Ni sahihi kuchimba kisima maji kipindi cha masika?

Ni sahihi kuchimba kisima maji kipindi cha masika?

Futi 250 !!!? Hiyo hapana, chukulia futi 40 ni sawa na mlingoti wa umeme au container lile kubwa .

Sasa pima kwenda chini, kwa jinsi walivyochimba kwangu na uzoefu nilioupata uwezekano wa kawaida kuchimba bila kuhitaji nyongeza ya HEWA ni futi 80.
Kwa mujibu wa maelezo yake, anaweza kuchimba hata zaidi ya futi 150 kwenda chini, lakini mimi sikihitaji kirefu kiasi hicho. Naamini maji yapo umbali usiozidi futi 30 chini ya ardhi.
 
1. Ndio uwezekano wa kisima kilichochimbwa kwa mikono wakati wa masika ni mkubwa sana, kwa sababu wakati kina cha maji ya ardhini hupanda wakati wa masika hivyo maji kuapatikana na katika kina kifupi, na hushuka katika kipindi cha kiangazi hivyo maji hupatikana katika kina kirefu.

Haisumbui kuchimba kisima muda wa kiangazi au masika, ila kinachotakikana ni kwa mchimbaji kuwa na uelewa wa haidrojiolojia ya eneo husika, na hapa ndipo unakuja umuhimu wa mchimbaji kufanya kautafiti ili kufanya maamuzi sahihi ya urefu wa kisima.
 
Ni sahihi kuchimba kisima cha maji kipindi cha mvua?

Sikuwa na mpango wa kukichimba muda huu, lakini mtu anayelihudumia shamba langu kwa sasa kaniambia anaweza kukichimba kwa bei nafuu hadi ayakute maji. Nilipomwambia kuwa visima vianvyochimbwa nyakati za mvua zinaweza kuishiwa maji wakati wa kiangazi, kajibu kuwa hilo likitokea, atakifukua tena hadi ayakute maji.

Kwa wenye uzoefu, nini ushauri wenu?
1. Ni kweli kuwa kisima kichimbwacho kwa mikono nyakati za mvua zina uwezekano wa kuishiwa maji wakati wa kiangazi?

2. Ikiwa kisima kitakaukiwa maji wakati wa kiangazi, kuna uwezekano wa kupata maji endapo kitafukuliwa zaidi kwenda chini?

Asanteni🙏🙏🙏
2. Kuhusu kuongeza urefu wa kisima baada ya kukichimba, hiyo inategemea na namna kisima kilivyochimbwa na kudizainiwa.
 
Hivi kuna sehemu hata wakitoboa futi nyingi kwenda chini hawakuti maji?
 
Back
Top Bottom