Ni nini kauli ya Serikali ya Tanzania/ IGP Dodoma kuhusu kifo cha Nasra mwanafunzi wa UDOM?

Marehemu alisafiri lini kwenda Moshi?
Nchi yetu ina mazonge mengi
 
Sina hakika kama ndio huo ila kuna mmoja uliliwa kichwa mapema kabisa
JAMII FORUM IMEGEUKA TOILET PAPER [emoji3474][emoji406] YA WAHUNI ...HATA UKICHEKI BAN WANAZOPIGWA WATU SIKU HIZI NI ZAKISIASA NA KIFISADI ..KWA SASA UWEZI KUKUTA HABARI NYETI YOYOTE HAPA JF ZOTE ZINAPIGWA PIN KABLA YA KUTUFIKIA ...SERIKALI YA SAMIA INAMAMBO MAOVU MAKUBWA SANA WATU WAKILETA HUMU YANA PIGWA PIN [emoji419] SASA HIVI NI WAKATI WA KURUDI KULE KENYA TALK FORUM.... MAANA HAPA JF NAONA KABISA BWANA MERO... ULE MSEMO WA MASIKINI AKIPATA MATAKO ULIA PWATA UNA MUHUSU
 
Ohooo ! Hivyo tena ???!
 
Ndugu Lwiva naomba niwe na mtazamo tofauti kidogo hapa kwenye hili la kuilaumu JF (kwa maana ya wamiliki na wafanyakazi)
Mimi binafsi naona wanapambana sana na kwakweli wanajitahidi mno kuuwezesha huu mtandao kubaki hai hata wa leo
Kuna changamoto kubwa sana zisizosemwa popote wala kuwekwa hadharani wanazopitia kutokana tu na maudhui ya wanachama wake kwakuwa wao ndio wa kwanza kuulizwa

Sisi tunatumia utambulisho bandia hapa upenuni lakini uhalisia wetu wetu wote wanao wao na ndio walinzi wetu wanaotulinda.. Kuna nyakati walikuwa tayari kuumizwa na kuteswa lli tu kutulinda sisi wanachama wake

Hiki kitu kinaitwa SERIKALI kioneni hivihivi, tutanietanie tu hapa lakini kuna mipaka yake.. Serikali ina mikono mirefu sana na nguvu nyingi sana

Kuna baadhi ya maudhui yanaondolewa kwa faida yetu wenyewe, afya ya forum na ulinzi wa wamiliki na wafanyakazi wake.. Mimi na wewe inaweza kuchukua muda kufikiwa na ile mikono mirefu lakini sio wao wamiliki na wafanyakazi.. Wao kudakwa ni dakika tuu

Inawezekana kweli kuna mahali kuna mapungufu lakini sisi sote si wakamilifu.. Ni vema tuwatie moyo na ikibidi tuwashukuru na kuwapongeza maana wanayopitia pengine ni makubwa kuliko tunavyolaumu

Mungu ibariki JF
 
Mwili wa Nasra upo mkoa gani tunavyoongea sasa hivi?

Mama Samia anaitwa mama ameshindwa kujua kilichompata binti Nasra ambaya ni sawa na binti yake?

RPC Dodoma naye amepiga kimyaaaa?

Dr mpango naye alikwenda kumjulia Hali Naibu Waziri akalishwa matango pori. Nchi ngumu hii kwa Kweli.

Sasa nchi inaongozwa na mama mabinti wanaliwa vichwa na watu wasiojulikana??
 
Nafahamu jambo moja kuhusu Mh. Rais wetu, Mama ni mtu mwenye hofu ya Mungu na pia ni mpole na mwenye busara

Busara ya Mama itampeleka kwenye uvumilivu ili kuepuka kumuumiza mtu, atasubiri kidogo muda upite ili mwenye majeraha apone.

Hofu ya Mungu itamfanya achukue maamuzi ili kutenda haki na kufanya watu waendelee kuiamini serikali yake.

Mwenye ufahamu amenielewa
Tuwe na subra.
 
Nadhani Mpango akienda kumjulia hali dereva wa Ofisi yake ikawa hamna namna!
 
Ina maana kuna jambo hapa kati ya hiyo ajali ya Waziri na huyo mwanafunzi...
 
Maswali mazuri hayo.

Serikali na Polisi watuambie; Je! Tusubiri majibu au tuyatafute wenyewe?
 
Kwaio Naibu waziri akiondolewa waziri ndo Nasra atarudi.Ebu Tuache ujinga kama alikua mchepuko hawa wote wanamakosa kwaio atakaepaswa kutoa adhabu dhidi yao ni mwenyezi Mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…