Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Nakumbuka awamu ya tatu wakati serikali ikitaka kununua ndege ya Rais aina ya Gulfstream G550 kwa thamani ya bilioni 46
Watanzania walio wengi, walionyesha kupinga hatua hiyo, kwa kuzingatia hali ya uchumi ya nchi yetu kwa wakati huo
Lakini, aliyekuwa waziri wa fedha wa wakati huo, mzee Basil Pesambili Mramba, alikuja na kauli ya kusema, hata kama watanzania watakula majani, lakini ndege ni lazima inunuliwe , na kweli ndege ikanunuliwa
Lakini baada ya hapo, maisha ya kisiasa ya mzee Mramba, wote tuliona kilichofuata
Ni muhimu sana kwa viongozi wa kisiasa, kuwa makini sana kwenye aina ya maneno tunayotumia kujibu hoja zinazogusa maisha ya watanzania, hasa watanzania wa kipato cha chini
Kama hili la mheshimiwa waziri wetu wa fedha, kujibu wananchi wasiopendezwa na tozo hizi za mihamala ya simu kuhamia nchi jirani, si sawa kabisa
Kwa nafasi yake kama waziri, alipaswa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa tozo hiyo
Uongozi ni dhamana
Watanzania walio wengi, walionyesha kupinga hatua hiyo, kwa kuzingatia hali ya uchumi ya nchi yetu kwa wakati huo
Lakini, aliyekuwa waziri wa fedha wa wakati huo, mzee Basil Pesambili Mramba, alikuja na kauli ya kusema, hata kama watanzania watakula majani, lakini ndege ni lazima inunuliwe , na kweli ndege ikanunuliwa
Lakini baada ya hapo, maisha ya kisiasa ya mzee Mramba, wote tuliona kilichofuata
Ni muhimu sana kwa viongozi wa kisiasa, kuwa makini sana kwenye aina ya maneno tunayotumia kujibu hoja zinazogusa maisha ya watanzania, hasa watanzania wa kipato cha chini
Kama hili la mheshimiwa waziri wetu wa fedha, kujibu wananchi wasiopendezwa na tozo hizi za mihamala ya simu kuhamia nchi jirani, si sawa kabisa
Kwa nafasi yake kama waziri, alipaswa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa tozo hiyo
Uongozi ni dhamana