Ni nini tafsiri hasa ya "Kufanya siasa za kistaarabu?"

Ni nini tafsiri hasa ya "Kufanya siasa za kistaarabu?"

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ili watu wote tuwe kwenye ukurasa mmoja wa uelewa bila kujali itikadi zetu za kisiasa, elimu, jinsia na hata makabila na kanda zetu tunakotoka ni lazima neno "kufanya siasa za kistaarabu" lipewe tafsiri yake ili wadau wote wafahamu maana yake ili kama mtu mkifanya siasa zisizokuwa za kistaarabu kila mtu awe shahidi.

Siasa za kistaarabu ni nini na ni zipi?

Je, kufanya siasa zisizo za kistaarabu ni kufanya nini?

Je, ni nani anatakiwa kufanya hizo siasa za kistaarabu?
Je, ni nani atakaesema wewe umefanya siasa zisizo za kistaarabu?
Je, ni nani atawaadhibu wote wanaofanya siasa zisizo za kistaarabu bila kujali ni wa chama gani?

Na je, kusema uongo, kufichua ukweli ambao ulifichwa, kuiba kura, kuengua wagombea, kutumia mali ya umma kwenye siasa za vyama, kuzuia mikutanp ya vyama na maandamano na tumumia maneno ya kuudhi kwenye siasa ni sehemu ya siasa zisizo za kistaarabu pia?

Taifa lazima lisonge mbele na lionekane na wote likisonga mbele.
 
Kwani sheria ya haya unayosema si ipo? Je wale waliokua wanasema... Mpaka tuwape mimba wake zenu, mara rudi na mavi yako nyumban. Na mlikua mnashangilia je wao ni wenye haki? Wengine wakaitwa tumbili huku mkipiga makofi meza za bunge!!
Ndugu zangu ili kuliponya hili taifa siasa za kistaarabu lazima zifafanuliwe ni zipi na zifanywe na watu wote na zionekane zikitendeka, huwezi kusema kuengua wagombea wote wa uchaguzi na kupita bila kupingwa ni kufanya siasa za kistaarabu.

Ile kamati maalumu ya kuratibu malidhiano nchini lazima ije na orodha ndefu ya vitendo vyote ambavyo sio siasa za kistaarabu. Watu wasije wakaja na tafsiri kuwa siasa zisizo za kistaarabu zinafanywa na wapinzani tu.
 
Ndugu zangu ili kuliponya hili taifa siasa za kistaarabu lazima zifafanuliwe ni zipi na zifanywe na watu wote na zionekane zikitendeka, huwezi kusema kuengua wagombea wote wa uchaguzi na kupita bila kupingwa ni kufanya siasa za kistaarabu. Ile kamati maalumu ya kuratibu malidhiano nchini lazima ije na orodha ndefu ya vitendo vyote ambavyo sio siasa za kistaarabu. Watu wasije wakaja na tafsiri kuwa siasa zisizo za kistaarabu zinafanywa na wapinzani tu.
Mkuu nadhan unaelewa ule usemi... Kunya anye kuku akinya bata kahara 🤣🤣🤣
 
Siasa za kisataarabu ni kuacha kutibua asali za watu na kuacha kusema yale mabaya yanayofanywa na viongozi wa ccccmmmmuuu kwa wananchi wao
Tuwe na orodha ndefu ya vitendo ambavyo sio siasa za kisataarabu, tusimwachie mtu mmoja au kundi moja tu kazi ya kutafsiri ipi ni siasa ya kistaarabu ni ipi sio. tusimuachie Msajili wa vyama vya siasa au jeshi la polisi au usalama wa taifa au chama cha siasa wawe na tafsiri yao juu ya siasa za kistaarabu..
 
Ili watu wote tuwe kwenye ukurasa mmoja wa uelewa bila kujali itikadi zetu za kisiasa, elimu, jinsia na hata makabila na kanda zetu tunakotoka ni lazima neno "kufanya siasa za kistaarabu...
Kusifia miradi inayotekelezwa na Serikali pamoja na jitihada za Serikali husika.
 
Ni kufanya siasa kwa uhalisia wake.

Hakuna siasa isiyo ya kistaarabu, hao wanaofdnya hicho kinachoitwa siasa zisizo za kistaarabu hawafanyi siasa, kuna vitu vingine wanafanya

Tufanye siasa katika uhalisia wake
 
Siasa za kistaarabu ni pale mfalme anapokuwa uchi hutakiwi kusema, au ukiona watu wamekaa ndani ya sinia la ubwabwa au kwenye buyu la asali wewe wape hi' tu halafu endelea na safari zako...
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 Exactly
 
Back
Top Bottom