Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Elections 2010 Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

Status
Not open for further replies.
mimi binafsi na pia watanzania wengi hatumchukii kikwete kwa sababu ni muislam..!

kikwete hana uwezo wa kuongoza dola PERIOD...!!!! anabahati mungu alimpa sura inayovuta kura za akina mama...!
angekuwa na sura kama yangu hata ubalozi wa nyumba kumi hawezi kuongoza..!

HUYU JAMAA ANAFAA KUTUMIWA KAMA MSHENGA ZAIDI....! yani ku-negotiate mahali..! :tape::tape::tape:
 
Katika hali ya kujikanganya dakika za mwisho mwisho mbia wa utawala wa JK na CCM yake, gazeti la Mtanzania limeona kuna uhaja wa kuwatoa wasiwasi wapigakura hisia nzito zilizojengeka miongoni mwa jamii ya kuwa utawala wa JK una udini na kutoa makanusho na kudai kumbe wakristo ni wengi zaidi ya waislamu katika ngazi za baraza la mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.

Tatizo la takwimu hizo ni hizi hapa:-

1) Mtanzania ina dhana potofu ya kuwa idadi ya wakristu na waislamu ni sawa na hivyo kama wakristu ni wengi kweye teuzi za JK basi hakuna udini. Ukweli ni kuwa mrandano wa wastani wa 2 kwa 3 kati ya wakristu na waislamu haujaweza kutoa linganisho sahihi kwa vile uwiano halisi wao katika jamii haufahamiki vizuri.

2) JK anazo teuzi nyingi za wakurugenzi kwenye taasisi mbalimbali za umma na mabalozi ambazo hazimo kwenye taarifa hii ya Mtanzania hivyo ni vigumu kusema JK hana udini kwa taarifa hizo zilizotolewa.

3) Udini siyo tu katika teuzi za Raisi ila udini ni lazima pia upimwe kwa mikakati ya JK na serikali yake ya CCM katika kuanzisha mahakama za Kadhi na kujiunga nchi hii kwa shirika la dini la kislamu la OIC. Yaani misingi ya usawa wa kidini imo hatarani chini ya utawala wa JK

3) Takwimu za Mtanzania ambazo wamepewa kutoka Ikulu zinalenga kufunika ukweli kuwa teuzi za JK karibu zote bila ya kujali dini zimebeza suala zima la tija na halikuzingatia sifa wala vigezo vya kituendaji na matokeo yake kiuchumi kama nchi tunazidi kurudi nyuma
 
ni kweli ulichosema............
KIKWETE,BILAL,KINANA,RIZIWANI,SALMA KIKWETE, SHEIN,NI WAKRISTO....HONGERA MWANDISHI KWA KUWA MPOFU
 
uchambuzi nimeupenda! CCM kama kuna kosa kubwa walilolifanya ni kutolea maelezo hili jambo... watz wa leo sio wa jana.
 
Mjadala kama huu utanoga zaidi endapo utaambatanishwa na orodha ya majina ya maafisa wote walioteuliwa na raisi pamoja na dini zao. Otherwise kila mtu atakuwa anaangalia wateule fulani tu na kusahau wengine.
 
Mara zote mimi nimekuwa napiga vita hisia za udini zinazoendelea kujengeka Tanzania. Kwa nyakati tofouti kama leo nalazimika kuandika kile nisichokipenda kukijadili, lakini kwa faida yetu sote ni lazima tuwe wakweli na weledi.
Ndugu Rutashubanyuma, kauli mbiu yako ni kuwa wewe ni public policy analyst, na ninaanza kuingiwa na shaka juu ya hili hata kama ni kweli.
Kama wewe ni Mtanzania, basi utakuwa hujaipitia vema historia ya nchi yako. Nukta yako ya tatu inanitia wasi wasi kama kweli una nia njema na nchi hii ya Tanzania unayoishi.
Kwanza naomba urejee miaka 23 ya Mwalimu Nyerere uwiano ulikuwaje ili ujenge hoja ya uwiano wa sasa.
Pili, viongozi hawachaguliwi ili kuongoza dini, wao ni public servants, sijui unataka kutuaminisha nini juu ya uteuzi wa viongozi.
Tatu, mbona hujaangalia huko nyuma Nyerere,Mwinyi,Mkapa uteuzi ulikuwaje ili utupe ulinganifu na huu wa sasa.
Nne, Suala la kadhi limeanza kitambo lakini ni wakati wa mkapa ndipo liliposhika kasi, sijui kama unajua aliyeibua hoja ya kadhi na kuifanya agenda ya uchaguzi Ni A.L.Mrema akimtumia sheikh mtopea.!!!
Tano, Mkapa alifanya nini kama kiongozi wa Chama kuzuia hoja ya Kadhi isiingizwe ndani ya ilani 2005. Iweje suala lililopata baraka za chama leo liwe la JK peke yake. Je nani aliandaa ilani ya ccm 2005, na kwanini halmashauri kuu na CC ziliafiki suala la kadhi.
Sita, Suala la OIC lilianza miaka ya akina Mwinyi na Malecela, na kama unakumbuka hili ni miongoni mwa mambo yaliyozaa G55 na hatimaye Mzee Malecela kuwekwa pembeni katiak u-PM. Suala hili liliendelea wakati wa Mkapa, je yeye alilishughulikiaje? na kwanini leo ionekane ni agenda ya JK ili hali viongozi wawili [miaka kumi kumi] hawakulishughulikia!

