Stan Mashamba
JF-Expert Member
- Apr 22, 2020
- 3,183
- 2,479
Kwa kanuni hizi za uchaguzi na tume hii; mpinzani yeyote haoni mbali. That is why Bia Yetu & Co. are celebrating.Kisheria bdo lissu ana sifa za kugombea urais.Lissu akigombea magu ajipange...
Daaah . . . . naona watanzania tumemiss amsha amsha. Anyway, uchaguzi utakuwa wa kipekee kutokana na utani na vijembe na hoja zitakazokuwepoKwa kweli maswali ni mengi sana. Lakini all in all, Tundu A. M. Lissu akiwa mgombea wa CHADEMA/UKAWA kupambana na mtesi wake, kwa hakika, uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 kuanzia kampeni utakuwa wa kipekee sana na tutashuhudia msisimuko na amsha amsha ya kisiasa kali maradufu kuliko ilivyokuwa ktk uchaguzi uliopita wa 2015 nyakati za kina Edward Ngoyai Lowassa...
Tujadili....
Ni kweli. Halafu hizi kanuni wengi wetu hatuzijui. Na hapo ndipo shughuli itaanzia kuwa pevuKwa kanuni hizi za uchaguzi na tume hii; mpinzani yeyote haoni mbali. That is why Bia Yetu & Co. are celebrating.
"....he survived death in order to tell the tale....."
Kwa akili zako unadhani for the name of SYMPATHY pekee ni kigezo tosha chankumsimamisha mtu Kama mgombea wa nafasi nyeti kama Urais?
Mwanaharakati hawezi kuwa Rais wa nchi Mkuu, nchi inahitaki Kiongozi na dola inahitaji Mtawala.
Madhara ya wanaharakati ni pamoja na kutuletea Ndoa za Jinsia moja, kukubali zile Sheria zote ambazo ni universal mfano, watoto kutokuadhibiwa, wanafunzi kujifungua na kurudi mashuleni, utoaji mimba kuwa haki ya kisheria, nk
Kumbuka Sheria hizo inawezekana sio mbaya kwa jamii za waasisi wa Sheria hizo kwakua wamefanya tafiti zankutosha na kujiridhisha na madhara ambayo yatajitokeza.
Ila kwa kuabsisi tutalazimishwa kusaini kwa ajili ya kuonekana tuko pamoja na Jumuia za kimataifa na kupata misaada madhara yatakua na athari kubwa kihisia na kijamii.
Sifa za mtu kugombea nafasi ya urais zipo na zinajulikana.
Haya mapya unayoyaeleza, na kwa kiaina kama kuwastua wasiopenda Lissu agombee yatazuliwa kama sababu na kulazimisha iwe hivyo watu watake au wasitake.
Hili linajulikana kwa wote.
Kwa hiyo, kwa kifupi kujibu uliyoyaandika; ni kazi ya CHADEMA na wengine wote wanaokataa maovu ya kila aina ya hawa watu, kujizatiti kukataa mbinu za kila namna watakazotumia CCM katika kuvuruga uchaguzi kwa sababu yoyote ile, ikiwa ni pamoja na hii ya kumwekea mizengwe mgombea wa CHADEMA, kama atakuwa ni Tundu Lissu.
Kwa kanuni hizi za uchaguzi na tume hii; mpinzani yeyote haoni mbali. That is why Bia Yetu & Co. are celebrating.
Tungu akifika hapa tu pingu amelisaliti taifa na kulichafua piaUkiniuliza swali hili; Je, ungependa Tundu A. M. Lissu awe mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA/UKAWA katika uchaguzi mkuu wa 2020?
Hakika jibu langu haraka haraka na pasipo kupepesa macho huku nikitabasamu, ningekujibu tu....YES, HUYU NDIYE...!!
Huyu ndiye si kwa sababu kina Zitto Z.R. Kabwe ama wengine wowote wale hawafai ama hawatoshi...
Ni kwa vile tu ukiwaweka katika mizania, Tundu Lissu anawazidi kwa kiwango kikubwa sana wenzake na ni kwa sababu;
".......he survived death in order to tell the tale...."
Nina hakika hata wengi wa wapenda mabadiliko nje ya CCM wanaweza kukubaliana kuwa, Tundu A. M. Lissu ndiye mgombea sahihi na mwenye uwezo kisiasa (ingalau kwa sasa) wa kukabiliana na CCM ikiyokufa chini ya mgombea wao (hopefully, Magufuli)...
