Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.

View attachment 3173753
Tatizo mmekariri Hilo dude la mwisho PhD Bioregulatory medical science ndio kila kitu ni zaidi ya hizo Mmed au wenyewe mnaita specialist ..
 
Mwalimu wa biology hapa Tanzania mwenye degree anaweza kusoma masters of science in urology kwa mujibu wa comment uliyoandika?
Hebu Usinifanye Nicheke ndugu yangu Ndo maana Nimeanza na Afya..Mkuu Kwenye Hiyo comment..

Ila Ukizungumzia Urology kwa Tz Ni Super Hiyo Haingiwi Kichwa kichwa Mpaka Uwe Umesoma MMED ya Internal au Paed..

Usione ina Msc basi ukajua Ni Kwenye zile nilizozungumzia MSc na MMED..
Msc ya Urology ni Ubingwa Bobezi
 
Sasa kama MCT haimtambui kama Daktari aliwezaje kufanya kazi kama Daktari Bingwa Siku zote hizo? Mbona kama hii Mifumo inatuvuruga? Sasa ni wangapi wana hii changamoto na mmeekaa kimya?

Pili kama ndani tu wataalamu wenzake mmeanza kumkataa huko nje ataenda kushindana na nani? Reference point tayari imegoma????

Tatu wataalamu wenzake mnasema hata u Profesa wake haujulikani ni wa CHUO gani na nime google kweli sijaona!! Sasa hii inakuwaje mkapeleka CV kwa Rais ambayo ina utata na duniani kote macho yapo kwenye hii vurugu mliyoleta!

Nne kama hana MMED aliwezaje kutufanganya kwenye social media kuwa amewafundisha madaktari kadhaa hapo MUHAS?? This is confusing and shame kwa nchi!

Mwisho! MWENYE CV YA MTITIRIKO WA MIAKA NA QUALIFICATION KUANZIA SHULE YA MSINGI TUNAOMBA ALETE!! Tusije kusikia hata Uraia wake una mashaka!!

Nasubiri majibu nichangie zaidi!

Queen Esther
🤣🤣 Duuh!

Hebu ngoja wataalamu watujuze. Mwenyewe napata utata hapa.

Maana hapa Bongo elimu za mchongo ni nyingi sana.

Unayemuona ni mtaalamu kumbe na yeye ni wa mchongo.
 
Sio nakupiga kamba, nenda popote katika hii nchi kaulize madaktari watakwambia hichi kitu.
Mhitimu (fresh from university) wa udaktari wa binadamu (Md) aliyehitimu USSR ya zamani, Russia ya sasa, Ukraine, China au India hana uwezo kamili wa kutibu mgonjwa kumkaribia mhitimu wa hapa Tanzania hususani kutoka Muhimbili. Na siri ni moja tu, daktari mwanafunzi, tena mgeni kutoka afrika, halafu mwenye ngozi nyeusi hawezi kupewa nafasi kamili ya kujifunza kwa kutibu (clinical practice) kwenye mwili wa mzungu (mrusi), mchina au mhindi.
Hili ni kweli kabisa,nimeshuhudia haya.
 
Nakusahihisha.
Professor Janabi alifanya Msc in Tropical health (ambayo mhitimu yoyote wa kada ya afya anaweza kufanya, sio lazima awe Md) na hakufanya Mmed of Tropical medicine.
Msc of tropical health sio sawa na Mmed.
Mimi kilaza wa mambo ya afya naomba nikuelewe hivi mkuu:

1. Msc ya Tropical Medicine sio kigezo sahihi kinachohitajika kwa daktari kwenda ngazi ya kuja kubobea magonjwa ya moyo. Msc hiyo ni hafifu, hata Degree holder wa Pharamacology anaweza soma.

2. Ili mtu akasomee kuwa Cardiologist inabidi kwanza asome Mmed, na sio Msc.

Lakini kwa maelezo ya DR Mambo Jambo ambayo nilichanganya nikadhani Prof. Janabi ana Mmed ya Tropical Medicine kumbe ana Msc ya Tropical Health, je mtu mwenye Msc hiyo (badala ya Mmed) naye ana sifa za kubobea kwenye cardiology?

Wakuu kumbuka mwanzoni hoja ya ndugu Zanzibar-ASP ilikuwa Prof. Janabi hana Mmed ya Internal Medicine hivyo hana sifa. Kwahiyo nikataka kumtetea kuwa hana Mmed ya Internal Medicine ila ana ya Mmed ya Tropical Disease, sasa nazidi kuambiwa pia hana hiyo Mmed bali ana Msc ya Tropical Health.

Nimerudi kwenye CV yake naona MD, Msc. PhD.
Kwahiyo ndugu DR Mambo Jambo nakuuliza tena, Msc ya Tropical Health ya Prof. Janabi inafaa kuwa mbadala wa Mmed ya Tropical Medicine. Ili Zanzibar-ASP aridhike?