Napenda kuweka wazi kuwa sijengi hoja kujibu au kufanunua hoja za Gazeti la Tanzania au JK, ninachokifanya hapa ni kutaka kuwafahamisha wana forum wenzangu kuwa ni vema mtu akatuliza akili kabla hajaandika na kuhukumu, na kuwa hizi thread za kidini zisizo na mantiki zinataka kuwagawa watanzania kwa misingi ya udini, jambo la kipumbavu sana kama alivyowahi kusema mwalimu Nyerere, na sijui kama wanaoandika ni watanzania kweli au ni watu wanaotaka tuingie katika machafuko kama ya Rwanda, Burundi au Nigeria.
Kuna msemo unasema [tafsiri isiyo rasmi] '' Kama hujui jambo ni bora ukae kimya, maana unaweza kusema na kuwatoa watu mashaka waliyokuwa nayo dhidi yako''
Mwisho, mkuu Rutashubanyuma, wewe kama analyst hebu wape ma analyst wenzako hoja hii wakusaidie. Mimi simwangali kiongozi kwa misingi ya dini yake bali uwezo wake. Simwangalii mtu kwa dini yake bali utu wake. Dini zinazoongelewa sijui ni zipi maana mzee Kingunge hana dini, je huyu hapaswi kuwa kiongozi eti kwasabau si mwislam au Mkristo.
Rutashubanyuma, nikuulize kama unajua historia ya nchi yetu, je Mkwawa alikuwa dini gani, je Kinjekitile alikuwa dini gani, Rumanyika na Mirambo walikuwa dini gani. Kama unaamini ukristo na uislam ndiyo dini pekee, nitakuomba urejee tena darasani. Tukiendekeza mambo ya kijinga ipo siku tutawakana ndugu zetu eti ni wapagani. Lakini Pia Rutashabanyuma unapaswa kutueleza, iwapo wizara au idara X ina watu wa dini fulani, je kuna faida gani inapatikana hapo.

Ahsante. Nguruvi3, mchukia thread za udini.
 
Nasema dhana hizo zinazojengwa na Mtanzania ni dhana za hatari kwa mstakabali wa Taifa, ni dhana inayoweza kulisambaratisha Taifa tuendako, Nasema , ni dhana ya hatari, wanajuaje dini ya Mtu ? Jina si dini ya mtu.
wanamtetea JK kwa gharama mbaya ya maisha , ni gharama ya damu.
Rostam na wahariri wake pale Kijiweni wanatuandalia Janga.

Ukitaka kujua kama kunaupendeleo wa Kidini ama laah, fanya Jambo moja, Tafuta ratio ya wasomi wa Kiislamu na wakristo, kisha tafuta ratio yao makazini, lazima utagundua jambo kuwa Tunapendelewa.
unaposema kuna mlingano wa 2 kwa tatu katika post za juu kwa taifa, lazima uzingatie mlingano wa wasomi katika Taifa....!
 
I hate this cheap politics...udini udini udini..na hilo gazeti lifungiwe linaboa sasa...
 
ni kweli ulichosema............
KIKWETE,BILAL,KINANA,RIZIWANI,SALMA KIKWETE, SHEIN,NI WAKRISTO....HONGERA MWANDISHI KWA KUWA MPOFU


Makamba, Januari, Shimbo, Mwinyi(waziri wa ulinzi)...........................
 
Hivi haliko online?

yaani ukiliona ni pathetic....hakuna mtanzania mwenye kutaka kujua hayo kwa sasa hivi....na ningekuwa na uwezo ningelifungia mbali kwa sababu wanataka kupandikiza hisia za udini miongoni mwetu....sasa hivi focus ni kwenye uchaguzi basi!

