Ni mwaka wa 6 sasa sijapata ajira ya ualimu TAMISEMI

bora hata wewe umenisaidia manake watu wengi wanauelewa mdogo sana humu ndani yani wanawaza tu kukosoa
Watu huwa wanafurahia ukiteseka.

Pambana mkuu, unaweza kukuta anayekukejeli humu anashindia tumihogo tuwili na chachandu hana mbele wala nyuma (tomboy).

Endelea kujichanganya kama wanavyosema.
 
bora hata wewe umenisaidia manake watu wengi wanauelewa mdogo sana humu ndani yani wanawaza tu kukosoa
usiwazuie watu kukushauri, huo ni ushauri tu bila kujali kwamba umesema au hujasema unajichanganya au la.
 
Wewe umesema ukweli afu anakuja mjinga mmoja anakwambia serikali imeelemewa kwenye kuajiri
 
usiwazuie watu kukushauri, huo ni ushauri tu bila kujali kwamba umesema au hujasema unajichanganya au la.
Sio kwamba nazuiq watu wasinishauri ila watu wengine wanaokosoa kwa kuniona kama mzembe ndio nawamaindi , au wewe ungekuwa mzazi umesomesha kijana wako kwa kujinyima afu miaka 6 hana ajira utajiskiaje , hatukusoma ualimu ili tuje kuuza machungwa, tuliona fursa kuwa walimu wa sayansi hawatoshi ndio tukaingia shule kusoma hivo nnachokiona hapa ni kuwa serikali imetusaliti.
 
Mkuu inasikitisha sana lakini serikali haiwezi kuajiri graduates wote nchini, sahau hilo na ukilielewa hilo ni vizuri.

Hatuna fursa za ajira za kutosheleza wahitimu wote, na hii sio tz tu.
 
Mkuu inasikitisha sana lakini serikali haiwezi kuajiri graduates wote nchini, sahau hilo na ukilielewa hilo ni vizuri.

Hatuna fursa za ajira za kutosheleza wahitimu wote, na hii sio tz tu.
Ndio ni sawa ila utajiskiaje kuona watu wa 2020 wameajiriwa na wa 2017 wameachwa kwa masomo yaleyale
 
Watu huwa wanafurahia ukiteseka.

Pambana mkuu, unaweza kukuta anayekukejeli humu anashindia tumihogo tuwili na chachandu hana mbele wala nyuma (tomboy).

Endelea kujichanganya kama wanavyosema.
kweli kaka
 
Mkuu serikali haiwezi kuajiri graduates wote waliopo mtaani ...kwaio kwa maarifa uliyonayo tena degree holder kabisa wa miaka saba mtaani endelea kufanya unachofanya kwa bidii I hope utafanikiwa zaidi kuliko kwenda kuanza ualimu
 
Na sisi journalist tuseme hivyo 🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…