Ni sababu zipi za msingi zilizosababisha Wakuu wa Wilaya wengi kiasi hiki kuhamishwa vituo vyao vya kazi?

Ni sababu zipi za msingi zilizosababisha Wakuu wa Wilaya wengi kiasi hiki kuhamishwa vituo vyao vya kazi?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Nimestushwa Sana na taarifa iliyotolewa Ikulu, ikionyesha kuwa wakuu wa wilaya 48, wamehamishwa vituo vyao vya kazi.

Hivi Rais anawezaje kuwahamisha wakuu wa wilaya 48, Ili waende kwenye vituo vyao vipya vya kazi?

Pia nimuulize Rais, je alipokuwa anafanya uteuzi huo, hakujua mapungufu ya wakuu hao wa wilaya?

Kwa kuwa Mimi kama raia wa nchi hii, nina wajibu wa kuliuliza hili, Kwa kuwa najua uhamisho wowote, hususani wa hao vigogo, unaligharimu Taifa hili mabilioni ya pesa za uhamisho, ambazo tutakamuliwa Kwa Kodi na tozo Mimi na Wewe!

Hivi kama mamlaka ya uteuzi limegundua kuwa hao wakuu wa wilaya walifanya "madudu" kwenye vituo vyao vya awali, ni kwanini wasipigwe chini na kuachishwa kazi badala ya kuwahamisha vituo vyao vya kazi, ambapo mzigo wa kuwalipia hiyo inayoitwa "transfer allowance" tunaibeba sisi walipa Kodi wa nchi hii?

Hivi katika kipindi hiki ambacho nchi yetu inapitia kipindi kigumu mno, Cha upandaji wa gharama za maisha, hususani bei vya vyakula, ndiyo Serikali yetu, inatumia matumizi mabaya kiasi hicho Cha kuwalipia mabilioni ya pesa, wateule hao wa Rais?

Ndio maana tunaungana na hoja kuu ya Chama kikuu Cha upinzani nchini Cha Chadema, kuwa Taifa hili Kwa hivi Sasa linahitaji kuwa na Katiba mpya ambayo itampunguzia Kwa kiasi kikubwa madaraka makubwa mno aliyo nayo Rais wetu.

Ikumbukwe kuwa yeye Rais ndiye anayewateua wakuu wote wa wilaya 140 nchini na Wala huwezi muuliza, ni vigezo gani alivyotumia, katika uteuzi wake!

Pia ndiye anayewateua wakurugenzi wa wilaya, Kwa idadi hiyo hiyo ya 140

Pia ndiye anayewateua Mkuu wa Jeshi, IGP,Mkurugenzi wa Uchaguzi, Majaji na Wenyeviti wa Bodi mbalimbali za mashirika ya Umma

Haya madaraka makubwa mno ya ki-mungu-mtu ambayo Rais wa Taifa letu, amepewa na Katiba ya nchi yetu, ndiyo inayoliangamiza Taifa letu!
 
Mtumish kuhamishw kituo cha kaz ni jambo la kawaid ambalo husaidia ufanis wa kaz kwa mtumishi


Au wew ni yule mwanakondoo wa mchungaji kmaro
 
Subiri raisi atakwenda mwembe yanga kulitolea ufafanuzi kwa kuwa haijawahi kutokea hata mara moja ni jambo jipya!
 
Wilays 140 zote hizo za nini?,nchi ilitakiwa iwe na wilaya zisizozidi 60,mimi ninahitaji services delivers sio utitiri wa Wilaya, serikali yetu ni kubwa mno!,Namibia 🇳🇦 mikoa yao haizidi 15,hivyo hivyo na Zambia 🇿🇲 ila wananchi wake wanapata huduma zaidi ya kwetu sisi!,why mkoa wa Mbeya, Iringa iligawanywa?,huu ni upuuzi wa politicians wapeane vyeo
 
Mtumish kuhamishw kituo cha kaz ni jambo la kawaid ambalo husaidia ufanis wa kaz kwa mtumishi


Au wew ni yule mwanakondoo wa mchungaji kmaro
Hatukatai mtumishi kuhamishwa kituo Chake Cha kazi, kuwa ni kitu Cha kawaida katika utumishi wa Umma, lakini "concern" yangu kubwa ni kuona hao wateule wengi kiasi hicho, tunawalipia "transfer allowance" zao tunazokamuliwa sisi wananchi, Kwa kupitia Kodi zetu
 
Hoja ya hovyo kabisa, unataka wapigwe chini, hao watakaokuja wataingia bure?