Shame on you Mtanzania
 
Hiki kitu kilicho anza kuhubiriwa kwa nguvu mwaka huu na jk,kina impact kubwa sana katika miaka ijayo. maana hata ambao tulikua hatuangalii mambo kwa misingi ya udini, ametufanya tuanze kungalia kila aliye katika nafasi flani ndani ya serikali yake ni mtu wa dini gani.

Anaweza kupata kura za huruma kwa kulalamikia udini ila sumu wanayo ipanda kwa kuhubiri udini itawadhuru watoto na wajukuu zao
 
Hivi ile hotuba ya MWL JKN ya kukemea mambo ya udini na ukabila imefichwa wapi siku hizi. Kwa mujibu wa nyenyere si ajabu kesho Mtazania likaandika: Serikali ya JK si ya Kibabila kwa vile kuna wachaga wengi kwenye taasisi za umma... na kama muda ungetosha kesho kutwa: Serikali ya JK si ya kibaguzi ina wapemba kibao....Tuwe macho na hawa watu. Hivi naweza kuwasilisha hisia zangu kwa Waziri wa Habari Michezo na Utamaduni kutaka ufafanuzi?
 
Udini mimi naupima kwa wizara ambazo zipo strategic kama Utumishi, elimu, fedha na miundombinu! Pia balozi maarufu duniani kama UK, South Africa na Marekani. Ukinipa data za hizi post nitaweza kuevaluate Jk
 
Ni JK na CCM yake waliowahadaa waislam kuhusu mahakama ya kadhi kwa kuwaahidi mahakama ya kadhi katika ilani yao ya uchafuzi mwaka 2005!!!! Hilo unalizungumziaje mkuu??? .... Wala Mkapa hahusiki na hili la mahakama ya kadhi hata kidogo!!!! Mwaka 2005 baada ya JK kupitishwa na NEC CCM, JK na mtandao wake(Lowasa, Rostam, etc.) walijipa madaraka na kiburi kikubwa cha maamuzi, kiasi kwamba hata Mkapa hakua na nguvu tena ya kuzuia hasa ukizingatia yeye alikua outgoing President, hakutaka malumbano baada ya kuondoka madarakani...... Kuhusu Malecela kilichomgharimu hasa dhidi ya Nyerere siyo mahakama ya kadhi ila ni kudai serikali tatu(hata Jenerali ulimwengu yupo katika kashfa hii)
Mara zote mimi nimekuwa napiga vita hisia za udini zinazoendelea kujengeka Tanzania. Kwa nyakati tofouti kama leo nalazimika kuandika kile nisichokipenda kukijadili, lakini kwa faida yetu sote ni lazima tuwe wakweli na weledi.
Ndugu Rutashubanyuma, kauli mbiu yako ni kuwa wewe ni public policy analyst, na ninaanza kuingiwa na shaka juu ya hili hata kama ni kweli.
Kama wewe ni Mtanzania, basi utakuwa hujaipitia vema historia ya nchi yako. Nukta yako ya tatu inanitia wasi wasi kama kweli una nia njema na nchi hii ya Tanzania unayoishi.
Kwanza naomba urejee miaka 23 ya Mwalimu Nyerere uwiano ulikuwaje ili ujenge hoja ya uwiano wa sasa.
Pili, viongozi hawachaguliwi ili kuongoza dini, wao ni public servants, sijui unataka kutuaminisha nini juu ya uteuzi wa viongozi.
Tatu, mbona hujaangalia huko nyuma Nyerere,Mwinyi,Mkapa uteuzi ulikuwaje ili utupe ulinganifu na huu wa sasa.
Nne, Suala la kadhi limeanza kitambo lakini ni wakati wa mkapa ndipo liliposhika kasi, sijui kama unajua aliyeibua hoja ya kadhi na kuifanya agenda ya uchaguzi Ni A.L.Mrema akimtumia sheikh mtopea.!!!
Tano, Mkapa alifanya nini kama kiongozi wa Chama kuzuia hoja ya Kadhi isiingizwe ndani ya ilani 2005. Iweje suala lililopata baraka za chama leo liwe la JK peke yake. Je nani aliandaa ilani ya ccm 2005, na kwanini halmashauri kuu na CC ziliafiki suala la kadhi.
Sita, Suala la OIC lilianza miaka ya akina Mwinyi na Malecela, na kama unakumbuka hili ni miongoni mwa mambo yaliyozaa G55 na hatimaye Mzee Malecela kuwekwa pembeni katiak u-PM. Suala hili liliendelea wakati wa Mkapa, je yeye alilishughulikiaje? na kwanini leo ionekane ni agenda ya JK ili hali viongozi wawili [miaka kumi kumi] hawakulishughulikia!

