Ni mawazo yamenizidi au uzembe?

Ni mawazo yamenizidi au uzembe?

changamoto za kimaisha ukichanganya na maisha binafsi inaweza kuwa chanzo cha mambo haya.
nakushauri nenda eneo la bustani ukiwa na chupa ya maji kama lita na nusu peke yako kaa ukimya ukitafakari moja baada ya lingine na kisha kupata majibu kisha ndo tafuta mtu wa kushare naye kwa yale ambayo majibu hukuwa nayo ya kutosha huku ukilinganisha na ya kwako.
  1. katika kujadili kwako anza na mafanikio kisha matatizo na hapa matatizo utaona ni changamoto usianze na mtatizo kisha mafanikio hutaondoa stress.
  2. jitahidi usijihukumu na mshushe kila mtu aliyekukwaza na uliyembebaikiwezekana waweza kumpigia simu ya kumsalimia na hata asipopokea usijali ruhusu moyo usukume damu na sio machungu.
  3. tumia muda pia kujadili uchumi wako kwa kuangalia nini ulipanga mwaka jana kipi hakikwenda na kipi unafikiri unaweza kuendelea nacho na ni kwanini?
  4. panga upya mambo yako ya mwaka huu kwa kadri ya resource chache ulizonazo
  5. yatazame mahusiano yako yakoje, na angalia jinsi ya kuyaboresha ukianza kuangalia mapungufu yako kwa mpenzi wako na sio yake kwanza. anza kubadilika wewe kwanza kisha mwenzako
yapo mengi lakini nafikiri haya yanaweza kuwa msaada kwako.
Mkuu upo safi
Ila hapa ni nyeegee
 
Juzi jumatano nilikua namnunulia mtu voucher kwenye max malipo ya elfu 10 nikakosea namba ikaenda kwa mtu mwingine. Leo asubuhi nilikua namtumia dogo hela nikakosea hapa nasubiri ndani ya hizi siku 3 irudishwe hiyo hela maana ilikua ni hela ya dogo nimepewa na mtu nimpe ikapitishwa kwangu.
Kinachoniuma zaidi ni sasa hivi nilikua nalipia tena king'amuzi nimekosea namba elfu 69 yangu imeenda na maji.
Inawezekana nina mawazo sana bila kujijua ndo maana nakosea sana au nimekua mzembe tu? Maana hali Hii si kawaida kabisa
Mh hiyo ngum kumeza aisee. Itakuwa kuna MTU mwingine anakukontrol mikono na mawazo Yako. Omba dua
 
Juzi jumatano nilikua namnunulia mtu voucher kwenye max malipo ya elfu 10 nikakosea namba ikaenda kwa mtu mwingine. Leo asubuhi nilikua namtumia dogo hela nikakosea hapa nasubiri ndani ya hizi siku 3 irudishwe hiyo hela maana ilikua ni hela ya dogo nimepewa na mtu nimpe ikapitishwa kwangu.
Kinachoniuma zaidi ni sasa hivi nilikua nalipia tena king'amuzi nimekosea namba elfu 69 yangu imeenda na maji.
Inawezekana nina mawazo sana bila kujijua ndo maana nakosea sana au nimekua mzembe tu? Maana hali Hii si kawaida kabisa
punguza mawazo jomba, jana nimeenda ktk ATM nlisahau password ikamezwa [emoji16] [emoji16]

ila mda uleule wakanitolea nkarudia tena mambo yakawa murua,,
 
Back
Top Bottom