FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,246
- 123,145
Kisa kinamhusu.Dada FaizaFoxy unamtaja mumeo kila baada ya sentensi mbili!!! Unatuogopesha........
Nikuogopeshe nini, wewe huna mume?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kisa kinamhusu.Dada FaizaFoxy unamtaja mumeo kila baada ya sentensi mbili!!! Unatuogopesha........
Leo amesafiri naona upo jf muda huu saa nane usikuDah umenikumbusha, hiyo ya kukatiziwa na nyoka nimekutana nayo mara zaidi ya tatu. Unajuwa mume wangu kazi zake Tanzania ni za kusafiri sana na hupenda kufatana nae. Siku hiyo tunatoka Tanga tunarudi Dar., kabla ya kufika hale bonge la nyoka limetoka kulia kwenda kushoto mbele ya gari, mume wangu kasimamisha gari, laktupita taratibu, kumaliza njia kufika kushoto kanyanyuwa kichwa, mume wangu akaondosha gari akasema, anatwambia ahsante. Ile scene nilitamani ingekuwa nimeipiga picha, ilikuwa nzuri sana.
Dah, nna visa vingi sana vya safari za Tanzania na nje ya Tanzania, ntakuwa nawapa kidogo kidogo. Vinapotokea unaona vya kawaida tu, lakini baadae ukivifikiri vinakuwa ni "adventure".
Mimi nashukuru Mungu, nimesafiri sana hii Tanzania na duniani kwa ujumla. Mwenyezi Mungu alimjaalia kazi za safiri mume wangu na mimi huwa nakuwa betri kila inapotokea fursa.
Jibu mada au hoja zilizopo.Leo amesafiri naona upo jf muda huu saa nane usiku
Mi1mi mume ninayetafuta mke ndo maana nikasema mbona unatuogopesha sasaKisa kinamhusu.
Nikuogopeshe nini, wewe huna mume?
Wewe unataka Ninywe Uji tu basi.Utakuwa ni mlevi sana, cha pombe. Unategemea uone nini ukisha lewa?
Sasa unachoogopa ni nini? Unataka kunitongoza?Mi1mi mume ninayetafuta mke ndo maana nikasema mbona unatuogopesha sasa
Jiyu lipo clear kabisa. Siku utaanza kunywa "uji tu" ndipo macho yatafunguka na akili zitaanza kufanya kazi.Wewe unataka Ninywe Uji tu basi.
Hatari sanaView attachment 2870193
Nakumbuka tulikuwa tunatoka kijijini Kibungo wilaya ya Kigamboni, tunaelekea Pemba Mnazi kuogelea.
Tulipokuwa tunaingia Pemba Mnazi, barabara imefunikwa na kivuli kikali cha miti mikubwa ya miembe.
Katikati ya kivuli ukatokea mwanga mkali sana kiasi cha kutufanya tusiweze kuona mbele.
Basi wale wamama niliokuwa nao wakaanza kukemea, mara mbele katikati ya barabara kakatokea kababu kamevaa nguo zote nyeupe, kana ndevu nyeupe, kamekaa chini barabarani.
Basi nilikuwa naendesha Mark ll Super Charger ya boss TAJIRI MKUU WA MATAJIRI, bwana ehh, kazee haka hapa, nikakwepe au nikagonge?
Ile nimekakwepa,, mara bonge la shimo hili hapa, ndio gari inaenda kuzama. Pongezi kwa wana maombi.
Tukarudisha gari nyuma, wananchi wanapiga miluzi kama yote, mna bahati sana nyie, huu ni muda wa majini kwenda kuswali, kweli MUNGU wenu ni mkubwa.
Duh, dereva naye alikuwa kajisindikaYes, barabarani kuna visa vingi.
Miaka kama 10 hivi nilikuwa nasafiri kwenye basi jina Born city toka Arusha kuelekea Singida.
Baada ya kupita Endasak, kuna Mwiraq alikuwa amesimama ukingo wa kulia mwa barabara, gari ilipokaribia alijirusha katikati ya barabara, jambo la kushangaza sikusikia kishindo cha kugongwa wala dereva hakushtuka wala kupunguza mwendo.
Aisee, kumbe na wewe shule ulienda kusomea digrii ya ujingaVisa vingi sana, kimoja wapo; Nilikuwa nasafiri na mume wangu, kufika mikumi tukaenda Snake Park, kuna Restaurant nzuri pale, baada ya kula tunatoka nje tukamkuta kijana mmoja akatwambia na yeye hajala, tumsaidie akale, mume wangu akampa pesa, tukaondoka. Tunafika mbele kidogo kuelekea ilima vya uaha kuna getilipo karibu na reli, tukasimamishwa, ile tumesimama askari wawili wakaja, mmoja akauliza mnaenda wapi, mume wangu akamwambia Iringa, yule askari akamwambia, "mzee tuwachie chochote, getini hapa mambo magumu" ile mume wangu kabla hajasema chochote yule askari mwenzake akamwambia, tayari wazee hao wameshatupa pesa ya kula, kumtazama ni yule kijana alikuwa pale Snake Park aliyepewa pesa na mume wanu na alikuwa kavaa kiraia sasa yupo kwenye magwanda. Yule askari akatwambia haya safari njema wazee.
Hilo tukio lilitushangaza sana na mume wangu, mpaka leo tunashindwa kupata jibu.
Mie huwa nayaita, majegajega ya mikumi.
Nasikia huyu ni mamsap wa Mshana JrDada FaizaFoxy unamtaja mumeo kila baada ya sentensi mbili!!! Unatuogopesha........
KUnywa togwa😂Wewe unataka Ninywe Uji tu basi.
Hakuna kosa la R na L hapo. Hizo ni typo za kawaida tu ambazo hazibadili maana.Aisee, kumbe na wewe shule ulienda kusomea digrii ya ujinga
🤣🤣🤣🤣Sasa unachoogopa ni nini? Unataka kunitongoza?
Khaaa ulikaa siti ya ngapi ukamuona?Yes, barabarani kuna visa vingi.
Miaka kama 10 hivi nilikuwa nasafiri kwenye basi jina Born city toka Arusha kuelekea Singida.
Baada ya kupita Endasak, kuna Mwiraq alikuwa amesimama ukingo wa kulia mwa barabara, gari ilipokaribia alijirusha katikati ya barabara, jambo la kushangaza sikusikia kishindo cha kugongwa wala dereva hakushtuka wala kupunguza mwendo.
Yaan umenichekesha, huu uzi unatakiwa usomwe saa saba usiku hadi saa tisaSa hivi saa Tisa kasoro usiku
Nimeshtuka usungizini naangalia JF naona story za majini
Nikashangaa sana haya mauzauza usiku WOTE huu nikavaaa miwani meusi
they liveView attachment 2870200