Napenda kuweka wazi kuwa sijengi hoja kujibu au kufanunua hoja za Gazeti la Tanzania au JK, ninachokifanya hapa ni kutaka kuwafahamisha wana forum wenzangu kuwa ni vema mtu akatuliza akili kabla hajaandika na kuhukumu, na kuwa hizi thread za kidini zisizo na mantiki zinataka kuwagawa watanzania kwa misingi ya udini, jambo la kipumbavu sana kama alivyowahi kusema mwalimu Nyerere, na sijui kama wanaoandika ni watanzania kweli au ni watu wanaotaka tuingie katika machafuko kama ya Rwanda, Burundi au Nigeria.
Kuna msemo unasema [tafsiri isiyo rasmi] '' Kama hujui jambo ni bora ukae kimya, maana unaweza kusema na kuwatoa watu mashaka waliyokuwa nayo dhidi yako''
Mwisho, mkuu Rutashubanyuma, wewe kama analyst hebu wape ma analyst wenzako hoja hii wakusaidie. Mimi simwangali kiongozi kwa misingi ya dini yake bali uwezo wake. Simwangalii mtu kwa dini yake bali utu wake. Dini zinazoongelewa sijui ni zipi maana mzee Kingunge hana dini, je huyu hapaswi kuwa kiongozi eti kwasabau si mwislam au Mkristo.
Rutashubanyuma, nikuulize kama unajua historia ya nchi yetu, je Mkwawa alikuwa dini gani, je Kinjekitile alikuwa dini gani, Rumanyika na Mirambo walikuwa dini gani. Kama unaamini ukristo na uislam ndiyo dini pekee, nitakuomba urejee tena darasani. Tukiendekeza mambo ya kijinga ipo siku tutawakana ndugu zetu eti ni wapagani. Lakini Pia Rutashabanyuma unapaswa kutueleza, iwapo wizara au idara X ina watu wa dini fulani, je kuna faida gani inapatikana hapo.

Ahsante. Nguruvi3, mchukia thread za udini.
 
Tunachokitaka hapa si dini ya mtu, kabila wala rangi yake! Tunamtaka kiongozi mwenye nia ya dhati ya kuwakomboa watanzania kutoka mikononi mwa mafisadi wachache na si vinginevyo. Kama serikali ya Kikwete imepandikiza udini mpaka jamii ikahisi hivyo, si jambo la kujadiliwa hapa, dahambi hii tuikatee hailitakii taifa letu mstakabali mzuri na sidhani kama kiongozi mwenye akili timamu na fikira hai atadhubutu kujenga uongozi wa namna hiyo. Watanzania wote tu ndugu bila kujali imani na tofauti ya dini zetu. Unapoongelea masuala yanayohusu imani ya mtu inabidi uwe makini sana! Tanzania haijajengwa katika misingi hiyo, kama serikali ya Kikwete imefanya hivyo, basi lidhibitiwe na lisitokee tena. Watanzania wote tunasumbuliwa na adui mkubwa tu asiyekuwa na dini wala kabila -UFISADI Watanzania hatuna dini wala kabila kama adui huyu ila Mtanzania mmojammoja ana dini yake na kabila lake lakini si vya Watanzania. Kwa mantiki hiyo tunapoingia vitani kupigana na adui mkubwa kama huyo inabidi tulielewe hilo.UFISADI ni sawa na ukimwi unaumiza kila mmoja wetu bila kujali imani ya dini yako wala kabila. Mkisema Kikwete amefanya hivyo mtakuwa mnakosea, watanzania wote matatizo yetu ni sababu ya uongozi mbaya na serikali corrupt! Si dini zetu! Hivi kiongozi akifisadi nchi huwa anagawa hela kwenye nyumba za kuabudia au misikitini? Jibu ni hapana. Wahumini wa dini zetu wameshiriki kuifisadi nchi lakini dini zao hazikuifisadi nchi na hili liko wazi kabisa.

Mwisho ni kuchagua kiongozi mwenye hekima na busara wa kufutilia mbali ufisadi na suara la udini litakuwa limeisha kabisa. Tusijidangenye eti kiongozi akiwa mkristo, wakristu wote mtaenda na maaskofu wenu ikulu mlipwe posho wala waislamu wote waende ikulu eti kwa kuwa rais ni mwislamu ili mlipwe posho bila kufanya kazi! Jitume kufanya kazi kwa biddi, uadilifu na umakini na kama kiongozi wako akiwa mwadilifu,makini na mchapakazi hatutaongelea udini, tutaongelea ufanisi. Kinachoongelewa sasa naona ni matokeo ya kukosa, uadilifu, uchapakazi na uwajibikaji na si udini.

