Ni sahihi kumpa kichapo dingi iwapo anampiga mama?

Ni sahihi kumpa kichapo dingi iwapo anampiga mama?

Kuna washikaji wangu walifanya kama unavyo taka kufanya wewe . Walimchezeshea kichapo mshua wao hadi nguo za mshua zikavuka. Hawa jamaa ni mtu na mdogo wote wanaume wana mdogo wao wakike pia huyu wa kike alikua bado mdogo .


Ila hawa jamaa hakuna kitu walifanya kikafanikiwa na hakuna kitu cha thamani walinunua kikadumu zaidi ya mwezi.

Mshua wao alicho kifanya aliamua kuto Fukuza mtu wala yeye kuondoka ila aliamua kujitenga na wao. Alichukua tu geto moja la nje na kuwaachia nyumba kubwa na wao na mama yao.

So mzee anakageto kake la nje hana habari na mtu na kubwa kuliko mzee ana pensheni yaani anaishi vimaisha vyake na tangu siku hiyo hajawahi ongea na hao watoto na huu ni mwaka 15 na zaidi tangu tukio litokee.

Yaani mzee ni kama amewatenga na hataki hata habari zao. Vikao vya kibalozi vya aina yote vilikaliwa kusuruhisha jibu la mzee lilikua hata nyie mnashida na watoto chukueni kama mnawataka na anae taka huyo mke amchukue pia mimi sina matatizo na mtu .na huyu mwanamke alisha lia machozi ya rangi zote alimaliza ila mzee kadinda

Huyu mzee anapendeza kichizi yani yaani full mastory na watu huku nje na ni mcheshi balaa ila ukitaka kumuuzi mgusie Jabari za wanawe.


So bro kuwa makini na hatua unayo taka kupiga
 
Jamaa mmoja mtu mzima na familia yake ana wazazi wake ambao wako above 60. Sasa dingi yake akajitia ukidume kumpiga mama yake mbele ya jamaa. Jamaa akaingilia na kumtwanga baba yake, akimkunja chini. Hili suala ni sahihi? Baba yako akimpiga mama yako mbele yako unaweza ungilia kupigana na dingi?
Wakati wanaoana ulikuwepo? Mpige mitama halafu akwambie unatembea na Mama yako ndiyo maana unamtete na kumpiga yeye. Sijui utajificha wapi na hiyo laana
 
Anatandikwa tu akileta upuuzi wazazi wenye kujitambua hawakwaruzani mbele ya macho ya watoto kama ugomvi ameshindwa kuuacha baada ya kuamuliwa na kujifanya nunda kuendelea kumfanya kibogoyo maza kinacho fuatia ni makonde mpaka akili zimrudi
Na kitandani kamtoa babako kifuani pa mamako ili umlale wewe kwa maana nayo hayo ni mapigano!
Kama huwezi,jibu unalo.
 
Back
Top Bottom