Ni muda muafaka uvaaji wa barakoa uwe jambo la lazima kwenye umma

Ni muda muafaka uvaaji wa barakoa uwe jambo la lazima kwenye umma

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Watu huangamia kwa kukosa maarifa, lakini watu huangamia kwa upumbavu wao au kiburi chao.

Sisi kama Taifa na dunia kiujumla tunalo la kujifunza kutoka Uchina na nchi za Asia, kulekule ambapo ugonjwa wa Korona ulianzia! Wao waliweka sheria ya lazima kuvaa mask ukitoka nje na hiyo sheria ilikuwa very strict. Na kwa kweli hii ilielekea kuona rate ya maambukizi ikipungua siku baada ya siku mpaka wakawa katika hali inayoridhisa.

Wazungu walicheza makidamakida kwenye ishu ya barakoa, mwanzoni wakawa na mchezo wa "vaa usivae", wakaleta habari zao za "uhuru wa mtu binafsi" lakini sasa korona ilivyokuja kuwatandika kisawasawa ndo wanakumbuka kufanya uvaaji wa barakoa kuwa kitu cha lazima!, Tunaona eti madakatari wao wanashauri watu wavae barakoa doubledouble. Walikumbuka shuka asubuhi.

Sasa sisi kama Taifa hatuna luxury ya kuacha anayetaka avae na asiyetaka asivae.

Hatuna option kwa sababu:

1. Uhai wa mtu mmoja siyo mali yake peke yake ni mali ya Taifa, ndiyo maana kutaka kujiua ni kosa la jinai

2. Pili kuvaa barakoa hakumnusuru mvaaji asiambukizwe bali kunawanusuru wengine pia ambao huenda wangeambukizwa na mvaa barakoa kama ana huo ugonjwa.

3. Gharama za kupoteza mwabanchi mmoja na kwa Taifa zima ni kubwa, maana unakuta mtu ndo mlisha familia, mlipa kodi kwa serikali, daktari, mwalimu, injinia, Lecturer, mhasibu etc. Ni ujinga kutoona madhara kwa nchi kutokana na vifo vya mtu mmoja mmoja

Sasa huu siyo muda muafaka wa serikali kuendelea na approach zake za kusuasua, au za "hayanihusu kila mtu apambane na hali yake", Ni lazma serikali itimize wajibu wake wa kikatiba wa kulinda uhai wa wananchi.

Chombo kuitwa serikali maana yake ni chombo cha nguvu kwa ajili ya common good. Nchi haiwi na wanajeshi, polisi, mgambo na usalama kwa ajili ya kuweka gwaride zuri tu kwa ajili ya mtawala, baki hivi ni vyombo vya kulinda uhuru, mali na uhai wa wananchi pindi vikiwa called ob duty. Kwa hiyo kupitia vyombo hivi kwa kushirikiana na wananchi suala la kufanya uvaaji wa barakoa kuwa ni jambo la lazima linawezekana na ndiyo njia sahihi kwa sasa ili kuzuia usambaaji wa kirusi kama moto wa kiangazi.

Raisi Magufuli akumbuke tu kuwa pale alipoapishwa, alipewa ngao na mkuki, ile ngao siyo urembo, ile ni ishara kuwa ni lazima atumie uwezo wake wote kuhakikisha analilinda taifa dhidi ya hatari yoyote inayotishia maisha ya watu wake.

Hii approach ya Rais Magufuli kupigana vita ya Korona kwa shingo upande ni staili ya upiganaji legelege na ni aibu kwa kiongozi aliyeapa kulinda katiba inayotamka kuhusu haki ya kuishi kuwa legelege kwenye kulinda uhai wa watu wake.

Viongozi wa Magufuli hawaishi kwa mfano kwenye vita hii, na kwa tabia zao za kutovaa barakoa, kutoweka social distance, kuzungumiza uwepo wa korona kwa kudonyoadonyoa, kutopiga kampeni ya kuelimisha umma juu ya hatari hii kama jinsi tulivyowahi kuona kampeni mbalimbali za kitaifa zikifanywa ni aibu kubwa.

