Ni mapema mno kumnyooshea kidole mheshimiwa Rais, Tumpe muda!

Ni mapema mno kumnyooshea kidole mheshimiwa Rais, Tumpe muda!

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

Suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
 
suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU....
Na hao ambao wanalipa kodi hiyo bila kustahili mbona huwasemei? Wazee ambao sheria inasema wasilipe kodi hiyo ila kwa sababu nyumba zao zina umeme sasa wanalipa!

Na hao wenye nyumba zisizo za kudumu lakini wana umeme, si wanalipa kodi hiyo sasa?

Ni kweli kodi hii haikuwekwa na Samia lakini mfumo wa ukusanyaji wa sasa umewekwa na serikali yake, na watu wanacholalamikia siyo kodi yenyewe bali mfumo wa ukusanyaji umewaingiza mbao hawapaswi kulipa.

Unafikiri haya yamezingatiwa katika mfumo wa kulipa kwa Luku kila mwezi 1,000?

KODI YA MAJENGO
Kodi ya majengo ni kodi inayotozwa kwenye majengo ya kudumu. Majengo yaliyojengwa kwa tofali za kuchoma au tofali za kawaida isipokuwa yale yaliyojengwa kwa nyasi au udongo.

MAJIJI, MANISPAA NA HALMASHAURI ZA MIJI
Kodi hii ni shilingi 10,000 kwa kila nyumba ya kawaida na 50,000 kwa kila sakafu kwenye jengo la ghorofa.

HALMASHAURI ZA WILAYA
Kodi hii ni shilingi 20,000 kwa ghorofa zima na 10000 kwa majengo yaliyokatika kiwanja kimoja kama kuna nyumba za kawaida ila kama kuna ghorofa itakuwa shilingi 20,000.
 
ACHEN KUMDEKEZA

MPE MUDA MPE MUDA NN???

HUYO NI MTI MZIMA ANA AKILI TIMAMU.

HAFAI, HAFAI NA HAJAWAHI KUFAA KUA RAIS.

2025, VYOMBO VYA DOLA, KAMA MMESHINDWA SANA KUACHA WANANCHI WACHAGUE, BASI MSITULETEE MTU WA AINA HII KUPITIA CCM.
 
Ahsante kwa ufafanuzi vp waliochepusha bomba la mafuta kigamboni unaweza kutwambia ni hatua gani mpaka sasa zimechukuliwa je ni akina nani hao? na wale je waliokuwa wanajilipa mamilioni kwa mpango kazi maalum usiojulikana nao vp wamarudisha mamilioni yetu?? pesa walikuwa nayo kwenye akaunti zao.
 
Unajua kazi za jeshi la polisi kwa mapana yake?

Au kwa kuwa Mbowe ni malaika?
 
Mkuu utapata taabu sana ktk hiki kibarua chako cha kujaribu kumtenganisha rais na maovu yayaoendelea nchini.

Kwa mujibubwa mfo wetu wa uwongozuli, hakunq kitu kinafanyika bila rais kuidhinisha ama kufahamishwa.
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
Namuelewa sana MAMA, ila anahitaji kufumua safu ya juu ya uongozi kwa baadhi ya vyombo vyetu vya ulinzi...wanamuangusha na hajui
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
Gari inapoanza safari mda si mrefu wew abiria utajuwa tu dereva ni mzuri au mbaya.., hata sas Watz wameshajuwa dereva wao ni wanamna gani.., kikubwa kusubili tu atufikishe mwisho wake tuangalie uwezekano mwingine.
 
Unampaje muda Zezeta ambae kwa mfano Polisi wanashutumiwa na wananchi katika tukio alilofanya Bwana Hamza halafu anaruhusu Polisi wajichunguze wenyewe?Zezeta kama huyu unawezaje kusema kuwa apewe muda?Upo sawa kichwani?
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.

Vipi kuhusu bei ya mbolea, bei ya Petrol?

Unajua Rais wa Zanzibar amefanya mengi kwa muda mfupi. Maelewano na Cuf, kaiunganisha Zanzibar. Ana sera zinazoeleweka (Blue Economy) mikakati ya ukweli kuwavutia wawekezaji na Wazanzibari diaspora na kuweka mazingira mazuri wafanyabiashara, utalii, kilimo cha kisasa, miundombinu, utalii.

Mchapa kazi mwenye maono, malengo,dira, uthubutu na kasi. Watu wanawajibishwa wasipowajibika.

Matokeo yanaonekana wazi.

Lakini Huku bara dah?
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
Acha kujipendekeza!
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.

Huyu hapa:

IMG_20210829_163746_049.jpg


Hata apewe Karne nzima kama masikioni kukavu forget it.

Suala la Mbowe wewe na mtoto mdogo anajua ni yale yale ya kubambikiziana kesi.

Miamala, kodi na tozo - zinaongezwa vipi kwetu si kwao katikati ya janga la Corona?

Serikali 'sikivu' Inaposikia nusu nusu

Unajua hata wagonjwa wa Corona tunajigharimia wenyewe lakini si wao?
 
Kwa viwango vyake muda huu umekwishatosha kumfahamu fika! Gari linavuja oil unatoa muda wa nini kulipeleka gereji au kufanywa chuma chakavu!
 
BILA SHAKA KBS!! MTOA MADA ANATAKA ATEULIWE.....
But anyway bongo unafiki na kujipendekeza hakujawahi kuisha ...

Kiufupi maza anatia kichefuchefu
Ni muda wa kumpindua tu!!!
 
Back
Top Bottom