Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Hapa tunazungumzia sifa za kuwa daktari bingwa mbobezi kwa kanuni, taratibu na sheria za baraza la madaktari la Tanganyika (MCT), standard za MCT zinashahabiana mnoo na nchi nyingi za Africa zilizopiga hatua kwenye fani ya utabibu kama Kenya, Ghana, Nigeria, South Africa. Huna Mmed ya internal medicine huna sifa za kusomea ubobezi wa moyo. Na kwa ubingwa ubobezi wa watoto, huna Mmed ya watoto (paediatric) huna ubobezi wa moyo.

Kwa nchi zilizoendelea sana kama USA, UK, Germany, France, Canada mziki wa kuwa Daktari bingwa wa moyo ni mchakato mrefu, mpana na mzito. Kwa alichosomea Professor Janabi huko anaweza kuishia masijala tu akihifadhi kumbukumbu za taarifa ya wagonjwa.
Ila humu ndani heti masijala
 
Aliye juu hashushwi kwa uchawi wa hivi mazee! We ulosomea ubingwa unaumia ukiwa wapi? Eti umeingia chimbo, hahaha hawa ndo wabongo! Bado hatujaappreciate juhudi za mtu na bahati zake zinamfikisha alipo sio makaratasi ya jalalani! Ni ngazi tu ya kupandia
Mkuu hoja hujibiwa kwa hoja sio misemo! Anayoyasema mtoa mada yameandikwa na tovuti ya chombo kinacho watathmini na kuwapima madaktari wetu na watoa huduma za kiafya ….wao ndio wanasema Prof Janabi si daktari bingwa wa magonjwa ya moyo….tulikuwa tunajidanganya!

Jibu hoja sasa
 
Hilo dude (Phd Bioregulatory medical science) ndio uchafu mtupu, ndio maana hata yeye mwenyewe Janabi kaogopa kabisa kuliweka kwenye CV yake aliyoileta soon mitandaoni baada ya wakuda kumchana live, kwa sasa anasema hajasomea hilo badala yake kasomea Phd ya Cardiology! Sasa MCT wamemuumbua kwa kumkana, wanasema Phd yake ni ya hilo dude ambalo halihusiki popote kutibu mgonjwa, sembuse mgonjwa wa moyo.
Kwa hiyo hapa MCT ndio wamemwagia upupu aiseee….kusema kweli mimi nilikuwa najua ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo
 
Mkuu hoja hujibiwa kwa hoja sio misemo! Anayoyasema mtoa mada yameandikwa na tovuti ya chombo kinacho watathmini na kuwapima madaktari wetu na watoa huduma za kiafya ….wao ndio wanasema Prof Janabi si daktari bingwa wa magonjwa ya moyo….tulikuwa tunajidanganya!

Jibu hoja sasa
Kwani anatibu huyu? Yani liuzi reeefu kutafuta namna ya kumshusha mtu tu! Anataka degree ya clinical ya nini sasa wakati ni manager? Na hata kama hana so what? Kaua ntu? Wabongo roho za korosho tu, sina haja ya kujibu huu upuuzi! Madaktari wa kibongo wana kiburi sana cha kuamini wana akili kupindukia sijui kwa kuwa wamekaa chuo miaka mingi zaidi? Wizara ya afya na taasisi zake ni ngumu sana kufanya transformation kwa sababu za huu ujinga wa kuamini hamna mtu anaweza kuwaongoza, wakati hata kujiongoza tu hawawezi zadi na majungu na uchawi, ukianzia kwa madmo panda juu ni ujinga tu mara MMed, Mph, Superspeciality so what?

MOI alikuwepo mswiss miaka fulani wakajiorganize na kumfukuza kama mbwa, just kwa kuwa ni manager na hana clinical education! Pathetic
 
Weka ushahidi hapa kuwa hana i.e:-barua ya chama cha madaktari ikimkana Janabi
Uwe unasoma vizuri na kuelewa! Kwa nchi yetu kuna vyombo maalum vya kutambua na kutathmini taaluma za watu na kwa afya kimojawapo ni MCT na hao ndio wanataarifa za madtari wetu wote na kulingana na wenyewe MCT kupitia tovuti yao hakuna mahali Dr Janabi anatambulika kama Daktari bingwa wa moyo …kwa hiyo MCT hawamtambui kama tunavyomjua sisi na MCT ndio wasema kweli hakuna siasa pale na alichofanya mtoa mada ni kutuhabarisha tuu
 
Kwani anatibu huyu? Yani liuzi reeefu kutafuta namna ya kumshusha mtu tu! Anataka degree ya clinical ya nini sasa wakati ni manager? Na hata kama hana so what? Kaua ntu? Wabongo roho za korosho tu, sina haja ya kujibu huu upuuzi! Madaktari wa kibongo wana kiburi sana cha kuamini wana akili kupindukia sijui kwa kuwa wamekaa chuo miaka mingi zaidi? Wizara ya afya na taasisi zake ni ngumu sana kufanya transformation kwa sababu za huu ujinga wa kuamini hamna mtu anaweza kuwaongoza, wakati hata kujiongoza tu hawawezi zadi na majungu na uchawi, ukianzia kwa madmo panda juu ni ujinga tu mara MMed, Mph, Superspeciality so what?

MOI alikuwepo mswiss miaka fulani wakajiorganize na kumfukuza kama mbwa, just kwa kuwa ni manager na hana clinical education! Pathetic
Wewe ulikuwa unamtambuaje Prof Janabi?
 
Wewe ulikuwa unamtambuaje Prof Janabi?

Ni manager na mshauri wa rais wa mambo ya afya tu inatosha nimtambue vipi zaidi? Elimu iliyomfikisha hapo haina tija so long as yupo effective na anadeliver sawasawa!
 
Daktari yoyote anaweza na anaruhusiwa kutibu moyo popote, lakini linapokuja suala la kutibu moyo kwa ngazi ya kibingwa ni daktari bingwa pekee mwenye hayo majukumu.

Ukiona Daktari ambaye sio bingwa anatoa matibabu ya kibingwa basi ujue anafanya hivyo chini ya usimamizi wa daktari bingwa. Tofauti na hapo ni makosa.

Nakuhakikishia kwa 99% kwa elimu ya kutibu moyo aliyonayo Janabi (ya kawaida mnoo) tukisema akae pale JKCI kutibu moyo yeye mwenyewe (bila kusimamiwa na madaktari bingwa waliopo pale) huenda atapaswa kuishia kumpima mgonjwa presha na mapigo ya moyo tu, kwa sababu hana sifa za kutibu moyo kibingwa.
Whata punch
 

Attachments

  • FB_IMG_1733128812738.jpg
    FB_IMG_1733128812738.jpg
    17.4 KB · Views: 3
Unaujua kwa kina ufahamu wake wa hiyo fani ya kutibu moyo?. Uzoefu alionao kwenye hiyo fani unaweza kuulinganisha na wa watu wengine baki tu?.

Huu uzi umekaa kichuki zaidi umekaa kiroho mbaya kuliko uhalisia. Huyo mleta mada mbona haweki hadharani sifa zake za kielimu ili tumjadili kwa kina?.
Mleta mada kama katumia sehemu CV ya "urongo" sehemu Naye atalimwa, lakini ukiona hajafanyiwa hivyo basi sio "mrongo"
 
Ila watanzania kwa wivu hamjambo na kujifanya mnajua...kumbe mna degre moja tuu ya MD.....
 
Back
Top Bottom