Lakini changamoto pekee anayokabiliwa nayo ndugu Tundu A. M. Lissu ni ya kisheria....
Na huu ndiyo msingi wa mjadala katika mada hii ya leo na tunaomba wataalamu wa katiba na sheria waliomo nasi ktk jukwaa hili watusaidie kutupa mwanga juu ya aidha INAWEZEKANA ama HAIWEZEKANI kwa ndugu huyu kutumia haki yake ya kiraia ya kupigiwa kura kwa mazingira ya sasa....
Hii ni kwa sababu kila mtu anafahamu kuwa, Tundu A. M. Lissu ana mlolongo wa kesi mahakamani...
Na moja ya kesi ni ile ya uchochezi na mwenzake mwandishi wa gazeti la (Mawio? MwanaHalisi?) ambayo siku chache zilizopita kidogo isababishe wadhamini wake kutaka kufungwa na mahakama na baadaye kuwaamuru wamlete mshitakiwa mahakamani...
Sasa tujaribu kujiuliza maswali kadhaa wa kadhaa ya kutuongoza ktk mjadala wetu;
1. Je, wapinzani wake kisiasa hususani CCM wana nafasi gani kutumia kesi hizi kama mapingamizi kumzuia Tundu A.M. Lissu asigombee Urais?
2. Katiba na Sheria ya uchaguzi inasemaje kuhusu mgombea mwenye kesi ya jinai mahakamani kugombea nafasi ya uongozi hasa ktk ngazi ya Urais?
3. Najua katiba na sheria inam - disqualify mtu ama mgombea yeyote kama alishahukumiwa kifungo cha miezi 6 au zaidi kwa makosa fulani fulani ya jinai au uaminifu kugombea nafasi ya uongozi...
Hebu sasa tujiulize, CCM ndio wanaongoza serikali kwa sasa. Mgombea wao (possibly) anaweza kuwa huyu huyu Bwana Magufuli ambaye ndiye Rais mpaka siku anaapishwa Rais mpya.....!!
Na katika jambo ambalo Magufuli na CCM wasingependa kuliona linatokea, ni ndugu Tundu A.M. Lissu kusimama kama mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA/UKAWA akipambana na Magufuli...!
Unadhani ni mipango gani (kwa kutumia dola: TISS na mahakama) inafanyika ktk viunga vya Lumumba kuhakikisha hili halitokei?
4. Unadhani wataweza kumzuia huyu ndugu huyu na kuzima ndoto ya Tundu Lissu mwenyewe, wananchi wanaomuunga mkono na CHADEMA/UKAWA yenyewe?
5. Je, unadhani CHADEMA wenyewe wanalijua hili? Je, Tundu Lissu mwenyewe anajua hili? Je, unadhani wana mkakati gani thabiti kukabili hujuma hizi na kufanya quick counter attack kuizima?
6. Je, una macho makali na mangavu ktk kutazama mambo kwa kina chake? Kama jibu lako ni ndiyo, sasa eleza kwa hoja thabiti kabisa, kwamba, unaweza kuunganishaje "dots" kwa hiki kinachotokea sasa kwa CHADEMA kushambuliwa kwa namna hii?
Je, unadhani anayetafutwa ni Freeman Mbowe? Au ni jambo kubwa zaidi linatafutwa na Mbowe ni kama "WAY IN" tu kuingia huko na kumaliza shughuli?
Kwa kweli maswali ni mengi sana. Lakini all in all, Tundu A. M. Lissu akiwa mgombea wa CHADEMA/UKAWA kupambana na mtesi wake, kwa hakika, uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2020 kuanzia kampeni utakuwa wa kipekee sana na tutashuhudia msisimuko na amsha amsha ya kisiasa kali maradufu kuliko ilivyokuwa ktk uchaguzi uliopita wa 2015 nyakati za kina Edward Ngoyai Lowassa...
Tujadili....
Anakesi ya uchochezi uchochezi ni jinai hafaiTundu Lissu hana kesi yeyote ya kikatiba wala jinai
Ni vijikesi vya kuokoteza vya kisiasa aje agombee wakimkamata tuandamane mpaka kieleweke.
Tatutaki rais mremavuKisheria bdo lissu ana sifa za kugombea urais.Lissu akigombea magu ajipange...