Just Imagine kuna kipindi serikali ilikuwa ikinenga awareness kubwa juu ya ugonjwa wa Tezi Dume, Mabusha etc lakini serikali hiyohiyo haitaki kuendesha kampeni kubwa kwenye vyombo vya habari vya kuelimisha umma juu ya hatari ya gonjwa hili linavyoua.

Yaani laiti muda ambao TBC wanautumia kumsifu Magufuli ungekuwa unatumika kujenga public awareness ya ugo jwa huu hakika tungeupiga vita vizuri zaidi.

Sasa Serikali iachane na denial, na iache uyageuza maisha ya watanzania sinema.
 
Viongozi wa Magufuli hawaishi kwa mfano kwenye vita hii, na kwa tabia zao za kutovaa barakoa, kutoweka social distance, kuzungumiza uwepo wa korona kwa kudonyoadonyoa, kutopiga kampeni ya kuelimisha umma juu ya hatari hii kama jinsi tulivyowahi kuona kampeni mbalimbali za kitaifa zikifanywa ni aibu kubwa.
Huenda wengine wameshapata chanjo, acheni kuwa mafala wa Tz piganieni uhai wenu msiuweke rehani mikononi mwa mtu/watu.
 
Wenzako wanakwambia Corona ile phase ya kwanza ilimalizwa na maombi, sasa kiumbe mwenye mawazo kama haya unadhani utamvalisha vipi barakoa? lakini unakuta mtu huyo anayejisifu kwa maombi akipata ugonjwa mwingine anakimbilia hospitali, huu ujinga wa hawa watu sijui wameurithi toka wapi.
 
Wenzako wanakwambia Corona ile phase ya kwanza ilimalizwa na maombi, sasa kiumbe mwenye mawazo kama haya unadhani utamvalisha vipi barakoa? lakini unakuta mtu huyo anayejisifu kwa maombi akipata ugonjwa mwingine anakimbilia hospitali, huu ujinga wa hawa watu sijui wameurithi toka wapi.
Ujinga ni kuziba pua na mdomo,alafu unaacha macho wazi! Ikiwa virus wa Corona wanaweza kutwa hadi kwenye njia ya haja kubwa,watashindwa kupenya machoni!!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
wadada poa wa Sinza nao wava barakoa, pia nyumba za kulala wazinzi[GESTI HOUSE ] waweke Condom na barakoa kwenye kila chumba
 
Kila mtu ana njia yake aliyoichagua ya kudili na Covid, ki Dunia mpaka Sasa hakuna njia ya uhakika kwa 100%. Wengine tumechagua kutovaa barakoa Ila kila siku tunapiga tangawizi + limao vya Moto asubuhi na jioni na tunadunda. Ila hatuvai barakoa na maisha yanaenda. Wewe na wenzako mmechagua kuvaa barakoa ndo njia ya kisayansi mnayoiamini kwasababu mzungu kasema. Swali ni mbona sisi hatuwakomalii mpige tangawizi/limao+nyungu kama nyie mnavyotukomalia na barakoa?????... Mimi nasema kila mtu akomae na njia anazoamini zitamnusuru. Muache kulazimisha kwasababu unaamini mzungu yupo sahihi na barakoa ndo kila mtu aamini hivyo. Kama Covid ingekuwa tishio Kama mnavyoeleza wanaoudhuria kwenye viwanja vya soka tangu December 2020 wangekuwa wamekufa hata robo. Ila Mimi ni mmojawapo na nadunda tu. Msitake kila mtu afanye unachoona ni sahihi kwako. Wengine tulio wengi hatuamini hayo ma barakoa, na nature inazidi kuwaumbua. Endeleeni kuvaa barakoa Ila msilazimishe kila mtu afuate nyayo zenu.
 
Serikali hauwezi kupoteza Muda na vijimafua visivyoweza kuua hata kuku!!!
 
Kuvaa barakoa inaokoa kiasi flani usipate maambukizi ya magonjwa kwa njia ya upumuaji hasa maeneo yenye hali ya hewa isiyo na joto kama Arusha, Mbeya, Iringa nk. Lakini kwa maeneo ambayo hali yake ya hewa ni joto kali kama mikoa ya Dsm na Pwani uvaaji wa barakoa katika mikoa hiyo kwa muda mrefu pia ni hatari sana kwa afya, kwa sababu unaweza ukawa kwenye kazi zako huku jua linakupiga mara unaanza kusinzia sinzia kwa sababu hewa ni ndogo kinachofuata ni kuanguka chini ukazimia au ukafa kabisa.
 
