Ni mauzauza gani ulishawahi kukutana nayo barabarani?

Ni mauzauza gani ulishawahi kukutana nayo barabarani?

Kiranja Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2010
Posts
4,219
Reaction score
4,608
1705097895486.jpg


Nakumbuka tulikuwa tunatoka kijijini Kibungo wilaya ya Kigamboni, tunaelekea Pemba Mnazi kuogelea.


Tulipokuwa tunaingia Pemba Mnazi, barabara imefunikwa na kivuli kikali cha miti mikubwa ya miembe.

Katikati ya kivuli ukatokea mwanga mkali sana kiasi cha kutufanya tusiweze kuona mbele.

Basi wale wamama niliokuwa nao wakaanza kukemea, mara mbele katikati ya barabara kakatokea kababu kamevaa nguo zote nyeupe, kana ndevu nyeupe, kamekaa chini barabarani.

Basi nilikuwa naendesha Mark ll Super Charger ya boss TAJIRI MKUU WA MATAJIRI, bwana ehh, kazee haka hapa, nikakwepe au nikagonge?
Ile nimekakwepa,, mara bonge la shimo hili hapa, ndio gari inaenda kuzama. Pongezi kwa wana maombi.

Tukarudisha gari nyuma, wananchi wanapiga miluzi kama yote, mna bahati sana nyie, huu ni muda wa majini kwenda kuswali, kweli MUNGU wenu ni mkubwa.
 
Visa vingi sana, kimoja wapo; Nilikuwa nasafiri na mume wangu, kufika mikumi tukaenda Snake Park, kuna Restaurant nzuri pale, baada ya kula tunatoka nje tukamkuta kijana mmoja akatwambia na yeye hajala, tumsaidie akale, mume wangu akampa pesa, tukaondoka. Tunafika mbele kidogo kuelekea vilima vya uaha kuna geti lipo karibu na reli, tukasimamishwa, ile tumesimama askari wawili wakaja, mmoja akauliza mnaenda wapi, mume wangu akamwambia Iringa, yule askari akamwambia, "mzee tuwachie chochote, getini hapa mambo magumu" ile mume wangu kabla hajasema chochote yule askari mwenzake akamwambia, tayari wazee hao wameshatupa pesa ya kula, kumtazama ni yule kijana alikuwa pale Snake Park aliyepewa pesa na mume wanu na alikuwa kavaa kiraia sasa yupo kwenye magwanda. Yule askari akatwambia haya safari njema wazee.

Hilo tukio lilitushangaza sana na mume wangu, mpaka leo tunashindwa kupata jibu.

Mie huwa nayaita, majegajega ya mikumi.
 
Visa vingi sana, kimoja wapo; Nilikuwa nasfiri na mume wangu, kufika mikumi tukaenda Snake Park, kuna Restaurant nzuri pale, baada ya kula tunatoka nje tukamkuta kijana mmoja akaywambia na yeye hajala, tumsaidie akale, mume wangi akampa pesa, tukaondoka. Tunafika mbele kidogo kuelekea kuna geti tukasimamishwa, ile tumesimama askari wawili wakaja, mmoja akauliza mnaenda wapi, mume wangu akamwambia Iringa, yule askari akamwambia, "mzee tuwachie chochote, getini hapa mambo magumu" ile mume wangu kabla hajasema chochote yule askari mwenzake akamwambia, tayari wazee hao wameshatupa pesa ya kula, kumtazama ni yule kijana alikuwa pale Snake Park na alikuwa kavaa kiraia sasa yupo kwenye magwanda. Yule askari akatwambia haya safari njema wazee.

Hilo tukio lilitushangaza sana na mume wangu, mpaka leo tunashindwa kupata jibu.

Mie huwa nayaita, majegajega ya mikumi.
 

