Ni Njia Gani Sahihi ya Kumwambia Mpenzi Wako Kuwa Hauko Tayari Kuendelea Naye?

Ni Njia Gani Sahihi ya Kumwambia Mpenzi Wako Kuwa Hauko Tayari Kuendelea Naye?

madameA

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
435
Reaction score
176
Wapendwa habari zenu,
I hope everybody enjoyed the weekend.
Nimekuwa nikijiuliza hili swali bila kupata majibu, naomba mnisaidie.
kwa mfano uko kwenye mahusiano na mtu wako halafu ikatokea unataka kuachana naye kwa sababu zozote zile. Je ni njia ipi sahihi ambayo wewe ungeitumia kufikisha ujumbe kwa mpenzio au wewe unaipenda njia ipi mpenzi wako aitumie kukufikishia ujumbe kuwa hayuko tayari kuendelea na wewe? Baadhi ya njia zifuatazo zimekuwa zikitumika na watu wengi:
1. Kunyamaza kimya na kukata mwasiliano bila kuongea chochote?
2. kumpigia simu mlengwa na kumwambia ukweli kuwa hauhitaji kuwa naye.
3. Kumtumia sms na kumweleza lililo moyoni mwako.
4. Kumfanyia vituko ili akate tamaa yeye mwenyewe.

Je njia hizo ni sahihi kutumiwa au huwa zinatumika kwa makosa? Tujadili kwa pamoja tuone ni njia ipi sahihi ya kutumia kufikisha ujumbe (ambao sio mzuri kwa anayeachwa). Au kama kuna njia nyingine basi be free kuiweka wazi kwa faida yetu wote.
FUNGUKA MWANADADA, FUNGUKA MWANAKAKA UWANJA NI WAKO!
 
Kumpa makavu live utamuumiza sana hasa kama na yeye amekupenda sana, kukaa kimya ghafla pia itamuumiza sana. Jaribu kufanya vituko kidogo kidogo kila siku ukivizidisha , yani ya jana iwe afadhali kuliko ya leo ili achoke mwenyewe mdogo mdogo hadi aachie ngazi. Hii itamfanya awe ameshaanza kujitayarisha kisaikolojia na hivyo maumivu hayatakuwa makali kama ambavyo ungempa makavu live.
 
Kama mlivyoanza..ila kuongea ndo mpango mzima!!!!!!!

Kama kuna sababu genuine sio kubwa ila kama ni maneno ya mujini ndo utaanza kutafuta njia!!!!!

Mfano; Nimeamua kumrudia muumba wangu kwa ibada na funga kwa hiyo siwezi kuendelea na zinaa!!!!!!!

Hapo nini mbaya!!!!!!
 
hii ya Mrembo by nature nahisi inaweza kusaidia,japo kuwa a real Lady/gentleman hatoingia kwenye uhusiano kichwa kichwa na mwishowe afikirie kuvua gamba muite mkae chini mzungumze namna sahihi ya exit programme,where mmoja hata anaweza kuomba xtra time wakati mnajiandaa kuachana totally faida ya hii itamwacha kila mmoja na heshima na upendo kwa mwenzie,all in all ni bora usiingie kwenye mahusiano na mtu na kesho mtangaziane talaka!
 
Kumpa makavu live utamuumiza sana hasa kama na yeye amekupenda sana, kukaa kimya ghafla pia itamuumiza sana. Jaribu kufanya vituko kidogo kidogo kila siku ukivizidisha , yani ya jana iwe afadhali kuliko ya leo ili achoke mwenyewe mdogo mdogo hadi aachie ngazi. Hii itamfanya awe ameshaanza kujitayarisha kisaikolojia na hivyo maumivu hayatakuwa makali kama ambavyo ungempa makavu live.


Hapo mi nakuwa nimefungwa au?????

Mwanamke mwenye vituko ni kumfanya nyumba ndogo tu akome..akianza vituko we kuwa mpole huku unatafuta mwenye hadhi zaid yake kimya kimyaaaaaa siku akija gundua machozi juu yake wewe kama sio muhusika vileee!!!!!!

Vituko mwenzie dharau
 
mwambie ukweli.....kwamba.....unajua bana.....mimi huu uhusiano sioni future yake.....yaani sioni muendelezo kabisaaaa.......wewe kama vipi....kuna mtu unaona anakuvutia.....endelea tu.....mimi kwa sasa bado nipo nipo sana......

very simple.....
 
Sioni sababu ya kuanza visa wakati unaona kabisa huna sababu ya kuendelea na uhusiano. Tuma sms au piga simu, mwambie ungehitaji kuongea nae seriously, pangeni mda muafaka mkae muongee, mwambie ukweli na sababu za kutaka kufanya hivyo.
Wengi huwa wana-panic ila ni vema kumwambia mtu ukweli kuliko kupoteza mda na nguvu zake. Mambo ya kuzungushana, visa visivyoisha naona vimepitwa na wakati..mapenzi yenyewe siku hizi yamekuwa ya kuungaunga..
 
Hakuna wakati mbaya kwenye mahusiano kama wakati wa kutengana...haswa kama kulikuwa na mapenzi ya dhati.

Binafsi huwa ninaamini kwenye jambo moja, nalo ni kuelezana UKWELI maana KWELI huwa inaweka huru...
 
Dr naungana na wewe katika hili...kuwa muwazi ni kitu kizuri mno...

Kutengana huacha makovu ndio, lakini kidonda hicho hutibika na muda ukipita huwa chapona...

mwambie ukweli.....kwamba.....unajua bana.....mimi huu uhusiano sioni future yake.....yaani sioni muendelezo kabisaaaa.......wewe kama vipi....kuna mtu unaona anakuvutia.....endelea tu.....mimi kwa sasa bado nipo nipo sana......

very simple.....
 
Huwa natumia namba moja.... Just in case
 
Mwambie mpenzi wako alikuwa nje ya nchi ndio karudi!!hii wanaume wenzio wanaitumia sana
 
baada ya kumgegeda na kumchoka sasa hivi unatafuta mbinu za kumuacha ili uende kwa wengine,utazunguka sana lakin wako vile vile,hakuna tofauti
 
Kumpa makavu live utamuumiza sana hasa kama na yeye amekupenda sana, kukaa kimya ghafla pia itamuumiza sana. Jaribu kufanya vituko kidogo kidogo kila siku ukivizidisha , yani ya jana iwe afadhali kuliko ya leo ili achoke mwenyewe mdogo mdogo hadi aachie ngazi. Hii itamfanya awe ameshaanza kujitayarisha kisaikolojia na hivyo maumivu hayatakuwa makali kama ambavyo ungempa makavu live.


hii haifai inajenga chuki ,kuathiri kisaikolojia na upotevu wa muda.
 
it must have been love..but it's over now..... BAK njoo!
 
Kumpa makavu live utamuumiza sana hasa kama na yeye amekupenda sana, kukaa kimya ghafla pia itamuumiza sana. Jaribu kufanya vituko kidogo kidogo kila siku ukivizidisha , yani ya jana iwe afadhali kuliko ya leo ili achoke mwenyewe mdogo mdogo hadi aachie ngazi. Hii itamfanya awe ameshaanza kujitayarisha kisaikolojia na hivyo maumivu hayatakuwa makali kama ambavyo ungempa makavu live.

duhh kumbe umepanga kuniacha??
 
Back
Top Bottom