Buenos Aires
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 1,894
- 1,622
Ila wa Ethiopia wabishi kinoma wamejenga Bwawa na wamehanza kuingiza maji , muda si muda itazuka Vita kati Wamisri Na Ethiopia
Cha kulaumu zaidi ni yule aliyetunyima akili, ni sawa na swala au pundamilia waanze kujilaumu huko porini kwa nini wanaliwa na Simba. That's nature my dear, lazima viumbe tutegemeane. Ulishawahi kujiuliza hivi hao wazungu kwa mfano waamue kuacha kuchukua dhahabu huku Afrika au madini mengine ambayo unasema yana thamani, utayafanyia nini? Hiyo thamani unayoiona wewe kwenye madini imesababishwa na hao wazungu la sivyo sisi tungekuwa tunayaona kama mawe tu.Sasa nimeanza kuamini Maudhui ( Content ) ya Kitabu alichoandika Rais Yoweri Museveni wa Uganda mwaka 1992 ambacho Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliandika Dibaji ( Fowerword ) yake chenye Title ya ' What is Africa's Problem ' ambapo Rais Museveni aliwalaumu mno Mababu zetu kwa Kuzubaa, Kutojitambua na Kuwaachia Wazungu wawatawale na kuwazidi Akili kiasi kwamba hadi sasa Waafrika tupo tupo tu kama Watu Wendawazimu na tuliolaanika wakati Utajiri Wetu mkubwa ndiyo unazitajirisha nchi za Wazungu hawa hawa.
Ahahaha na kweli hao ni maswahiba barabara kimaslahi misri yupo tayari kufinga mipaka yote wakimbizi wa kiarabu wasiingie lakini sio kuwaudhi israelEthiopia anachokifanya hakimake sense kabsa. Akidundwa asije kulalamika na kulialia mbele ya swaiba wake muisraeli.
Hivi kwa mfano mtu ukaenda pale daraja la jinja uganda na kumwaga vifusi vya zege mto nile utaendelea kuwepo!?
Nadhani mwenyezi mungu alituumba waafrica hivi tulivyo kwa makusudi yake mwenyewe.hatuna elimu,teknologia, uchumi bora nk lakini ndo tunaishi maisha magumu in a very simple way.
Kama wakina Bgate walisema afrika tutaokotwa mitaani maiti kama kuku walio kufa na fowl typhoid kwa corona na leo hii tuna sumbuliwa na corona lakini hatufi kama wao. Na maisha yanaenda .
Vita ya aina hiyo ikizuka Kenya, Uganda, Tanzania, Sudan tusimame na Ethiopia.
Maana wanachotaka kuleta Misri ni upuuzi
Ni wapi nimetaja waarabu au wafrika?Huu sasa ni ubaguzi kisa wale ni waarabu, lakini umesahau hao pia ni waafrika.
Ili mambo yatuendee sawia tuachaneni na roho mbaya, chuki, na tusaidiane na tushirikiane kwa pamoja. Huu ndio ubinadamu na sio uhasama
Acha mambo yako kariakoo ya wapi!!!?? Lini watu walidondokaAisee! Unakumbuka kariakoo watu wanadondoka mpaka kufa, umesahau eti! Sema hivi wanaokufa hapa hatujui idadi yake kwa sababu takwimu hazitolewi. Nakushauri nenda kwenye hospitali kubwa hasa za serikali ukajionee wagonjwa wa corona walivyo wengi utashika kichwa kiongozi, acha kusikiliza maneno ya mtaani kwenye vijiwe vya kahawa na mitandaoni, nenda mwenyewe kajihakikishie utarudi kunishukuru.
Nikija kua Rais wa hii nchi naapa
Hao waarabu Koko wataisoma namba kwanza nitawashawishi watu wa Uganda huo mto tuupindishe Kwa kuupiga livasi kunyumenyume utiririke kwenda Burigi chato
Hao wavamizi walijimilikisha mapiramid ya Babu zangu farao Imhotep, Tut,khofu na wengineo
Wangeisoma namba!
Ndio watajua na roho mbaya zaidi ya Jiwe!
Mikataba iliyosainiwa na wakoloni inaendelea kutafuna mpaka sasa,hao wamisri Wana haki miliki ya maji yaliyomo ziwa Viktoria pia.kutahitajika viongozi shupavu kutangua mikataba hiyo.Huwa najiuliza nani aliwamilikisha Masri hiyo 87% nakosa jibu. Labda wajuzi wa history watatujuza.
usichukulie serious mkuu,nachangamsha genge tu mkuu kwanza huo utakua ukatili Kwa binadamu wenzangu unaanzaje kuzuia maji Kwa watu wa jangwani wakati sisi tuna Kila Aina ya chanzo?Maisha hayendi unavyotaka wewe bosi, hata ukiwa raisi hutoweza kufanya hilo.
Hivi ikitokea vita Kati ya Misri Vs Ethiopia,Kenya, Uganda, Tanzania Na Sudan. Nani atashinda?Vita ya aina hiyo ikizuka Kenya, Uganda, Tanzania, Sudan tusimame na Ethiopia.
Maana wanachotaka kuleta Misri ni upuuzi
Hlf yeye Museven amefanya nini sio kwa Ajiri ya Afrika kwa Ajiri Uganda tu...Sasa nimeanza kuamini Maudhui ( Content ) ya Kitabu alichoandika Rais Yoweri Museveni wa Uganda mwaka 1992 ambacho Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliandika Dibaji ( Fowerword ) yake chenye Title ya ' What is Africa's Problem ' ambapo Rais Museveni aliwalaumu mno Mababu zetu kwa Kuzubaa, Kutojitambua na Kuwaachia Wazungu wawatawale na kuwazidi Akili kiasi kwamba hadi sasa Waafrika tupo tupo tu kama Watu Wendawazimu na tuliolaanika wakati Utajiri Wetu mkubwa ndiyo unazitajirisha nchi za Wazungu hawa hawa.
Makao makuu ya AU yamejengwa na mchinaNilipoona tu tamko la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likisema kuwa haliwezi Kuingilia kati Mgogoro wa Matumizi ya Maji ya Mto Nile kati ya nchi za Misri na Ethiopia kwakuwa inajua kuwa Misri ina uhalali wa 87% ya Maji ya Mto huo nimeshtuka na kuwa na maswali mengi mno.
Hivi ni lini Waafrika na hasa huu Umoja wa Afrika (AU) utasimama imara kabisa Kutetea na Kusimamia Maslahi ya Bara la Afrika na Rasilimali zake kwa ujumla? Kwanini iliyokuwa (OAU) miaka ya nyuma ilishindwa kuwa Sauti ya Kujiamini kwa nchi zote za Afrika ili Afrika tusikike, tueleweke na tuheshimike mno.
Hainiingii Akilini kabisa leo hii kusikia nchi kama za Misri na Ethiopia kila Uchao tu zinagombania Umiliki wa Mto Nile wakati sehemu Kubwa na iliyoanzia hadi hata kupita nchi kama za Uganda na Sudan nazo zina haki ya Umiliki lakini zimenyamaza na zikiwaangalia kama hata si Kuwashangaa pia.
Wazungu wanapenda sana Kutuingilia na Kutupangia mambo yetu mengi Waafrika na kwa jinsi Viongozi wengi wa Bara la Afrika walivyo Goi Goi na wa hovyo hovyo kiasi cha Kuwaogopa Wazungu hawa Waafrika wote tunadharaulika na kuonekana hakuna tunalolijua na hata kuliweza zaidi ya kuwa Waongo, Wavivu na Wachawi wa Kutukuka.
Acha mambo yako kariakoo ya wapi!!!?? Lini watu walidondoka
Hivi ikitokea vita Kati ya Misri Vs Ethiopia,Kenya, Uganda, Tanzania Na Sudan. Nani atashinda?
Maji mengi ya Mto Nile yanatoka Ethiopia kwenye mto unaitwa Blue Nile amabao chanzo chake ni lake Tana iliyopo Ethiopia. Ziwa Victoria na tributaries zake zinatoa 20%Hivi kwa mfano mtu ukaenda pale daraja la jinja uganda na kumwaga vifusi vya zege mto nile utaendelea kuwepo!?
Wa misri asilia sio warabu. Warabu ni wahamiaji na wagiriki ispkuwa warabu nfio watawala pale misri ila ni waafrika kweli hata damu tu nashare jwa asilimia fulani ila haki izingatiwe bila kujali rangi dini wala kabila.Huu sasa ni ubaguzi kisa wale ni waarabu, lakini umesahau hao pia ni waafrika.
Ili mambo yatuendee sawia tuachaneni na roho mbaya, chuki, na tusaidiane na tushirikiane kwa pamoja. Huu ndio ubinadamu na sio uhasama