Attachments

  • IMG_20240113_003425.jpg
    IMG_20240113_003425.jpg
    31.4 KB · Views: 8
Visa vingi sana, kimoja wapo; Nilikuwa nasfiri na mume wangu, kufika mikumi tukaenda Snake Park, kuna Restaurant nzuri pale, baada ya kula tunatoka nje tukamkuta kijana mmoja akaywambia na yeye hajala, tumsaidie akale, mume wangi akampa pesa, tukaondoka. Tunafika mbele kidogo kuelekea kuna geti tukasimamishwa, ile tumesimama askari wawili wakaja, mmoja akauliza mnaenda wapi, mume wangu akamwambia Iringa, yule askari akamwambia, "mzee tuwachie chochote, getini hapa mambo magumu" ile mume wangu kabla hajasema chochote yule askari mwenzake akamwambia, tayari wazee hao wameshatupa pesa ya kula, kumtazama ni yule kijana alikuwa pale Snake Park na alikuwa kavaa kiraia sasa yupo kwenye magwanda. Yule askari akatwambia haya safari njema wazee.

Hilo tukio lilitushangaza sana na mume wangu, mpaka leo tunashindwa kupata jibu.

Mie huwa nayaita, majegajega ya mikumi.
Majira ya saa 10 alasiri Same kilimanjaro nikielekea Dar, ndani ya gari tupo watatu, mmoja dada askari JkT amekaa kushoto kwangu.

Ghafla akatokea Nyoka mkubwa tokea kushoto mwa barabara kuelekea kulia.

Ninawaambia mnameona yule nyoka?
Wote wananishangaa hawaoni kitu.

Jambo la ajabu nilipofika eneo alokatisha nyoka upepo ulivuma sana kiasi cha gari kuhama barabarani.

Nilibaki na maswali hadi leo
 
visa vya ukweli ni vichache

vingi ni hallucinations watu kuendesha gari usiku wakiwa na usingizi ama wamejibusti na kahawa, pombe kali, bangi, miraa. Zoezi la kuendesha linahotaji focus na ukiwa na usingizi ama ukitumia kilevi kikate usingizi waweza pata hallucinations.
 
Majira ya saa 10 alasiri Same kilimanjaro nikielekea Dar, ndani ya gari tupo watatu, mmoja dada askari JkT amekaa kushoto kwangu.

Ghafla akatokea Nyoka mkubwa tokea kushoto mwa barabara kuelekea kulia.

Ninawaambia mnameona yule nyoka?
Wote wananishangaa hawaoni kitu.

Jambo la ajabu nilipofika eneo alokatisha nyoka upepo ulivuma sana kiasi cha gari kuhama barabarani.

Nilibaki na maswali hadi leo
Dah umenikumbusha, hiyo ya kukatiziwa na nyoka nimekutana nayo mara zaidi ya tatu. Unajuwa mume wangu kazi zake Tanzania ni za kusafiri sana na hupenda kufatana nae. Siku hiyo tunatoka Tanga tunarudi Dar., kabla ya kufika hale bonge la nyoka limetoka kulia kwenda kushoto mbele ya gari, mume wangu kasimamisha gari, laktupita taratibu, kumaliza njia kufika kushoto kanyanyuwa kichwa, mume wangu akaondosha gari akasema, anatwambia ahsante. Ile scene nilitamani ingekuwa nimeipiga picha, ilikuwa nzuri sana.

Dah, nna visa vingi sana vya safari za Tanzania na nje ya Tanzania, ntakuwa nawapa kidogo kidogo. Vinapotokea unaona vya kawaida tu, lakini baadae ukivifikiri vinakuwa ni "adventure".

Mimi nashukuru Mungu, nimesafiri sana hii Tanzania na duniani kwa ujumla. Mwenyezi Mungu alimjaalia kazi za safiri mume wangu na mimi huwa nakuwa betri kila inapotokea fursa.
 
