SoC02 Ni muda muafaka wa kuinua vilivyo vyetu

SoC02 Ni muda muafaka wa kuinua vilivyo vyetu

Stories of Change - 2022 Competition

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2022
Posts
221
Reaction score
197
NI MUDA MUAFAKA WA KUINUA VILIVYO VYETU.

Utangulizi.

Mpaka sasa, kumekuwa na imani hafifu kwa watanzania hasa linapokuja suala la kukubali vitu mbalimbali vinavyotengenezwa au kuzalishwa na raia kutoka nchini. Imani hii hafifu imekwenda mbali zaidi hadi kufikia hatua ya kudharau na kukandamiza baadhi ya huduma au bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa nchini, hivyo kupelekea kuwepo na ushindani uliokithiri kati ya bidhaa za ndani dhidi ya bidhaa za nje. Huku ikionekana dhahiri bidhaa zilizotengenezwa nchini kukosa soko zaidi ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje ya nchi.

Baadhi ya maeneo ambayo yanaonekana kupokea upinzani mkubwa kutoka kwa wazawa.
Ni ukweli usiopingika kuwa kuna baadhi ya maeneo mengi ambayo yamepoteza imani kwa Watanzania licha ya kujitahidi katika kutoa huduma au bidhaa bora kwa watanzia. Baadhi ya maeneo hayo ni kama ifuatavyo;
  • Viwanda vya bidhaa za majumbani, kuna viwanda vingi nchini Tanzania vilivyojikita katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zitumikazo majumbani kama vile sabuni, samani. Hizi ni baadhi ya bidhaa ambazo zinazalishwa kwa wingi nchini Tanzania, lakini mapokeo ya baadhi ya watanzania yamekuwa ni tofauti huku wengi wakiamini bidhaa hizo si bora ukilinganisha na zile zinazoagizwa nje ya nchi.
  • Viwanda vya bidhaa kama nguo, viatu pamoja na vitu vya urembo kama nywele bandia. Pia linapokuja suala la bidhaa hizi, bado inaonekana kuwa kuna upinzani mkubwa wa wananchi kukubali bidhaa hizi huku wengi wakiamini zaidi bidhaa zinazotoka nje. Mfano, nguo au viatu vya mtumba.
  • Huduma mbalimbali za kijamii kama vile elimu, afya n.k. Pamoja na serikali kuonesha jitihada zake katika kuboresha huduma za kijamii bado kuna baadhi ya wananchi ambao hawana imani thabiti juu ya huduma hizo. Mfano, wananchi wengi huamini zaidi huduma za afya au elimu zinazotolewa nje ya nchi hata kama ni nchi ambayo iko nyuma kiuchumi ukilinganisha na Tanzania.
  • Sekta ya michezo, sambamba na yote bado wananchi wengi hawana imani juu ya ubora wa michezo yetu ya ndani. Mfano dhahiri huonekana hata kwa mashabiki ambavyo hujenga imani kubwa kwa wachezaji wanaotoka nje ya nchi hata kama viwango vyao kuwa sawa na wachezaji wa ndani ya nchi.

Je, ukweli ni upi juu ya suala hili?
Ukweli ni kuwa kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea mambo haya kuonekana kwa wananchi, baadhi ya mambo hayo ni kama ifuatavyo;
  • Uchakachuaji wa bidhaa unaofanywa na baadhi ya wazalishaji. Kuna baadhi ya wamiliki wa viwanda wamekuwa wakizalisha bidhaa ambazo ni dhahiri kuwa zimechakachuliwa, hii kupelekea kutodumu kwa muda mrefu. Jambo hili limefanya wananchi wengi kuondoa imani hata kwa baadhi ya wazalishaji wa nchini ambao bidhaa zao ni halisi na zenye ubora wa hali ya juu.
  • Gharama za upatikanaji wa bidhaa zinazozalishwa nchini. Ukweli ni kwamba, baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini huonekana ni aghali mno ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje ya nchi jambo hili limefanya wananchi wengi kususia bidhaa za ndani na kupendelea zaidi bidhaa zinazotoka nje ya nchi.
  • Nguvu ya ushawishi kutoka kwa watu mashuhuri. Pia kumekuwepo na kasumba ya kufuata mkumbo kwa baadhi ya watu mashuhuri katika kufanya jambo fulani. Mfano dhahiri huonekana kwa baadhi ya watu ambao hupendelea kutumia vilevi kutoka nje ya nchi kwa sababu vimeonekana vikitumika na wasanii wakubwa, mf. Pombe aina ya Hennessy, Jack Daniels, Russian Vodka, jambo ambalo limedidimiza vilevi/vinywaji vinavyozalishwa nchini.