Update: Nimekuja kujua hapa kupitia kwa DR Mambo Jambo kuwa Mmed ile ni (Internal medicine Specified In Tropical Medicine). Mwanzoni nilijua Internal Medicine na Tropical Medicine ni vitu viwili tofauti, mnaandika kwa kifupi sana nyie waganga.
 
Hapana Mkuu!
Janabi kafanya vyote..
Janabi kasoma MD, Mmed (Internal medicine Specified In tropical Medicine)

Kaja Akafanya Fellowship ya Cardiology Na akafanya reseaexh na study kibao mpaoa Kufikia Alipo We Jiulize Fellowship alifanya mwaka 2001 kama sijakosea sana Sasa Mpaka Leo study ngapi kafanya..

Mleta mada ana Chuki binafsi na Janabi nimewahi kueleza Humu kuhusu Janabi tangu mwaka jana
Asante mkuu.
Mchangiaji hapa anadai Prof. ana Mmed ya Internal Medicine Specified in Tropical Medicine.

Mleta mada ndugu Zanzibar-ASP umedai Prof. Janabi hana Mmed bali ana Msc ya Tropical Health. Mleta mada unaamini uko sahihi na data zako?
 
kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.
Hivi wewe kwa akili yako, kuna chuo kikuu hapa kwetu ambacho kinaweza kumpa mtu cheo cha mhadhiri (lecturer) na mtu huyo akapanda vyeo hadi kuwa profesa, bila kuwa na elimu ya MMed or equivalent? Yaani unaamini chuo kikuu chetu cha udaktari (MUHAS) kilifanya hivyo kwa Dr Janabi? Kama ni hivyo basi kinapaswa kufutwa kwenye orodha ya vyuo vikuu nchini na duniani.

Tatizo lako ni kwamba hujui kuwa MMed ni equivalent to PhD degree. Terminology ya MMed ni ya hapa kwetu tu, kwingineko duniani hakuna neno kama hilo, kuna PhD tu.
 
Hoja ya Mleta mada siyo kwamba Prof hajasoma bali Prof hajasomea na hana Udaktari Bingwa wa Moyo kama ambavyo anatambulika kwa kuwa hajasoma Mmed (Masters of Medicine) in Internal Medicine kwanza kabla ya hiyo Fellowship ya Moyo kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Unajua zamani au mpaka sasa vijijini, hata waliosoma Clinical Officer au Assistant Medical Officer, wanaitwa nankujulikana Madaktari (kwa maana ya Medical Doctor) ilhali hawana/hawajasoma Degree of Medicine.


Ni vizuri tujaribu kumuelewa Mleta Hoja, na kujibu Hoja zake kwa ufasaha. Tuepueke mihemuko kisa anayeongelewa ni Prof.
Nimetoka kuongea na mchepuko wa mdogo wangu mmoja hupo huko Utete,Rufiji, anaitwa dokta wakati yeye ni mgawa "mbaazi".

Ameongelea hili swala la watu kuwaita madokta wafanyakazi wote wa hospotali/zahanati.
 
Hivi wewe kwa akili yako, kuna chuo kikuu hapa kwetu ambacho kinaweza kumpa mtu cheo cha mhadhiri (lecturer) na mtu huyo akapanda vyeo hadi kuwa profesa, bjla kuwa na elimu ya MMed or equivalent? Yaani unaamini chuo kikuu chetu cha udaktari (MUHAS) kilifanya hivyo kwa Dr Janabi? Kama ni hivyo basi kinapaswa kufutwa kwenye orodha ya vyuo vikuu nchini na duniani.
Inategemea unafundisha nini, kuna wengine si MD lakini wanafundisha MD hapo MUHAS.
 
Hivi wewe kwa akili yako, kuna chuo kikuu hapa kwetu ambacho kinaweza kumpa mtu cheo cha mhadhiri (lecturer) na mtu huyo akapanda vyeo hadi kuwa profesa, bila kuwa na elimu ya MMed or equivalent? Yaani unaamini chuo kikuu chetu cha udaktari (MUHAS) kilifanya hivyo kwa Dr Janabi? Kama ni hivyo basi kinapaswa kufutwa kwenye orodha ya vyuo vikuu nchini na duniani.

Tatizo lako ni kwamba hujui kuwa MMed ni equivalent to PhD degree. Terminology ya MMed ni ya hapa kwetu tu, kwingineko duniani hakuna neno kama hilo, kuna PhD tu.
Kwani Muhimbili wanafundisha Medicine tuu hakuna programme zingine anazoweza kufundisha?

Na je kwani hata hao wa Medicine si kuna masomo ya biomedical science anaweza kufundisha. Kuwa
lecturer Muhimbili haimpi uhalali wa kuwa na MMED Internal Medicine.
 
Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.

View attachment 3173753

Hiyo picha ni kabla gajaanza kunywa supu ya mchicha kama breakfast...?
 