Dah umenikumbusha, hiyo ya kukatiziwa na nyoka nimekutana nayo mara zaidi ya tatu. Unajuwa mume wangu kazi zake Tanzania ni za kusafiri sana na hupenda kufatana nae. Siku hiyo tunatoka Tanga tunarudi Dar., kabla ya kufika hale bonge la nyoka limetoka kulia kwenda kushoto mbele ya gari, mume wangu kasimamisha gari, laktupita taratibu, kumaliza njia kufika kushoto kanyanyuwa kichwa, mume wangu akaondosha gari akasema, anatwambia ahsante. Ile scene nilitamani ingekuwa nimeipiga picha, ilikuwa nzuri sana.

Dah, nna visa vingi sana vya safari za Tanzania na nje ya Tanzania, ntakuwa nawapa kidogo kidogo. Vinapotokea unaona vya kawaida tu, lakini baadae ukivifikiri vinakuwa ni "adventure".

Mimi nashukuru Mungu, nimesafiri sana hii Tanzania na duniani kwa ujumla. Mwenyezi Mungu alimjaalia kazi za safiri mume wangu na mimi huwa nakuwa betri kila inapotokea fursa.
Dada FaizaFoxy unamtaja mumeo kila baada ya sentensi mbili!!! Unatuogopesha........
 
Visa vingi sana, kimoja wapo; Nilikuwa nasafiri na mume wangu, kufika mikumi tukaenda Snake Park, kuna Restaurant nzuri pale, baada ya kula tunatoka nje tukamkuta kijana mmoja akatwambia na yeye hajala, tumsaidie akale, mume wangu akampa pesa, tukaondoka. Tunafika mbele kidogo kuelekea ilima vya uaha kuna getilipo karibu na reli, tukasimamishwa, ile tumesimama askari wawili wakaja, mmoja akauliza mnaenda wapi, mume wangu akamwambia Iringa, yule askari akamwambia, "mzee tuwachie chochote, getini hapa mambo magumu" ile mume wangu kabla hajasema chochote yule askari mwenzake akamwambia, tayari wazee hao wameshatupa pesa ya kula, kumtazama ni yule kijana alikuwa pale Snake Park aliyepewa pesa na mume wanu na alikuwa kavaa kiraia sasa yupo kwenye magwanda. Yule askari akatwambia haya safari njema wazee.

Hilo tukio lilitushangaza sana na mume wangu, mpaka leo tunashindwa kupata jibu.

Mie huwa nayaita, majegajega ya mikumi.
Ilima- vilima, uaha- Ruaha
 
Dah umenikumbusha, hiyo ya kukatiziwa na nyoka nimekutana nayo mara zaidi ya tatu. Unajuwa mume wangu kazi zake Tanzania ni za kusafiri sana na hupenda kufatana nae. Siku hiyo tunatoka Tanga tunarudi Dar., kabla ya kufika hale bonge la nyoka limetoka kulia kwenda kushoto mbele ya gari, mume wangu kasimamisha gari, laktupita taratibu, kumaliza njia kufika kushoto kanyanyuwa kichwa, mume wangu akaondosha gari akasema, anatwambia ahsante. Ile scene nilitamani ingekuwa nimeipiga picha, ilikuwa nzuri sana.

Dah, nna visa vingi sana vya safari za Tanzania na nje ya Tanzania, ntakuwa nawapa kidogo kidogo. Vinapotokea unaona vya kawaida tu, lakini baadae ukivifikiri vinakuwa ni "adventure".

Mimi nashukuru Mungu, nimesafiri sana hii Tanzania na duniani kwa ujumla. Mwenyezi Mungu alimjaalia kazi za safiri mume wangu na mimi huwa nakuwa betri kila inapotokea fursa.
Yes, barabarani kuna visa vingi.
Miaka kama 10 hivi nilikuwa nasafiri kwenye basi jina Born city toka Arusha kuelekea Singida.
Baada ya kupita Endasak, kuna Mwiraq alikuwa amesimama ukingo wa kulia mwa barabara, gari ilipokaribia alijirusha katikati ya barabara, jambo la kushangaza sikusikia kishindo cha kugongwa wala dereva hakushtuka wala kupunguza mwendo.
 
Back
Top Bottom