Je, ni kipi kifanyike ili kuondoa tatizo hili kwa Watanzania?
Ni dhahiri kuwa wahenga waliposema “ukiona vya elea ujue vimeundwa” hakika walikuwa sahihi, ni wakati wetu sasa wa kuinua vilivyo vyetu hususani katika kipindi hiki ambacho bidhaa nyingi zimeonekana kupanda bei kutokana na migogoro iliyopo baina mataifa makubwa tegemezi.Vifuatavyo ni baadhi ya vitu vinavyotakiwa kutiliwa mkazo ili kuinua thamani ya bidhaa zetu nchini;
  • Utiliaji mkazo katika ukaguzi wa bidhaa kabla hazijamfikia mtumiaji. Licha ya kuwepo kwa kaguzi mbalimbali bado kuna baadhi ya wazalishaji ambao wamekuwa wakitumia njia za panya katika kupitisha bidhaa zao sokoni. Hivyo ni wakati thabiti wa serikali kupitia taasisi yake husika kuongeza mkazo juu ya suala hili kwa kuziba mianya yote batilifu ili kuongeza upatikanaji wa bidhaa au huduma bora kwa wananchi.
  • Uwiano wa bei baina ya bidhaa zinazozalishwa nchini na zile zinazotoka nje. Suala la bidhaa kuwa na bei kubwa hutokana na sababu mbalimbali kama vile tozo za kodi kutoka katika mamlaka husika, ubora pamoja na upatikanaji wake. Ni muda muafaka wa serikali kutoa msaada kwa wazalishaji wazawa ili kuongeza ushindani kwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi.
  • Kuinua viwanda vidogovidogo vilivyopo nchini. Pia ili kuonesha nia ya kuthamini bidhaa zetu ni wakati muafaka wa serikali pamoja na mashirika binafsi kuweka mikakati thabiti itakayolenga kuinua viwanda vidogovidogo vinavyozalisha bidhaa mbalimbali ili kuendana na soko la ushindani juu ya bidhaa zingine.
  • Kuongeza juhudi katika kuwahusisha watu mashuhuri au wenye ushawishi wa hali ya juu katika matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini. Mfano matangazo ya bidhaa kama vile vinywaji, mavazi, sabuni n.k. hii itasaidia katika kuvuta imani za watu juu ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini.
  • Uboreshaji wa matamasha mbalimbali yanayohusu maonesho mbalimbali ya bidhaa kutoka kwa wajasiriamali. Hii ni pamoja na kuweka mashindano mbalimbali kwa wabunifu/watengenezaji wa bidhaa mbalimbali ili kutia chachu katika uboreshaji wa huduma au bidhaa zao.
  • Sambamba na yote, ni wakati wetu pia kudumisha uzalendo kwa kukubali na kupenda huduma au bidhaa zinazozalishwa nchini. Yote yanaweza kufanyika lakini likabakia suala la uzalendo kwani hili ndio jambo kuu katika kuona thamani ya vilivyo vyetu. Kwa sababu kupitia uzalendo ni dhahiri kuwa tunaweza kushirikiana kwa pamoja katika kuimarisha misingi itakayotuwezesha kuwepo kwa uzalishwaji wa bidhaa au utolewaji wa huduma bora nchini. Mfano kuripoti baadhi ya taarifa zinazohusu bidhaa feki au huduma zitolewazo kwa kiwango cha chini.
Kwa ujumla, ni ukweli usiopingika kuwa tunao uwezo na nguvu ya kushindana katika masoko mbalimbali duniani endapo tu tutakapo kubali kuwa huduma na bidhaa zetu ni bora kama zilivyo zingine. Hivyo ni wakati wetu sahihi wa kukubali na kuthamini vilivyo vyetu kwani hata hayati Dr. John Pombe Magufuli aliwahi kusema kuwa “ni lazima tuipende nchi yetu, kwani hatuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania”.
 
