Ni kweli Papa Wemba kauawa na sumu iliyowekwa kwenye Mic?

Ni kweli Papa Wemba kauawa na sumu iliyowekwa kwenye Mic?

Ni kweli aliugua na kulazwa mda mrefu. Bendi yake ilikosa dili na wanamuziki wake walikuwa hali mbaya kifedha kipindi cha ugonjwa wa Papa wemba. Katoka hospitali tu akapewa hiyo shoo na akaenda kupiga. Bado alikuwa mgonjwa.

Kutoa kipaza sauti sio ishu, watu wanapata ajali na badala ya kusaidiwa wanavuliwa mpk nguo, sembuse kubadilisha au kuondoa mic stejini?

Yule jamaa alisogeza mic na stend yake Kuongeza nafasi tu kwa watu wa huduma ya kwanza kufanya kazi.
Tena afadhali yeye aliyesogeza mic pembeni kuliko waliojazana kumzunguka marehemu na kuzidi kumkosesha hewa pale stejini.
 
He was sick
Nikweli yani anaonekana kabisa analazimisha hapo stage....inasikitisha sana, ametutoka akifanya kile alichokua akikipenda maisha yake yote, kuimba na kutoa burudani kwa fellow human beings wacheze waburudike wasahau stress za maisha kwa muda, and make more money. RIP
 
mkuu hii intelejensia yako huenda ikawa kweli maana haiwezekani mtu adondoke chini hiivi hivi bila sababu.
 
Umeona eeh! Pilika za jamaa zinaonekana 3 times, 1.Akija kutoa Mic ambayo Papa Wemba alikua anatumia, Na Ni baada Tu ya Papa Wemba kusogea mbele kuongea Na Mashabiki... 2.anaileta Stand Na Mic nyingine... 3.anakuja kuondoa Ile mic aloileta baada ya papa wemba kuanguka! Na unaona wakati watu wote wanahangaika Na Papa aliyekua kalala chini, yeye peke yake anaonekana akijishughurisha Na kuondoa Ile mic
huyo mtu mwenye kuhangaika na mic ni JIPU!
 
Masikini papa wemba sijui atamueleza nini mungu wake,kafia katikati ya tope la shetani kafa kazungukwa na wanenguaji waliovaa vichupi,tusimsahau mungu jamani
 
Kuna kitu kinaitwa autopsy, nadhani kwa kifo cha ghafla hivi hii autopsy hufanyika na ndio hueleza sababu ya kifo mfano kifo cha prince majuzi, na sio video. Ni kweli huyo aliyeleta mic haeleweki vizuri.. Ila kwa sumu kumuua papa wemba gafla pale ni lazima iwe kali sana (very strong and powerful dose) kiasi hata huyo mbeba mic ingemuathiri tu na hata waimbaji na wachezaji walio kua karibu pale na pia kumshika.

Naamini sumu ya hivyo kama ni biological nilazima papa wemba mwili ungeonyesha kuathirika nahata kwa namna yoyote ile kama kuvuja damu, kubadili ka mwili rangi au kubabuka, nahali hii ingewapata pia waliomsogelea na kumshika sababu hiyo sumu imemuingia papa kwa kuvuta hewa if that is the case.

Pia kama waliweka chemical za kutoa miale ya sumu (radio active materials), kumuua pale gafla nilazima wale walio mkaribia, na jamaa aliyebeba mic wataathirika maana hata yeye hakua na protective gears kuziba mikono au pua.

Hicho kifo hapo nadhani ni stroke kubwa au ugonjwa wa moyo (heart failure)......umri na fatigue vinajionyesha hapo dhahiri, anaonekana kabisa ana struggle kutoa sauti na kucheza....hiyo shuguli hapo stage huwa ni pevu hata vijana wenye afya zao huanguka.

Ni mtazamo wangu tu. Ila autopsy ndio yakusema ukweli....video itasaidia ushahidi wa kimazingira tu.
Mkuu umeelezea vizuri sana,Big up Mkuu.
 
Jamaa anamletea PW Wireless Mic katika stand (Pengine ilikuwa na sumu Tayari) Baada ya Muda Jamaa yuleyule anakuja na Kuchukua ile Mic na kutokomea nayo (Pengine alihisi sumu haitoshi akaenda kuongezea Dose) Jamaa anakuja na Mic ikiwa Vilevile kwenye stand, Anamwekea PW, halafu anaondoka kuelekea alikotoka. Muda Mfupi PW anaanguka ghafla, Watu wanamzunguka kusaidia. Jamaa yuleyule anatokeza tena. Cha kwanza Badala hata ya Kushangaa, au hata kwa Udaku tu kuinama na Kujua PW yupo katika hali gani, Yeye Bila Kustushwa anachukua Mic ile tena, Anasogea Kidogo, anacheki Noma! Kisha anatokomea Nayo. Mwanzo Unaweza Kusema Kuwa labda Kuisogeza Mic Pembeni ni sawa ili Kupisha watu Kumsaidia PW, Lakini Lengo lake linaonekana wazi, Anachukua Mic na Kuondoka Bila Kujali au Kushangaa aliyeanguka kimempata Nini au yu hali gani. Ungedhani Mtu anayehangaika na Mics awe mhudumu na angekuwa mstari wa Mbele kusaidia. Huyu Hakuwa Ndiye "Hit Man"?

 
Ungeenda video tukaona .... may be tungekuwa na cha kucomment!!
 
Jamaa anamletea PW Wireless Mic katika stand (Pengine ilikuwa na sumu Tayari) Baada ya Muda Jamaa yuleyule anakuja na Kuchukua ile Mic na kutokomea nayo (Pengine alihisi sumu haitoshi akaenda kuongezea Dose) Jamaa anakuja na Mic ikiwa Vilevile kwenye stand, Anamwekea PW, halafu anaondoka kuelekea alikotoka. Muda Mfupi PW anaanguka ghafla, Watu wanamzunguka kusaidia. Jamaa yuleyule anatokeza tena. Cha kwanza Badala hata ya Kushangaa, au hata kwa Udaku tu kuinama na Kujua PW yupo katika hali gani, Yeye Bila Kustushwa anachukua Mic ile tena, Anasogea Kidogo, anacheki Noma! Kisha anatokomea Nayo. Mwanzo Unaweza Kusema Kuwa labda Kuisogeza Mic Pembeni ni sawa ili Kupisha watu Kumsaidia PW, Lakini Lengo lake linaonekana wazi, Anachukua Mic na Kuondoka Bila Kujali au Kushangaa aliyeanguka kimempata Nini au yu hali gani. Ungedhani Mtu anayehangaika na Mics awe mhudumu na angekuwa mstari wa Mbele kusaidia. Huyu Hakuwa Ndiye "Hit Man"
na MIC zilkua nyingi pale,kwa nini alihangaika na ile moja?!
 
Back
Top Bottom