Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni kujitahidi kuacha malumbano na ngumi mbele za watoto tu mkuu hakuna namna nyingine.Mambo haya unaweza dhani ni story ilaa omba yasitokee kwa wazazi wako ni Mtihani mkubwa sanaa.. Kama mzee hajitambui anajenga chuki na mwisho laana kwa watoto lakini Nilichojifunzaa Jitahidi kusuluhisha ugomvi wa baba na mama bila kupendelea na mbebeshe mzee majukumu ya kumantain amani ndani ya familia..
Mjomba kibaka kudhuru au kuua mtu kwa sababu yoyote ile ni kosa, ila hakimu kufunga au kunyonga huyo kibaka siyo kosa, kama haujaelewa soma tenaIla hao watoto kumpiga baba yao badala ya kuamulia ugomvi sio Domestic violence ni international violence si ndio?!
Umenena vyema mkuu
Utakubali mtu ampige mama yako?Laana inatafutwa kwa njia nyepesi, upo kwake unataka kumletea jeuri akiwa anamwadhibu mkewe?
Stori za vijiweni. Pia sijasema mimi ndiyo nataka kuchukua hiyo hatua.Kuna washikaji wangu walifanya kama unavyo taka kufanya wewe . Walimchezeshea kichapo mshua wao hadi nguo za mshua zikavuka. Hawa jamaa ni mtu na mdogo wote wanaume wana mdogo wao wakike pia huyu wa kike alikua bado mdogo .
Ila hawa jamaa hakuna kitu walifanya kikafanikiwa na hakuna kitu cha thamani walinunua kikadumu zaidi ya mwezi.
Mshua wao alicho kifanya aliamua kuto Fukuza mtu wala yeye kuondoka ila aliamua kujitenga na wao. Alichukua tu geto moja la nje na kuwaachia nyumba kubwa na wao na mama yao.
So mzee anakageto kake la nje hana habari na mtu na kubwa kuliko mzee ana pensheni yaani anaishi vimaisha vyake na tangu siku hiyo hajawahi ongea na hao watoto na huu ni mwaka 15 na zaidi tangu tukio litokee.
Yaani mzee ni kama amewatenga na hataki hata habari zao. Vikao vya kibalozi vya aina yote vilikaliwa kusuruhisha jibu la mzee lilikua hata nyie mnashida na watoto chukueni kama mnawataka na anae taka huyo mke amchukue pia mimi sina matatizo na mtu .na huyu mwanamke alisha lia machozi ya rangi zote alimaliza ila mzee kadinda
Huyu mzee anapendeza kichizi yani yaani full mastory na watu huku nje na ni mcheshi balaa ila ukitaka kumuuzi mgusie Jabari za wanawe.
So bro kuwa makini na hatua unayo taka kupiga
Safi.Anatandikwa tu akileta upuuzi wazazi wenye kujitambua hawakwaruzani mbele ya macho ya watoto kama ugomvi ameshindwa kuuacha baada ya kuamuliwa na kujifanya nunda kuendelea kumfanya kibogoyo maza kinacho fuatia ni makonde mpaka akili zimrudi
Huyo dingi anayekusingizia hivyo atakuwa fala anayestahili kabisa kupigwa.Wakati wanaoana ulikuwepo? Mpige mitama halafu akwambie unatembea na Mama yako ndiyo maana unamtete na kumpiga yeye. Sijui utajificha wapi na hiyo laana
Hata kuamua ni kuingilia.Unaanzaje kuingilia ugomvi wa wazazi wako?Ni kukosa busara.Waamue tu na siyo kumpiga mmoja.
Vipi baba yako wa kambo akinyimwa utelezi na mama yako halafu akaanza kumpiga? Au hili ni kwa baba mzazi tu!!?baba yako akikwambia ana mpiga sababu amemnyima utelezi utajibuje,je nawewe nisahihi mtoto wako kukuchapa makofi pale unapogombana na mama yake? mambo mengine nikujipa laana mwenyewe, maana ulichomfanyia baba yako ndivyo utakavyo fanyiwa na kwa uzao wakopia
Heri wapatanishi .....!Haina nia mbaya.Hata kuamua ni kuingilia.
PoaHeri wapatanishi .....!Haina nia mbaya.
Katika ubora wako mtibeliLabda ungejiuliza ni Sahihi Wakati ukimpiga Mkeo alafu mtoto wako akaja kukukata mitama?
Jibu utakalotoa ndio sahihi.
Labda kama unayeuliza ni Mwanamke. Tutakusaidia majibu.
Mkuu Uliwahi kuwa mwalimu Cuba?Labda ungejiuliza ni Sahihi Wakati ukimpiga Mkeo alafu mtoto wako akaja kukukata mitama?
Jibu utakalotoa ndio sahihi.
Labda kama unayeuliza ni Mwanamke. Tutakusaidia majibu.