Kila mtu ana njia yake aliyoichagua ya kudili na Covid, ki Dunia mpaka Sasa hakuna njia ya uhakika kwa 100%. Wengine tumechagua kutovaa barakoa Ila kila siku tunapiga tangawizi + limao vya Moto asubuhi na jioni na tunadunda. Ila hatuvai barakoa na maisha yanaenda. Wewe na wenzako mmechagua kuvaa barakoa ndo njia ya kisayansi mnayoiamini kwasababu mzungu kasema. Swali ni mbona sisi hatuwakomalii mpige tangawizi/limao+nyungu kama nyie mnavyotukomalia na barakoa?????... Mimi nasema kila mtu akomae na njia anazoamini zitamnusuru. Muache kulazimisha kwasababu unaamini mzungu yupo sahihi na barakoa ndo kila mtu aamini hivyo. Kama Covid ingekuwa tishio Kama mnavyoeleza wanaoudhuria kwenye viwanja vya soka tangu December 2020 wangekuwa wamekufa hata robo. Ila Mimi ni mmojawapo na nadunda tu. Msitake kila mtu afanye unachoona ni sahihi kwako. Wengine tulio wengi hatuamini hayo ma barakoa, na nature inazidi kuwaumbua. Endeleeni kuvaa barakoa Ila msilazimishe kila mtu afuate nyayo zenu.
Tarizo mnakuwa selfish. Kwa kuwa wewe binafsi Corona haikudhury kwa sababu unapiga matangawizi na vitu unavyoviamini hauangalii fact kuwa wewe unaweza kuwa na virusi ukaambukiza wengine ambao vitawadhuru.

Ninaona umimi umimi umimi mwingi sana kwenye hii issue ya covid

It may not affect you but you may spread it to others if you caugh, umewahi kufikiria hilo?
 
Watu huangamia kwa kukosa maarifa, lakini watu huangamia kwa upumbavu wao au kiburi chao.

Sisi kama Taifa na dunia kiujumla tunalo la kujifunza kutoka Uchina na nchi za Asia, kulekule ambapo ugonjwa wa Korona ulianzia! Wao waliweka sheria ya lazima kuvaa mask ukitoka nje na hiyo sheria ilikuwa very strict. Na kwa kweli hii ilielekea kuona rate ya maambukizi ikipungua siku baada ya siku mpaka wakawa katika hali inayoridhisa.

Wazungu walicheza makidamakida kwenye ishu ya barakoa, mwanzoni wakawa na mchezo wa "vaa usivae", wakaleta habari zao za "uhuru wa mtu binafsi" lakini sasa korona ilivyokuja kuwatandika kisawasawa ndo wanakumbuka kufanya uvaaji wa barakoa kuwa kitu cha lazima!, Tunaona eti madakatari wao wanashauri watu wavae barakoa doubledouble. Walikumbuka shuka asubuhi.

Sasa sisi kama Taifa hatuna luxury ya kuacha anayetaka avae na asiyetaka asivae.

Hatuna option kwa sababu:

1. Uhai wa mtu mmoja siyo mali yake peke yake ni mali ya Taifa, ndiyo maana kutaka kujiua ni kosa la jinai

2. Pili kuvaa barakoa hakumnusuru mvaaji asiambukizwe bali kunawanusuru wengine pia ambao huebda wangeamvukizwa na mvaa barakoa kama ana huo ugonjwa.

3. Gharama za kupoteza mwabanchi mmoja na kwa Taifa zima ni kubwa, maana unakuta mtu ndo mlisha familia, mlipa kodi kwa serikali, daktari, mwalimu, injinia, Lecturer, mhasibu etc. Ni ujinga kutoona madhara kwa nchi kutokana na vifo vya mtu mmoja mmoja

Sasa huu siyo muda muafaka wa serikali kuendelea na approach zake za kusuasua, au za "hayanihusu kila mtu apambane na hali yake", Ni lazma serikali itimize wajibu wake wa kikatiba wa kulinda uhai wa wananchi.