Hii Elimu yake inatusaidia nini kwa Kipindi hiki?

Jambo la Msingi aungwe Mkono.

Huu Upuuzi wa Elimu umebakia sana hapa kwetu Africa Mashariki.

Huko kwa Mabeberu kinachoangaliwa ni Uwezo wako Ku deliver.

Tuachaneni na Hizo mambo za Kuangalia Elimu , hazilijengi Taifa.

Mabeberu gani wanatoa kazi ya maana kwa mtu asiyekuwa na elimu?

Hospital gani imeajiri daktari asiye na elimu eti kisa ana uwezo?

Uwezo na elimu vinaenda sambamba acheni kujifariji. Unataka WHO iendeshwe na mtu asiye na elimu eti kisa ana uwezo haiwezekani.

Wewe unaweza kubali ufanyiwe operation ya kichwa au yeyote ile na mtu asiye na elimu hiyo kisa tu umeambiwa ana uwezo?

Mambo ya uwezo yaishie kwa fundi juma na fundi maiko wanaoangusha majengo. Mambo ya msingi yaendeshwe na watu wenye elimu ya kutosha na ujuzi.

Ungejua medical field ilivyo over-regulated usingeongea huu utopolo. Naamini Janabi ana vigezo vyote nontheless.
 
Hii Elimu yake inatusaidia nini kwa Kipindi hiki?

Jambo la Msingi aungwe Mkono.

Huu Upuuzi wa Elimu umebakia sana hapa kwetu Africa Mashariki.

Huko kwa Mabeberu kinachoangaliwa ni Uwezo wako Ku deliver.

Tuachaneni na Hizo mambo za Kuangalia Elimu , hazilijengi Taifa.
Kamanda mbona umeandika kinyume, hiyo nafasi inahitaji mtu mwenye elimu, wewe unasema tuachane na mambo ya kuangalia elimu. Utakua director wa WHO bila kuwa na elimu(mtaalamu wa hilo eneo)?

Hiyo sio nafasi ya mkuu wa mkoa au wilaya. Hiyo ni nafasi ya wenye elimu
 
Mimi kilaza wa mambo ya afya naomba nikuelewe hivi mkuu:

1. Msc ya Tropical Medicine sio kigezo sahihi kinachohitajika kwa daktari kwenda ngazi ya kuja kubobea magonjwa ya moyo. Msc hiyo ni hafifu, hata Degree holder wa Pharamacology anaweza soma.

2. Ili mtu akasomee kuwa Cardiologist inabidi kwanza asome Mmed, na sio Msc.

Lakini kwa maelezo ya DR Mambo Jambo ambayo nilichanganya nikadhani Prof. Janabi ana Mmed ya Tropical Medicine kumbe ana Msc ya Tropical Health, je mtu mwenye Msc hiyo (badala ya Mmed) naye ana sifa za kubobea kwenye cardiology?

Wakuu kumbuka mwanzoni hoja ya ndugu Zanzibar-ASP ilikuwa Prof. Janabi hana Mmed ya Internal Medicine hivyo hana sifa. Kwahiyo nikataka kumtetea kuwa hana Mmed ya Internal Medicine ila ana ya Mmed ya Tropical Disease, sasa nazidi kuambiwa pia hana hiyo Mmed bali ana Msc ya Tropical Health.

Nimerudi kwenye CV yake naona MD, Msc. PhD.
Kwahiyo ndugu DR Mambo Jambo nakuuliza tena, Msc ya Tropical Health ya Prof. Janabi inafaa kuwa mbadala wa Mmed ya Tropical Medicine. Ili Zanzibar-ASP aridhike?

Update: Nimekuja kujua hapa kupitia kwa DR Mambo Jambo kuwa Mmed ile ni (Internal medicine Specified In Tropical Medicine). Mwanzoni nilijua Internal Medicine na Tropical Medicine ni vitu viwili tofauti, mnaandika kwa kifupi sana nyie waganga.
Tatizo Kubwa Linakuja kuwa Muundo wa Afya Tanzania Hautambui Mchanganyiko ama Course inayoitwa MMED (Internal Medicine Specified In Tropical disease) ila wanaitambua tu ni Kama MSc In Tropical D'se..
Kitu ambacho kwa Tanzania Kinampa Ubingwa Kwenye Tropical Disease Peke yake na wala Hakumpi Ubingwa kwenye Magonjwa yote ya Ndani..

Kwa Tanzania (Muundo ma kanuni za MCT) Atakosa Sifa ya Moja kwa Moja Kusoma Fellowship ya Cardiology ila kwa Nje Anayosifa Hiyo kwa kuwa wanatambua Course hiyo..

Shida Kubwa ni Muundo Maana Tanzania Hawaitambui kama MMED inakosa Sifa Kuwa MMed ila Wanaitambua kama MSc..
 
Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.

View attachment 3173753
Muulizieni mpendwa mstaafu wetu 😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom