilete picha tupate kujifunza zaidi!
 
Childhood diplomacy hongera mpendwa,ila Cleopatra alikuwa mzuri kwa kuwa na mvuto mzuri wa kimapenzi,japo alikuwa na roho mbaya iliyojaa ulafi wa madaraka,tamaa na uaji!
 

Inasadikika kuwa huyu ndiyo mwanamke mzuri kuliko wote katika historia ya dunia.


Ametajwa katika vitabu kadhaa ikiwemo Biblia na aliishi kwa miaka 39.


Cleopatra alikuwa ndiyo mtawala wa mwisho wa Kigiriki kutawala Misri na ndiyo aliyekuwa Farao
wa Kwanza wa kike mgeni.


Alizaliwa mwaka 69 na akiwa na miaka 18 akatawazwa kuwa Malkia.


Cleopatra ni neno la Kigiriki linalomanisha "baba yangu ni maarufu"
Cleopatra ni jina walilolopewa
mabinti kifalme wa kigiriki huku wale wa kiume wa kifalme
waliitwa Ptolemy.


Ptolemy alikuwa ni mmoja wa wale majenerali wanne wa
Alexander Mkuu,ndiyo hawa waliougawa ufalme wa Alexander katika falme nne!


Ptolemy ndiye aliyeanzisha utawala wa Kigiriki Misri na mji
wa Alexandria ndiyo ukawa makao makuu ya ufalme wake.


Hivyo Cleopatra huyu
tunayemzungumzia hapa
alikuwa ni Cleopatra wa Saba na wa mwisho.
Dola la Misri lilitawaliwa na Ugiriki tangu mwaka 323 baada ya Alexander Mkuu kuishinda Misri na utawala huu uliisha
mwaka 30 baada ya Cleopatra kujiua kwa kumruhusu nyoka
aina ya Cobra kumgonga kifuani.


Cleopatra alikuwa na mahusiano na wanaume wengi ila wale maarufu walikuwa ni Julius Caesar na Mark Anthony huyu
Caesar ndiye ambaye walizaa naye mtoto mmoja wa kiume.


Baada ya kifo cha Julius Caesar mwaka 44 mapenzi yakahamia
kwa Mark Anthony mnamo mwaka 42
Ili kuweza kutawala pekee yake Cleopatra alifanikiwa kuwaua wadogo zake wote,na
pia aliutumia uzuri wake kupata ulinzi wa kijeshi kutoka majemedari mashukhuri wa kipindi hicho!


Mathalani,kuna kipindi akiwa binti mbichi wa miaka 21 aliwaagiza watumishi wake wamviringishe kwenye zuria zuri na kulibeba kama zawadi na
kulipeleka kwa Julius Caesar!


Julius Caesar alipolifunua
akakutana na Cleopatra na hapo hapo akamfanya Cleopatra mchepuko wake.


Mark Anthony na Cleopatra walijiua baada ya kushindwa kwenye vita ya Actium na Octavian!


Huyu Octavian ndiye mtawala alietoa
amri ya Wayuhudi wote kwenda walikozaliwa wahesbiwe Sensa!


TUNAJIFUNZA NINI?


Uzuri,pesa,mali,na madaraka yatarahisisha maisha yetu ya duniani,ila hayotukufikisha mbinguni.


Ni kumtegemea Mungu tu ndiyo kutatufikisha mbinguni!


REFERRENCES:


1 Makabayo 10:57-58
Daniel 11:12
Luka 2:1-7
Antiquities of Jews by Josephus
Cleopatra and Anthony by
Shakespeare


ANGALIZO:
Miaka yote ni Kabla ya Kristo.

Kuna series moja inaitwa ROME. imedepict kila kitu kwa details. Kama unapenda history za hawa jamaa, unaweza kuitafuta extratorrent.ag
 
Back
Top Bottom