Chombo kuitwa serikali maana yake ni chombo cha nguvu kwa ajili ya common good. Nchi haiwi na wanajeshi, polisi, mgambo na usalama kwa ajili ya kuweka gwaride zuri tu kwa ajili ya mtawala, baki hivi ni vyombo vya kulinda uhuru, mali na uhai wa wananchi pindi vikiwa called ob duty. Kwa hiyo kupitia vyombo hivi kwa kushirikiana na wananchi suala la kufanya uvaaji wa barakoa kuwa ni jambo la lazima linawezekana na ndiyo njia sahihi kwa sasa ili kuzuia usambaaji wa kirusi kama moto wa kiangazi.

Raisi Magufuli akumbuke tu kuwa pale alipoapishwa, alipewa ngao na mkuki, ile ngao siyo urembo, ile ni ishara kuwa ni lazima atumie uwezo wake wote kuhakikisha analilinda taifa dhidi ya hatari yoyote inayotishia maisha ya watu wake.

Hii approach ya Rais Magufuli kupigana vita ya Korona kwa shingo upande ni staili ya upiganaji legelege na ni aibu kwa kiongozi aliyeapa kulinda katiba inayotamka kuhusu haki ya kuishi kuwa legelege kwenye kulinda uhai wa watu wake.

Viongozi wa Magufuli hawaishi kwa mfano kwenye vita hii, na kwa tabia zao za kutovaa barakoa, kutoweka social distance, kuzungumiza uwepo wa korona kwa kudonyoadonyoa, kutopiga kampeni ya kuelimisha umma juu ya hatari hii kama jinsi tulivyowahi kuona kampeni mbalimbali za kitaifa zikifanywa ni aibu kubwa.

Just Imagine kuna kipindi serikali ilikuwa ikinenga awareness kubwa juu ya ugonjwa wa Tezi Dume, Mabusha etc lakini serikali hiyohiyo haitaki kuendesha kampeni kubwa kwenye vyombo vya habari vya kuelimisha umma juu ya hatari ya gonjwa hili linavyoua.

Yaani laiti muda ambao TBC wanautumia kumsifu Magufuli ungekuwa unatumika kujenga public awareness ya ugo jwa huu hakika tungeupiga vita vizuri zaidi.

Sasa Serikali iachane na denial, na iache uyageuza maisha ya watanzania sinema.
Siamini katika kulazimisha watu kuvaa barakoa, ninaamini katika kuwaelimisha. Tulifanya hivyo kwenye suala la UKIMWI na tumefanikisha kwa kiwango kikubwa. Hatukulazimisha wapenzi wasiingiliane, wala wanao oana kupima, au wenye UKIMWI kutozaa n.k.

Ukweli ni kwamba, ukitaka kuvaa barakoa kuwe lazima kwa wote ni lazima uunde sheria itayoweza kumshtaki asiyefanya hivyo. Hapa matatizo ni mengi.
  • Hatuna polisi wataotosha kutekeleza hilo, kuwashika wasiovaa barakoa na kuwafikisha mahakamani
  • Hatuna mahakama za kutosha kuendesha kesi hizo
  • Hatuna nafasi huko magereza za kukaa wafungwa hao, na ndio maana sasa hivi misamaha mingi inatolewa.
  • Kuvaa barakoa sio 100% kuwa hutapata korona.
Kwa hiyo la muhimu ni kuelimishana katika kuzingatia mambo makuu yafuatayo:
  • Kuutangaza ugonjwa huu wa COVID-19 kitaifa kuwa upo na unaua. Hii ifanywe na Mkuu wa nchi Rais wa JMT.
  • Waziri wa Afya aandae muongozo wa uelimishaji wa COVID-19 kwa Tanzania nzima.
  • Vipimo vya upimaji COVID-19 viwepo hospitali zote
  • Takwimu zitolewe ili tujue eneo lipi kwa leo limeathirika sana. Nia kubwa ni kupunguza maambukizi kwa mwananchi kujiuliza kama anaumuhimu wa kwenda huko kwenye ujazo wa maambukizi.
  • Kutojitenga na dunia, kumbuka Tanzaania sio kisiwa.
Kwa hayo madogo tu tutaupunguza huu ugonjwa kwa asilimia karibu 50.
 
Back
Top Bottom