Uongozi ni gharama, ni kimsingi mtumishi wa umma hatakiwi kukaa kituo kimoja zaidi ya miaka mitano. Inaathiri ufanisi na kuleta mazoea mazoea
 
Serikali inafumuliwa. Kwa hiyo viongozi wengi lazima wabadilishwe. Rais lazima aonekane kwamba anafahamu Kiswahili. Akisema "kufumua" maana yake lazima iwe devastating changes. Ndio sababu ya msingi viongozi wengi kubadilishwa.
 
Hatukatai mtumishi kuhamishwa kituo Chao Cha kazi, lakini "concern" yangu kubwa ni kuona hao wateule wengi kiasi hicho, tunawalipia "transfer allowance" zao tunakamuliwa sisi wananchi, Kwa kupitia Kodi zetu
Na mazuzu wengi humu wanajadili zaidi nani katemwa na nani kalamba asali, upande wa pili wa costs za mabadiliko haya hawajui, ni craze mkuu kuona middle class wanajadili upupu na hawaoni kabisa upande unaotuathiri kimaisha, now for the next 4mths tutashuhudia malori ya Halmashauri yakikimbizana barabarani na samani za ma DCs,unalitoa Lori Temeke hadi Korogwe why!,kama ameshindwa to perform hapo Temeke why umpeleke Korogwe?what's the difference?(sorry nimetumia mfano wa ke,Sina maana ya to undermine them,binafsi ninapiga vita sana kuhusu GBV, Nami ni ke!)
 
Wilays 140 zote hizo za nini?,nchi ilitakiwa iwe na wilaya zisizozidi 60,mimi ninahitaji services delivers sio utitiri wa Wilaya, serikali yetu ni kubwa mno!,Namibia [emoji1176] mikoa yao haizidi 15,hivyo hivyo na Zambia [emoji1268] ila wananchi wake wanapata huduma zaidi ya kwetu sisi!,why mkoa wa Mbeya, Iringa iligawanywa?,huu ni upuuzi wa politicians wapeane vyeo
Na bado walitaka chato iwe mkoa,haya majitu hayafai watanzania wameendelea kuwa masikini,wakisubiri kuletewa nguo na vitamba na kanga za CCM wakati wa uchaguzi,Inaumiza na kusikitisha sana.
 
Mbowe siku hizi hazungumzii swala la Katiba.
ukweli ni kwamba mamlaka ya raisi yanapaswa kupunguzwa.
Katiba ya Tz inamfanya Raisi kuwa Mungu mtu. Ndio maana kuna machawa wengi. Ubunifu wa kimkakati wa maendeleo hakuna
 
Yaweza kuwa ni utenguzi ulifanyika hivi karibuni na hatimaye kufuatiwa na tukio hili!
 
Wilays 140 zote hizo za nini?,nchi ilitakiwa iwe na wilaya zisizozidi 60,mimi ninahitaji services delivers sio utitiri wa Wilaya, serikali yetu ni kubwa mno!,Namibia 🇳🇦 mikoa yao haizidi 15,hivyo hivyo na Zambia 🇿🇲 ila wananchi wake wanapata huduma zaidi ya kwetu sisi!,why mkoa wa Mbeya, Iringa iligawanywa?,huu ni upuuzi wa politicians wapeane vyeo

Hawa wangekuwa wanachaguliwa kwa njia chaguzi za kidemokrasia zilizo HURU na za HAKI, ujinga huu usingekuwa unafanyika. Na pia ingeleta discipline ya utendaji na uwajibikaji.
Umeongea hoja ya msingi Sana

Hawa wakuu wa wilaya, wanapaswa wapigiwe kura na wananchi wa wilaya husika.

Ndiyo maana hoja ya kupata Katiba mpya Sasa inazidi kuwa na nguvu Sana hivi Sasa

Ni katika hali hiyo pekee, hao watendaji wangekuwa na Discipline ya hali ya juu sana, lakini Kwa mtindo huu wa Rais wa nchi kuwateua, hao wakuu wa wilaya wataendelea kula Kwa urefu wa kamba zao.😎
By Samia Suluhu's voice
 
Tshs.15,000,000 X 48 =720,000,000/=

NB: Zaidi ya 720,000,000/= Za uhamisho zinakwenda kulipwa,achana na za MaDC wapya.
Bahati nzuri ndigu yetu, unetuletea actual figure, ambayo wananchi tutapaswa yukamuliwe, kulipa hizo "transfer allowances"😎
 
Back
Top Bottom