Upvote 28
IDEAS ZA KUTOKA KIMAISHA KWA MTAJI MDOGO


1.Nunua pikipiki ya Dhamana ukaanza biashara ya Boda boda.
2.Fungua saluni
3.Mradi wa tofali za kuchoma
3.Fuga kuku
4.Somea ujuzi wowote
5.Mradi wa kushona nguo
6.kijiwe cha kuchomelea
7.kijiwe cha milango na madirisha ya aluminum
8.Mgahawa Mdogo
9.Kijjwe cha kahawa
10.Mashine ya kupukuchua mazao mfano mahindi, mpunga, mtama, karanga, nk
11.Mashine ya kukata nyasi, kupalilia
12.Kuuza mbuzi, kuku,
13.Biashara ya mazao.
14.kukodi bus, daladala na kuzisimamia upate cha juu
15.Kutengeneza sabuni, sanitizer, handwash,
16.Kutengeneza unga wa lishe
17.Kilimo cha umwagailiaji water pump, mbegu, madawa
18.Jiko la supu
19.kutengeneza mkaa mbadala
20.Kuuza chips
21.Kukaanga kuku
22.Kutengeneza vitafunio
23.Kuzalisha ethanol
24.kufuga poko mbuzi katoliki
25.Kufungua kilabu cha pombe za kienyeji
26.Kufungua vijiwe vya Kukusanya ubuyu maporini yakitimia magunia unaleta mjini
27.Kuuza juice
28.Kuuza juice ya miwa
29.Kijiwe cha kukaanga samaki jioni
30.Shughuli za upambaji kumbi
31.Kusambaza bidhaa majumbani
32.Kusambaza bidhaa basic needs kwenye maduka ya vijijini yaani unanua mjini unasambaza kwa oda viduka vya vijijini.
33.Kuzunguka minadani kuuza nguo za mitumba, vyombo, nk
34.Kufungua tuition center
35.Kufungua grocery
36.Kuwa wakala wa bidhaa za viwandani
37.kijiwe cha kukusanya taka za plastic, chuma,oil chafu na tairi chakavu.
38.Kufungua genge la kuuza basic home need
39.Kufungua ofisi ya kupiga nguo pasi.
40.Ofisi ya kutengeneza viatu na mabegi
41.Kutengeneza vyombo vya kupikia mfano, majiko, ndoo, sufuria, mifuniko, vikaangio, nk
42.Saluni ya kutengeneza kucha za wanawake
43......Jengea vyumba vitatu wazazi wako nyumba ya Bati upate baraka
44..Nunua shamba
45.Nunua ng'ombe wadogo watano kwa laki na nusu anza ufugaji.
Au nunua mbuzi anza kufuga
46.Fungua kijiwe cha kuonyesha mpira
47.duka la nguo za kupoint classic za mitumba piga pasi tundika kwenye enga
48..Ofisi za baiskeli za kukodi hapo unapata baiskeli nane
49..Duka la spea za pikipiki na baiskeli
50.Duka la dawa na vipodozi
51..ofisi ya kuchaji simu kwa sola vijijini
52..ofisi ya uwakala wa kutuma na kutoa pesa
53.. Bustani za kuzalisha miche ya miti na matunda
54... Ufugaji nyuki na kuuza asali
55.. Kuzalisha unga wa muhogo
56..Direct sale yaani door to door delivery hapa unakuwa na torori na speaker unapita KILA nyumba unauza bidhaa na kuchukua oda ya nini wanataka Ili kesho uwaletee.
57.Utengenezaji pellets chakula cha mifugo,samaki.
58..unga wa lishe
59..mikeka
60.bidhaa za mianzi.
61.wine,
62.usafi wa majumbani
63.kuuza uji wa ulezi,mchele
64.utengenezaji mbolea za mboji na za maji.
65.utengenezaji wa vigae vya cement na vya udongo.
66.kupanda miti kwa ajili ya nguzo na mirunda
67.utengenezaji wa ndala
68.utengenezaji viatu
69.Upondaji kokoto
70.ufundi simu na radio
71
Haua madini nimeyapenda ofcourse kuna moja apaaaa ai basiii tu
 
Karibuni tuendeleze mjadala wetu pendwa wana JamiiForums
 
Bidhaa ikiwa nzuri watu watatumia.
Mbona watu wamehamia kwenye samani local made
Yaaaap ni kweli kabisa naamin wote wakifany hivy tutafika mbali sana
Pia kura yako muhimu mkuu Vote^
 
Chapisho maridhawa, nalipa kura yangu. Hata hivyo naomba maoni yako na ikikupendeza kura yako kwenye chapisho langu
" SoC 2022 - Watu Maarufu na Bidhaa za Wanyonge" lililopo mtandaoni.

Asante.
 
