Ni kweli Rais Samia ana nasaba na familia ya Mfalme wa Oman?

Ni kweli Rais Samia ana nasaba na familia ya Mfalme wa Oman?

Wanyama hai ni pamoja na ng'ombe, mbuzi na kondoo.
“Asante sana mama maana kumsafirisha mnyama hai aina ya twiga kwa Meli ni gharama ndogo sana ukilinganisha na usafiri wa anga.” Alisikika haramia mmoja wa kiburushi….

“Meli ikiamua kushona makontena trip mbili tu mbona Serengeti yote inaweza ikahamia hapo An Naman Zoo nchini Oman chap, kwani wao hawapendi wanyama hai pia!”. ….
Alisikika mmatumbi mmoja pale ferry

Hawa viongozi wetu wanawaza vizuri sana.
 
Tukiwa na Katiba imara mtu yeyote anatawala tu hakuna shida lakini kwa Katiba hii ....Huku Mama Samia.....Huku Master Kinana.....Pale Mzee wa Msoga.....Pale Mwinyi Mpeku .....sidhani kama tutachomoa
 
Kuna shida nyingi sana za kifikra kwa watanzania wote hata viongozi wao wa juu kabisa kuwa tunamhitaji mtu wa race nyingine aje atukomboe katika umaskini wetu na sisi wenyewe hatuwezi. Mkuu wa nchi anaenda nchi za mbali kuomba msaada eti njooni tumewapa bahari kuu yetu ukavue, uanzishe usafiri wa kusafirisha mali hai zetu badala ya kufanya wenyewe au kwa kutumia wazawa. Nchi hii itauzwa mchana kweupe nakumbuka kauli ya Spika wa zamani Ndugai na JPM.
Ndugai alikuwa hataki hata kusikia habari za wapinzani zilizokuwa zikiikosoa serikali kama vile wale wapinzani walikuwa ni wa kutoka nchi nyingine ya mbali !! Sasa yamemtokea yeye yaliyomtokea ni bora aendelee kunyamaza tu maana hakujua kwamba nchi hii itajengwa na watu wote wa Tanzania sio watu wa chama kimoja pekee !!! Kwahiyo maneno aliyosema Ndugai hayawezi kuwa na impact yeyote kwa watu wengi kwa sababu wanamkumbuka yule mheshimiwa Spika Ndugai alivyokuwa akiliendesha Bunge jinsi alivyokuwa akitaka yeye sio huyu wa sasa aliyesema Nchi itapigwa mnada siku moja !!
 
“Asante sana mama maana kumsafirisha mnyama hai aina ya twiga kwa Meli ni gharama ndogo sana ukilinganisha na usafiri wa anga.” Alisikika haramia mmoja wa kiburushi….

“Meli ikiamua kushona makontena trip mbili tu mbona Serengeti yote inaweza ikahamia hapo An Naman Zoo nchini Oman chap, kwani wao hawapendi wanyama hai pia!”. ….
Alisikika mmatumbi mmoja pale ferry

Hawa viongozi wetu wanawaza vizuri sana.
Wanyama huzaliana na kuongezeka kama wakipunguzwa kuna ubaya gani? Kuna wakati hata Nuhu aliwasafirisha wanyama kwa meli, ikibidi wanyama kusafirishwa wache wasafirishwe nawe fanya maarifa ya kusafirisha japo mbuzi mmoja, alisikika muhenga mmoja pale Mfereji Maringo.
 
Acha kujitoa ufahamu hapo Zenji tu mbara hupati ajira wakati wazanzibari wamejaa kibao Tanganyika. Sembuse Serikali iruhusu na waarabu waajiriwe si mtakuwa watumwa maana hamuwezi kushindana nao kwenye Skills na elimu maana wao wanasomea ngambo wewe umesoma S/M mchambawima, ungepatia wapi ajira ua baba yako wa kiembe samaki?
Ni afadhali umetambua kuwa ni wabaguzi
 
Tatizo ni nini mkuu? Mbona munaogopa waarabu kiasi hicho? au ndio nyinyi wale mkiwaona tu waarabu suruali zinaanza kuvuka wenyewe?

Umenikumbusha aise 😁😁😁 kuna wengine wanawakimbia kabisa, ndukii😁😁😁
 
We
Husikii
Mabinti wa kazi wanaoenda huko wananyanyaswa hata kuipoteza uhai!!?
Uongo!!?hata passport zao hunyang'anywa!!?

Hao jamaa Sio wa kuw achukulia poa!
Uongo!!?
Nina marafiki type hiyo lakini sishoboki kihivyo coz nawapata!!
Nilifanya kazi ofisi moja, wakati finance director ni mhindi na HR director ni mkurya...finance dept ilijaa diverse people from different tribes na dini...miaka kadhaa baadae hizo nafasi zikachukuliwa na wakristo wakinga wa njombe, ile diversity ikayeyuka, kila vacancy wanahakikisha wanaajiri mkristo mtu wa kwao Iringa na Mbeya...

Kwa hiyo ubaguzi upo tu mkuu...
 
Inaonekana wewe ni kichwa maandazi. Uwezo wako wa kutafakari mambo ni sawa tu na wa watoto wa shule ambao wanaweza wakapewa taarifa fulani na wakashindwa kuing'amua juu ya ukweli na uongo wake.
lalago ya huko shinyanga ina umri sawa na nairobi! Muscat fisi ya huko shinyanga ina umri sawa na muscat. lakini dah!!
 
Back
Top Bottom