Ni mamlaka ipi yenye wajibu wa kusimamia matumizi salama ya barabara katikati ya jiji la Arusha?

Ni mamlaka ipi yenye wajibu wa kusimamia matumizi salama ya barabara katikati ya jiji la Arusha?

brokenagges

Member
Joined
Sep 29, 2022
Posts
58
Reaction score
33
IMG_4594.jpg
Hii nimeiona leo ktk jiji la arusha kwenye barabara ya jogoo house kwenda uhuru road,duka la vinywaji la MAINA HOLDINGS kwa namna wanavyopaki magari yao na hata magari ya wateja siyo salama kabisa kwa sababu barabara ni vinyu hairuhusu gari kupaki kwa kukatiza barabara kwani hii ni hatari kwa wapita njia wengine wanaotumia miguu na hata wenye vyombo vya moto na ambao nao wanayo haki ya kuitumia barabara

sidhani kama kuwa na leseni ya duka ama biashara ndo inampatia mtu uhuru wa kutumia barabara kwa matumizi yake binafsi na kwa namna anavyotaka yeye bila kujali wengine wala kufuata sheria na taratibu za amtumizi ya barababra.

Inakuwa ni rahisi sana kama picha inavyoonyesha uwezekano kugongwa watembea kwa miguu ama kugonga kwa wenye vyombo vya moto unakuwa ni mkubwa sana.

ni vizuri zichukuliwe hatua za kuepusha ajali kabla ajali haijajitokeza.

Barabara hii ilikuwa ni kero sana kipindi machinga waliporuhusiwa kufanya biashara eneo lolote la barabarani bila kujali na baadae machinga walipoondolewa eneo hili likawa liko sawa.

ila sasa kero ya machinga imeonekana kwamba haikuwa kero kubwa kama hila la kupaki gari kama Canter kukatiza barabara katikati mjini na kama tunavyofahamu ufinyu wa barabara zetu za katikati ya miji.
 
Ujinga huu Dar inaonekana ni jambo la kawaida kabisa. Njia za waenda kwa miguu ndio parking za wateja wa viduka vilivyojaa pembezoni mwa barabara manna yake waenda kwa miguu wapite barabarani.
 
Ujinga huu Dar inaonekana ni jambo la kawaida kabisa. Njia za waenda kwa miguu ndio parking za wateja wa viduka vilivyojaa pembezoni mwa barabara manna yake waenda kwa miguu wapite barabarani.

Ni vema TARURA kwa sababu kwamba wameweka wafanyakazi wa kukusanya ushuru wa parking pia wangetoa semina kwa hao wakusanya ushuru ili wawaelekeze wateja wao namna nzuri ya kupaki magari.
 
Back
Top Bottom