U
NI MUDA MUAFAKA WA KUINUA VILIVYO VYETU.

Utangulizi.
Mpaka sasa, kumekuwa na imani hafifu kwa watanzania hasa linapokuja suala la kukubali vitu mbalimbali vinavyotengenezwa au kuzalishwa na raia kutoka nchini. Imani hii hafifu imekwenda mbali zaidi hadi kufikia hatua ya kudharau na kukandamiza baadhi ya huduma au bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa nchini, hivyo kupelekea kuwepo na ushindani uliokithiri kati ya bidhaa za ndani dhidi ya bidhaa za nje. Huku ikionekana dhahiri bidhaa zilizotengenezwa nchini kukosa soko zaidi ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje ya nchi.

Baadhi ya maeneo ambayo yanaonekana kupokea upinzani mkubwa kutoka kwa wazawa.
Ni ukweli usiopingika kuwa kuna baadhi ya maeneo mengi ambayo yamepoteza imani kwa Watanzania licha ya kujitahidi katika kutoa huduma au bidhaa bora kwa watanzia. Baadhi ya maeneo hayo ni kama ifuatavyo;

  • Viwanda vya bidhaa za majumbani, kuna viwanda vingi nchini Tanzania vilivyojikita katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zitumikazo majumbani kama vile sabuni, samani. Hizi ni baadhi ya bidhaa ambazo zinazalishwa kwa wingi nchini Tanzania, lakini mapokeo ya baadhi ya watanzania yamekuwa ni tofauti huku wengi wakiamini bidhaa hizo si bora ukilinganisha na zile zinazoagizwa nje ya nchi.
  • Viwanda vya bidhaa kama nguo, viatu pamoja na vitu vya urembo kama nywele bandia. Pia linapokuja suala la bidhaa hizi, bado inaonekana kuwa kuna upinzani mkubwa wa wananchi kukubali bidhaa hizi huku wengi wakiamini zaidi bidhaa zinazotoka nje. Mfano, nguo au viatu vya mtumba.
  • Huduma mbalimbali za kijamii kama vile elimu, afya n.k. Pamoja na serikali kuonesha jitihada zake katika kuboresha huduma za kijamii bado kuna baadhi ya wananchi ambao hawana imani thabiti juu ya huduma hizo. Mfano, wananchi wengi huamini zaidi huduma za afya au elimu zinazotolewa nje ya nchi hata kama ni nchi ambayo iko nyuma kiuchumi ukilinganisha na Tanzania.
  • Sekta ya michezo, sambamba na yote bado wananchi wengi hawana imani juu ya ubora wa michezo yetu ya ndani. Mfano dhahiri huonekana hata kwa mashabiki ambavyo hujenga imani kubwa kwa wachezaji wanaotoka nje ya nchi hata kama viwango vyao kuwa sawa na wachezaji wa ndani ya nchi.

Je, ukweli ni upi juu ya suala hili?
Ukweli ni kuwa kuna sababu kadha wa kadha zinazopelekea mambo haya kuonekana kwa wananchi, baadhi ya mambo hayo ni kama ifuatavyo;

  • Uchakachuaji wa bidhaa unaofanywa na baadhi ya wazalishaji. Kuna baadhi ya wamiliki wa viwanda wamekuwa wakizalisha bidhaa ambazo ni dhahiri kuwa zimechakachuliwa, hii kupelekea kutodumu kwa muda mrefu. Jambo hili limefanya wananchi wengi kuondoa imani hata kwa baadhi ya wazalishaji wa nchini ambao bidhaa zao ni halisi na zenye ubora wa hali ya juu.
  • Gharama za upatikanaji wa bidhaa zinazozalishwa nchini. Ukweli ni kwamba, baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini huonekana ni aghali mno ukilinganisha na bidhaa zinazotoka nje ya nchi jambo hili limefanya wananchi wengi kususia bidhaa za ndani na kupendelea zaidi bidhaa zinazotoka nje ya nchi.
  • Nguvu ya ushawishi kutoka kwa watu mashuhuri. Pia kumekuwepo na kasumba ya kufuata mkumbo kwa baadhi ya watu mashuhuri katika kufanya jambo fulani. Mfano dhahiri huonekana kwa baadhi ya watu ambao hupendelea kutumia vilevi kutoka nje ya nchi kwa sababu vimeonekana vikitumika na wasanii wakubwa, mf. Pombe aina ya Hennessy, Jack Daniels, Russian Vodka, jambo ambalo limedidimiza vilevi/vinywaji vinavyozalishwa nchini.

