Ni kweli TISS hawafahamiani na hawaaminiani?

Ni kweli TISS hawafahamiani na hawaaminiani?

Kila mtihani wa taifa kunakuwa na route za misafara ambapo kila ruti ina watu hawa;

(A) wasimamizi wakuu wa mitihani (supervisors- ambapo mara nyingi ni maafisa wa elimu )
(B) wasimamizi wa ndani wa mitihani (invigilators- yaani walimu)
(C) watu wa ulinzi wa mitihani (polisi na migambo)
(D) watu wa usalama wa mitihani (maafisa/watu kutoka ofisi ya usalama wa taifa)

Kulingana na utaratibu huo kwa wale wakongwe kwenye maswala ya usimamizi wa mitihani ya kitaifa imekuwa ni rahisi kwao kuwajua/kujuana wao kwa wao

Juzi kwenye mapokezi ya mwenge sasa kabla ya mwenge kufika sehemu ile ghafla ikaja gari na wakashuka watu kadhaa ambao kwa haraka haraka watatu waligundulika kuwa ni walewale ambao huwa wanakwepo kwenye mitihani kwa utambulisho wa kundi D. Walivalia locally tu kama kawaida yao, wakazunguka zunguka tu pale wakikagua kisha baada ya muda hao wakasepa kisha jioni ndipo mwenge ukafika pale

Sijui tu hata nimeandika nini hebu aliyeelewa anisaidie maana me mwenyewe sielewi
 
Wanafahamiana kama wako kwenye mishe moja ila kama hawako mishe moja hawajuani

Na kama wamekutana mazingira anaweza kuhisi kwa kuona tabia za mwenzake sijui nimeeleweka maana hata mwenyewe sijaelewa nilicho kiandika
 
Wanafahamiana kama wako kwenye mishe moja ila kama hawako mishe moja hawajuani

Na kama wamekutana mazingira anaweza kuhisi kwa kuona tabia za mwenzake sijui nimeeleweka maana hata mwenyewe sijaelewa nilicho kiandika
Hawanaga depo?
 
Kuna wanaojuana, kuna wasiojuana, kuna wanao-wafanyia ujasusi wenzao uku nao wakifanyiwa ujasusi bila kuwajua wanaowafanyia ujasusi, kuna wanaofanyishwa kazi za usalama bila wao kujijua, iwe kwenye siasa, biashara, dini kote wapo majasusi.

Tatizo la ujasusi wa bongo umejikita kwenye kukusanya taarifa zaidi za mambo mbali mbali kusaidia utawala uliopo madarakani tofauti na wenzetu ambao wanajikita sana kwenye kuzuia hatari zote mbaya zizazohusu uchumi na siasa bila kuegemea upande wowote wa kisiasa.

TISS wanatakiwa kujikita kwenye ujasusi wa kiuchumi jinsi ya kutengeneza mabilionea, jinsi ya kupigana vita ya kiuchumi na mataifa jirani, kuhakikisha taarifa za kiujasusi wanazokusanya zinafanyiwa kazi haraka bila kuegemea upande wowote.
Wapo kila sehemu Airport, Tanesco sijui bandarini kila sehemu wapo kwenye mashirika ya serikali mpaka private sema taarifa wanazozipenda watawala nizile kama wanahatarisha utawala wao lakini kwenye kila kitengo wapo tena wengi tu. Taarifa zao zinafanyiwa kazi inategemea na kiongozi anataka kujuwa nini shida viongozi wamejikita kwenye usalama wao sio upigaji ila kama wako serious kabla ya report ya CAG wanajuwa kila upigaji.
 
Jamanieee hao usalama ni watu wa kawaida tu (hususani hawa wa hapa kwetu)

Tofauti kubwa iliyopo ni kwamba wanafanya shughuli zao kwa SIRI. Hapo ndio nguvu yao ilipo.

Hata wewe ukiweka maisha yako PRIVATE watu watakuwa wanakuogopa kwa kuwa hawakujui vizuri.

Hata Secret Societies kama Illuminati, Freemasonry, Klu Kla Klux et al zinatumia USIRI kama mbinu mojawapo.

Sababu nyingine: Kwa kuwa CCM inawatumia sana, hivyo imewapa nguvu fulani ( kuwaweka juu ya sheria kwa raia ) kiasi kwamba hata akikuonea huwezi kumfanya chochote.

Suala la kutoaminiana ni kawaida tu kwenye mambo ya ulinzi na usalama, hata walinzi hawaaminiani.

Na kuhusu kutojuana ni kawaida pia, hata mwalimu hajuani na walimu wote nchi nzima unless mmekuwa assigned sehemu moja.

Wanaruhusiwa pia kuwa na vifaa/silaha ambazo wewe raia huruhusiwi kuwa nazo kitu kinachowapa nguvu dhidi ya raia!

Mambo mengine yote ni yale yale.

Kwa kuongeza, nimewahi kuwa lindo moja na Hawa jamaa kwanza walikuwa wanalala tu, maana walikuja na tent na kitanda kikawekwa ndani. Bastola walikuwa wanakabidhiana ( taking and handing over ).
Ikulu ya dodoma! Geti la kwanza,la pili na la tatu! Endelea tu kutoa Siri za hapo!!
 
Kila mtihani wa taifa kunakuwa na route za misafara ambapo kila ruti ina watu hawa;

(A) wasimamizi wakuu wa mitihani (supervisors- ambapo mara nyingi ni maafisa wa elimu )
(B) wasimamizi wa ndani wa mitihani (invigilators- yaani walimu)
(C) watu wa ulinzi wa mitihani (polisi na migambo)
(D) watu wa usalama wa mitihani (maafisa/watu kutoka ofisi ya usalama wa taifa)

Kulingana na utaratibu huo kwa wale wakongwe kwenye maswala ya usimamizi wa mitihani ya kitaifa imekuwa ni rahisi kwao kuwajua/kujuana wao kwa wao

Juzi kwenye mapokezi ya mwenge sasa kabla ya mwenge kufika sehemu ile ghafla ikaja gari na wakashuka watu kadhaa ambao kwa haraka haraka watatu waligundulika kuwa ni walewale ambao huwa wanakwepo kwenye mitihani kwa utambulisho wa kundi D. Walivalia locally tu kama kawaida yao, wakazunguka zunguka tu pale wakikagua kisha baada ya muda hao wakasepa kisha jioni ndipo mwenge ukafika pale

Sijui tu hata nimeandika nini hebu aliyeelewa anisaidie maana me mwenyewe sielewi
Mkuu
Bado najiuliza, lengo la kuwafahamu hao TISS ni nini haswa?

Kama wapo na kama sheria inataka wasiwe public known basi tuache hiyo kwa sababu kuwafahamu ni kama kujianika usalama wetu ulivyo na adui anajipanga apenye wapi.

Nchi zinazozingatia uhai wa Taifa lao, hakuna utamaduni kama huu wetu wa kujimwambafai kuwa unajuana na TISS au yule ni TISS (kwa mataifa hayo)

Tanzania tuna mbwembwe nyingi asee
 
Back
Top Bottom