Aje awe raid hapo kwenuTundu Antiphas Mughwai Lissu Rais wa Tanzania 2020-2025
Tungu akifika hapa tu pingu amelisaliti taifa na kulichafua pia
Hili likitokea,jua litaanza kutoka kusini na kuzama kaskazini.Halafu kuwe na mdahalo wa hao wote kwa pamoja.
Kwa ubongo wako wa kuku huwezi pata mantiki katika tambo zangu.Peleka mitazamo ya siasa za kijamaa mbal we mbuzi jike.
Kuna kitu umezungumzia hapa ambacho wengi hawajui. Hizi harakati zooote na makombora yooote anayopigwa nayo Mbowe, siyo kwamba wanamwona Mbowe ni tishio kubwa. Hofu yao kuu iko kwenye mtu anayeweza kusimamishwa na Chadema kugombea urais. CCM na hasa viongozi wa juu na watu wa kitengo wanajua kabisa kuwa Magufuli sasa hivi hakubaliki na sehemu kubwa ya wananchi (labda ukindoa kanda ya Ziwa na hasa maeneo ya karibu na nyumbani kwake.) Na mbaya zaidi ndani ya CCM yenyewe kuna watu wengi wanaugulia na kulaani chinichini. Hii hali inafanya uchaguzi ujao uwe unpredictable, na hasa kama Chadema itasimamisha mtu kama Lissu. Naomba nisisitize CCM wasiwasi wao hasa uko kwenye ''kinachoweza kutokea'' wakati watakapoiba kura siku ya uchaguzi (wanajua kabisa kuiba ni lazima na wamejipanga, na ndivyo watakavyofanya). Shida iko kwenye ''je wakiiba wananchi hawawezi kukiamsha na ikatokea fujo kubwa kabisa?''. Hapo sasa ndiyo wanamekuja na mkakati wa kuhakikisha Chadema inayumbushwa ili wakati wa uchaguzi isiweze kujipanga. Na ili kuhalalisha mambo imebidi watafutwe vibaraka kama kina Mbatia na Lipumba.Wana "celebrate" hewa...
Wana "celebrate" mimba ambayo ndo tu imetungwa...
Wanasahau kuwa kuna uwezekano mimba ikaharibika ama kukawa na "pre mature delivery" ya mtoto....
Kuiangusha CCM ni wajibu na lazima kwa 100% kwa sheria na kanuni hizohizo za kulazimisha...
Nguvu ya umma (people's power) ikiamua kubadilisha mambo, hakuna cha kuzuia, hakuna linaloshindikana.....!!
Amesaliti nini?Huyo afiwe Ubeleji tu ni msaliti namba 1 Na atajuta aliyoyafanya
Kwa ubongo wako wa kuku huwezi pata mantiki katika tambo zangu.
By the way ahsante kwa kunipa jina jipya.
Kwa akili zako unadhani mleta hoja anatumia only ""....he survived death in order to tell the tale....." kumtambulisha TL kwenye post yake? Mleta hoja anajua kuwa JF ni platform yenye watu wasiohitaji kuelezwa sifa za TL kwa kuwa wanamfahamu. Halafu unataka kutuambia nini kuhusu JPM kutuletea sheria za kuzuia wengine wasifanye siasa isipokuwa yeye tu unapolinganisha na hao unaowaita wanaharakati?"....he survived death in order to tell the tale....."
Kwa akili zako unadhani for the name of SYMPATHY pekee ni kigezo tosha chankumsimamisha mtu Kama mgombea wa nafasi nyeti kama Urais?
Mwanaharakati hawezi kuwa Rais wa nchi Mkuu, nchi inahitaki Kiongozi na dola inahitaji Mtawala.
Madhara ya wanaharakati ni pamoja na kutuletea Ndoa za Jinsia moja, kukubali zile Sheria zote ambazo ni universal mfano, watoto kutokuadhibiwa, wanafunzi kujifungua na kurudi mashuleni, utoaji mimba kuwa haki ya kisheria, nk
Kumbuka Sheria hizo inawezekana sio mbaya kwa jamii za waasisi wa Sheria hizo kwakua wamefanya tafiti zankutosha na kujiridhisha na madhara ambayo yatajitokeza.
Ila kwa kuabsisi tutalazimishwa kusaini kwa ajili ya kuonekana tuko pamoja na Jumuia za kimataifa na kupata misaada madhara yatakua na athari kubwa kihisia na kijamii.