Je, ni kipi kifanyike ili kuondoa tatizo hili kwa Watanzania?
Ni dhahiri kuwa wahenga waliposema “ukiona vya elea ujue vimeundwa” hakika walikuwa sahihi, ni wakati wetu sasa wa kuinua vilivyo vyetu hususani katika kipindi hiki ambacho bidhaa nyingi zimeonekana kupanda bei kutokana na migogoro iliyopo baina mataifa makubwa tegemezi.Vifuatavyo ni baadhi ya vitu vinavyotakiwa kutiliwa mkazo ili kuinua thamani ya bidhaa zetu nchini;

  • Utiliaji mkazo katika ukaguzi wa bidhaa kabla hazijamfikia mtumiaji. Licha ya kuwepo kwa kaguzi mbalimbali bado kuna baadhi ya wazalishaji ambao wamekuwa wakitumia njia za panya katika kupitisha bidhaa zao sokoni. Hivyo ni wakati thabiti wa serikali kupitia taasisi yake husika kuongeza mkazo juu ya suala hili kwa kuziba mianya yote batilifu ili kuongeza upatikanaji wa bidhaa au huduma bora kwa wananchi.
  • Uwiano wa bei baina ya bidhaa zinazozalishwa nchini na zile zinazotoka nje. Suala la bidhaa kuwa na bei kubwa hutokana na sababu mbalimbali kama vile tozo za kodi kutoka katika mamlaka husika, ubora pamoja na upatikanaji wake. Ni muda muafaka wa serikali kutoa msaada kwa wazalishaji wazawa ili kuongeza ushindani kwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi.
  • Kuinua viwanda vidogovidogo vilivyopo nchini. Pia ili kuonesha nia ya kuthamini bidhaa zetu ni wakati muafaka wa serikali pamoja na mashirika binafsi kuweka mikakati thabiti itakayolenga kuinua viwanda vidogovidogo vinavyozalisha bidhaa mbalimbali ili kuendana na soko la ushindani juu ya bidhaa zingine.
  • Kuongeza juhudi katika kuwahusisha watu mashuhuri au wenye ushawishi wa hali ya juu katika matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini. Mfano matangazo ya bidhaa kama vile vinywaji, mavazi, sabuni n.k. hii itasaidia katika kuvuta imani za watu juu ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini.
  • Uboreshaji wa matamasha mbalimbali yanayohusu maonesho mbalimbali ya bidhaa kutoka kwa wajasiriamali. Hii ni pamoja na kuweka mashindano mbalimbali kwa wabunifu/watengenezaji wa bidhaa mbalimbali ili kutia chachu katika uboreshaji wa huduma au bidhaa zao.
  • Sambamba na yote, ni wakati wetu pia kudumisha uzalendo kwa kukubali na kupenda huduma au bidhaa zinazozalishwa nchini. Yote yanaweza kufanyika lakini likabakia suala la uzalendo kwani hili ndio jambo kuu katika kuona thamani ya vilivyo vyetu. Kwa sababu kupitia uzalendo ni dhahiri kuwa tunaweza kushirikiana kwa pamoja katika kuimarisha misingi itakayotuwezesha kuwepo kwa uzalishwaji wa bidhaa au utolewaji wa huduma bora nchini. Mfano kuripoti baadhi ya taarifa zinazohusu bidhaa feki au huduma zitolewazo kwa kiwango cha chini.
Kwa ujumla, ni ukweli usiopingika kuwa tunao uwezo na nguvu ya kushindana katika masoko mbalimbali duniani endapo tu tutakapo kubali kuwa huduma na bidhaa zetu ni bora kama zilivyo zingine. Hivyo ni wakati wetu sahihi wa kukubali na kuthamini vilivyo vyetu kwani hata hayati Dr. John Pombe Magufuli aliwahi kusema kuwa “ni lazima tuipende nchi yetu, kwani hatuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania”.Haswa tuna amini Leo Hali hii tunaweza kuitokomeza kwa kuamini ubora wetu
 
Chapisho maridhawa, nalipa kura yangu. Hata hivyo naomba maoni yako na ikikupendeza kura yako kwenye chapisho langu
" SoC 2022 - Watu Maarufu na Bidhaa za Wanyonge" lililopo mtandaoni.

Asante.
Thanks kiongoziii nalipitiaaa muda huuuuuu, pia asante kwa kushiriki nami
 
Back
Top Bottom