FIGHT FOR CORRUP GOVERNMENT AND POOR LEADERSHIP AND NOT RELIGIOUS BELIEVES! WE ARE ALL TANZANIA AND THAT'S THE ONLY ENEMY WE HAVE IN THIS COUNTRY!
 
Kaka kwangu mimi hata kama wangekua waislamiu tupu au wakristo tupu katika idara nyeti za serikali, issue ni je wana sifa zinazotakiwa!!!
Nasema dhana hizo zinazojengwa na Mtanzania ni dhana za hatari kwa mstakabali wa Taifa, ni dhana inayoweza kulisambaratisha Taifa tuendako, Nasema , ni dhana ya hatari, wanajuaje dini ya Mtu ? Jina si dini ya mtu.
wanamtetea JK kwa gharama mbaya ya maisha , ni gharama ya damu.
Rostam na wahariri wake pale Kijiweni wanatuandalia Janga.

Ukitaka kujua kama kunaupendeleo wa Kidini ama laah, fanya Jambo moja, Tafuta ratio ya wasomi wa Kiislamu na wakristo, kisha tafuta ratio yao makazini, lazima utagundua jambo kuwa Tunapendelewa.
unaposema kuna mlingano wa 2 kwa tatu katika post za juu kwa taifa, lazima uzingatie mlingano wa wasomi katika Taifa....!
 
Nne, Suala la kadhi limeanza kitambo lakini ni wakati wa mkapa ndipo liliposhika kasi, sijui kama unajua aliyeibua hoja ya kadhi na kuifanya agenda ya uchaguzi Ni A.L.Mrema akimtumia sheikh mtopea.!!!.


Ahhahah, bora umejisema mwenyewe leo kuwa CCM NI WADANDIAJI WA SERA, so walipoona Mrema anachukua KURA za waislam wao bila KUPAMBANU KWA KUWA NI WAZEE WA KUKURUPUKA wakachukua SERA za MREMA wakapachika kwao sasa WAISLAM WANADAI CHAO HAWANA MAJIBU WANA JIUMAUMA.

Poleni sana WADANDIAJI.
 
Siku zote uroho/tamaa ya kubaki madarakani kwa chama/serikali tawala uletelea kutoa sababu nyingi za kushawishi wananchi wao wasichague viongozi kutoka vyama vya upinzani. Baadhi ya sababu hizo pamoja na kuzungumzia udini na amani.

Kwa sasa TZ ni mfano hai kabisa, JK kwa bahati mbaya kwake na nzuri kwa upinzani ni kuwa hana tena cha kuwaambia WaTZ ili wamchague. Fursa alionayo na ambayo anaitumia kwa sasa ni kueneza tuhuma za udini kuwa kuna vyama vya udini na vinavyoshabikia udini ili kuwatisha wananchi.

Zaidi ya hapo anatumia kauli ya amani. Kuwa watanzania tukitaka amani tuchague chama tawala. kauli hizi kwanza zina maana kuwa kuna baadhi ya watu ambao wao wanahisi kuwa ni watanzania zaidi ya wengine. Ndio maana utasikia kauli kuwa vyama vya upinzani kuwa ni vya msimu tu.

Kwa busara ya kawaida kabisa JK/Chama chake wangekuwa zaidi wanazungumzia sera za CCM na sio amani udini etc. Wa-tz tunajivunia umoja na utuilivu ambavyo kwa bahati mbaya CCM wanataka tuamini kuwa vimeletwa na CCM. Wa-tz hatuna shida kabisa au wasiwasi na swala Udini au amani.

Nasema ni kushindwa uongozi kwa sababu tusingefika huku kama serikali ya JK ingekuwa makini ktk maswala ya mahakama ya kadhi ya swala la OIC. Hivi vitu viwili havikupashwa kuingia ktk agenda za CCM kwa namna yeyote ile. Hapa ni kushindwa uongozi tu na tamaa ya kubaki madarakani.
 
Maeneo yenye wakristo wengi SLAA na CHADEMA alipewa kura nyingi zaidi ya JK na maeneo ya Waislam wengi JK aliata kura nyingi sehemu zingine kama Bukoba vijijini ndio walikoamua kumnyima kabisa JK kura. Sasa mambo ya kudanganyana eti ohhh viongozi wa kidini wapige vita udini naona imekuwa kama kutwanga maji kwenye kinu.

Hamuamini tazameni matokeo ya uchaguzi huuu KILAKALA Morogoro na maeneo hata ya Dar yalivyojigawa kutokana na dini za watu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom