Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Binadamu tumeweka siasa Mbele maisha ya watu na utu wao nyuma. Katika kipindi chote ambacho matendo maovu ya Jeshi la Polisi yanafanyika hakuna aliyewahi kusikia Chama cha Mapinduzi wakikemea.
Tumesikia namna mwanachama wa CCM Bwana Sabaya alivyokuwa anakamata walinz wake nakuwapiga Kisha kuwaweka mahabusu, alivyotesa wananchi na wafanyabiashara Lakini hata siku Moja CCM haijawahi kumkemea.
Leo CCM inasema Polisi wajitathimini. Anayetoa tamko alikuwa DC Arusha akitokea U CCM Iringa, ambapo amewahi kutamka adharani Kwamba flan anapaswa kupotezwa; Leo anasema Polisi wajitathimini.
Uongozi wote uliopo Sasa Ndani ya chama ulikuwepo awamu ya Tano na Polisi walikuwa wanafanya KAZI Kwa kusifiwa sana , watu waleqale waliowasifia Polisi Leo Kwa sababu tu wanataka kumtoa IGP wamweke mtu mwingine wanakuja kumwambia IGP ajitathimini. Wakati anawasiadia kwanini hoja ya kujitathimini haikuwepo?
IGP ana mapungufu yake kama binadamu, ila makosa yaliyofanywa na Jeshi la Polisi IGP apaswi kubebeshwa lawama, lawama zinapaswa kwenda Kwa chama Cha Mapinduzi kinacholielekeza Jeshi la Polisi nini Cha kufanya Kila wakati.
Natambua hivi karibuni utafanyika UTEUZI wa viongozi wapya wa Jeshi la Polisi ikiwemo kuwapandisha vyeo baadhi ya maafisa kulingana na gap linalopigiwa makalele na wanaharakati mitandaoni ila niambiene Kati ya RPCs au wakuu wa vikosi waliopo Polisi Leo Nani msafi kuliko Siro? Je, hao viongozi wamejichafua au mfumo imewafanya wachafuke?
Siro anaweza akakaa benchi kama mlivyopanga ila ninyi pia mnaopanga Siro atoke tambueni anayeingia Hana usafi Kwa sababu mfumo wa chama Cha Mapinduzi ndio unaopanga wananchi wahudumiwe kikatili au wahudumiwe Kwa staha.
Siro kung'atuka siyo suluhu Kwa sababu Kila anayetaka kuishi Ndani ya Jeshi la Polisi atawajibika kumsikiliza Kila mjumbe wa chama cha Mapinduzi.
Jeshi la Polisi imara linategemea katiba inayoweka separation of power. Leo wanasiasa wamekwenda hata kupangua na kupanga Jeshi kubwa Jambo linalotishia ustawi na mipango ya vyombo hivi. CCM jitathiminini upya hasa mnapoingilia vyombo vya Ulinzi kuepusha kuwavunja Moyo askari wetu Kwa kile mnachoita hakuna aliyejuu ya chama Cha Mapinduzi.
Tumesikia namna mwanachama wa CCM Bwana Sabaya alivyokuwa anakamata walinz wake nakuwapiga Kisha kuwaweka mahabusu, alivyotesa wananchi na wafanyabiashara Lakini hata siku Moja CCM haijawahi kumkemea.
Leo CCM inasema Polisi wajitathimini. Anayetoa tamko alikuwa DC Arusha akitokea U CCM Iringa, ambapo amewahi kutamka adharani Kwamba flan anapaswa kupotezwa; Leo anasema Polisi wajitathimini.
Uongozi wote uliopo Sasa Ndani ya chama ulikuwepo awamu ya Tano na Polisi walikuwa wanafanya KAZI Kwa kusifiwa sana , watu waleqale waliowasifia Polisi Leo Kwa sababu tu wanataka kumtoa IGP wamweke mtu mwingine wanakuja kumwambia IGP ajitathimini. Wakati anawasiadia kwanini hoja ya kujitathimini haikuwepo?
IGP ana mapungufu yake kama binadamu, ila makosa yaliyofanywa na Jeshi la Polisi IGP apaswi kubebeshwa lawama, lawama zinapaswa kwenda Kwa chama Cha Mapinduzi kinacholielekeza Jeshi la Polisi nini Cha kufanya Kila wakati.
Natambua hivi karibuni utafanyika UTEUZI wa viongozi wapya wa Jeshi la Polisi ikiwemo kuwapandisha vyeo baadhi ya maafisa kulingana na gap linalopigiwa makalele na wanaharakati mitandaoni ila niambiene Kati ya RPCs au wakuu wa vikosi waliopo Polisi Leo Nani msafi kuliko Siro? Je, hao viongozi wamejichafua au mfumo imewafanya wachafuke?
Siro anaweza akakaa benchi kama mlivyopanga ila ninyi pia mnaopanga Siro atoke tambueni anayeingia Hana usafi Kwa sababu mfumo wa chama Cha Mapinduzi ndio unaopanga wananchi wahudumiwe kikatili au wahudumiwe Kwa staha.
Siro kung'atuka siyo suluhu Kwa sababu Kila anayetaka kuishi Ndani ya Jeshi la Polisi atawajibika kumsikiliza Kila mjumbe wa chama cha Mapinduzi.
Jeshi la Polisi imara linategemea katiba inayoweka separation of power. Leo wanasiasa wamekwenda hata kupangua na kupanga Jeshi kubwa Jambo linalotishia ustawi na mipango ya vyombo hivi. CCM jitathiminini upya hasa mnapoingilia vyombo vya Ulinzi kuepusha kuwavunja Moyo askari wetu Kwa kile mnachoita hakuna aliyejuu ya chama Cha Mapinduzi.