Ni kweli Wastara anatudanganya kuwa yupo hospitalini India?

Ni kweli Wastara anatudanganya kuwa yupo hospitalini India?

Wakati mwingine hiyo sindano inakuwa imetulizwa tu hapo ikingojea drip.
Mama mbona hujaelewa... Kinachohojiwa hapo ni uelekeo wa hiyo sindano ya huyo mgonjwa wetu ukilinganisha na hizo picha zingine ambazo uelekeo wake uko sahihi. Kusubili drip ni sawa, lakini namna ikivyochomwa.
 
Basi aje hata ndugu ay jamaa yake adhibitishe haya kwa vielelezo toka hospital , alafu pia tuone treatment ya mguu inavyoendelea , sio kutukuonyesha mikoni wakati mguu ndio unatatizo
 
Na anatibiwa kwa nzenza za serikali nakati Mbunge Lissu anaugulia risasi 38 bila hata msaada wa piriton toka seeikalini. Hiyo ndo Tanzania!
 
Mama mbona hujaelewa... Kinachohojiwa hapo ni uelekeo wa hiyo sindano ya huyo mgonjwa wetu ukilinganisha na hizo picha zingine ambazo uelekeo wake uko sahihi. Kusubili drip ni sawa, lakini namna ikivyochomwa.
Yaani Mamndenyi anakuambia kua hiyo sindano hata kuchomwa haijachomwa bado, madokta au manesi wameigundishia tu kwenye mkono ili drip ikija ndio waichome,
 
Huyu dada kuna tatizo mahali..

Kama anaweza hata kumchezesha movie mkuu wa nchi basi ameshindikana.
Huyu mkuu wenu wa nchi nae alizoea kulima tu mihogo huko Geita wacha akutane na mtoto wa mjini...bado Wema naye atazivuta tu!
 
Mamndenyi inaonekna wewe umetoka Mamndenyi juzi juzi na ushamba wa mamndenyi bado unao. Unatakiwa kuelewa somo kabla hujabisha! Na njia nzuri ni kuuliza. Tatizo sio hicho ''kidude'' ambacho kwa jina la kitibabu kinaitwa canulla kuwa hapo mkononi. Tatizo ni kimegeukia chini. Yaani ule uwazi wa kuingiza dawa yenye maji umekuwa kwa juu na sindano ikailekezwa chini kwenye vidole. Wakati inatakiwa ile sindano ichomekwe kwenye mshipa wa damu kuelekea juu! Kwanini wanaweka hivyo? Kwa sababu nia ni ku-pump dawa kwenye mishipa ili iingie kwenye mwili hivyo ni lazima ufuate mkondo wa damu unavyokwenda!
Nadhani wote wasiolewa sasa umewasaidia kwa maelezo haya mazuri, wakiongozwa na huyu Mamndenyi
 
Wakuu.
kampeni hii ni kubwa sana.
kumtapeli Rais ni kosa kubwa je ni wananchi wangapi amewatapeli?
Wastara rudisha pesa ya rais wetu huo utapeli ukawafanyie bongo movie wenzio sio Rais.
kumbe ndio maana walikutelekeza wakijua unazuga na nimuongo mkubwa unatumia ulemavu kutapeli watu wengine.
 
Huyu Dada Wastara kweli alipata maswahibu, na jamii ya Tanzania iliguswa sana. Binafsi sijawah kumchangia na wala sina kawaida ya kuchangia mastaa, sadaka yangu hua naitoa kwa wahitaji waliosetwa na hua ninasaidia kwa siri kubwa kiasi kwamba mkono wa kuume unapotoa basi mkono mwingine usijue kabisa kinachoendelea kama yanavyoagiza maandiko.

Huyu Wastara sasa kachangiwa na kiongozi wa nchi akapate matibabu ughaibuni. Kitendo cha yeye kuleta maigizo (kama ni kweli) ili atafune pesa ni jambo baya na linaaibisha haiba ya waliomchangia. Anawadhihirishia kwamba yeye ni mjanja sana na wao ni mabwegwe, yumkini! Hili litamcost sana, ikithibitika. Lazima mamlaka itamfanyia ushushushu akirudi au yumkini "watu" wapo nae huko aliko bila yeye kujua.

Namuombea sana isiwe kweli.
 
Kichwa cha habari kinamuhusu "kajara" content inamuhusu "wastara" ni kweli haujui kuwa hawa ni watu tofauti.
Sorry mkuu, hawa watoto mie siwafuatiliagi sana wananichanganya. Nafkir Mods wabadilishe tu jina likae sawa. Sasa usahihi wa jina la huyu anaeumwa mguu sjui ni upi mkuu, ni Kajara au Wastara?
 
Hiki kipaji ni sawa na cha tapeli aliyewauzia watu mnara wa Eiffel.

Kitunzwe na kilelewe
 
Back
Top Bottom