Ni sahihi kumpa mtoto mchanga maziwa ya kopo badala ya kumnyonyesha maziwa ya mama?


Maziwa ya kopo hayana shida, ila usininunue ya Tanzania, kuna dactari alinishauri mimi binafsi nitumie lactogen ya UK, na kuwa makini na expire dat, sababu kubwa ni kwamba mke hakuwa na maziwa kabisa kwa watoto wangu wote watano! So hawakuwawi nyonya ya Mama yao, ila ni gharama sana!
 
Shida ipo. Pamoja na nutrients kunyonyesha kunatengeneza bonding kati ya mama na mtoto
Pia mtoto akinyonya maziwa ya mama bila kuchanganya na chochote kwa miezi sita, anakuwa mwenye akili sana, haumwi hovyo hovyo, mchangamfu na mwenye afya nzuri sana. Hawa wanaolelewa na maziwa ya kopo mwisho wa siku wanakuwa kina kaoge, watukutu na spana mkononi magonjwa mara kwa mara.

Maziwa ya kopo hayana kinga kwa mtoto tofauti na ya mama
 
why
 
vipi vinakosekana kwenye maziwa ya kopo?
Kinga..
Maziwa ya mama yanakinga ya magonjwa mbali mbali kwa mtoto na pia ni muhimu sana kwenye kukuza ubongo wa mtoto tofauti na ya kopo hayana vitu hvyo muhimu ndio maana hata kwenye maziwa ya kopo yote yamekuandikia "maziwa ya mama ni bora kwa mtoto" kama huamini kaangalie kwny kopo unalompa mwanao
 

Vitaje.

Ya kopo hayana vitu gani?
 
sababu gani za kitaalam
Maziwa ya mama yana antibodies i. e During breastfeeding Immunogloblins G pass from the mother to the infants na kumpa mtoto kinga dhidi ya ear infection, diarrhoea, meningitis etc. Maziwa ya mama yako easily digested kuliko maziwa ya kopo na watoto wanaopata maziwa ya mama wako na fewer hospitalizations kuliko ambao hawakupata
 
Paediatricians wote duniani wanashauri hivyo
 
kunyionyesha inabaki ni choice,sio kwamba alternative hamna.
Sawa ni choice but kwa faida ya mwanao nyonyesha. Maziwa ya kopo hayana antibodies na siku mtoto akiuugua kwa sababu ya kinga dhaifu utalazwa na hutasema kulazwa hospitalini ni choice
 
Hata ukiwaachisha si mbaya. Kama ulifanya Exclusive breast feeding kwa miezi sita na ukaendelea kunyonyesha hadi angalau mwaka mmoja, ukiachisha hakuna noma.
 
Sawa ni choice but kwa faida ya mwanao nyonyesha. Maziwa ya kopo hayana antibodies na siku mtoto akiuugua kwa sababu ya kinga dhaifu utalazwa na hutasema kulazwa hospitalini ni choice
Wewe hahaaa umen'gang'ania WHO sijui hiki sijui kile, mbona hao WHO hawajakuambia specific watoto wangapi wamekufa kutokana na kupata maziwa ya Kopo??? Au mtoto gani ameathirika kiakili kutokana na maziwa ya Kopo? Acha uduanzi mkuu, huitendei haki profession yako, lol
 
Mi pia nawaza kuandaa kopo la formula, make maziwa kuna muda yanakata hayatoki, mara yanamimikika sijui kwanini.... Sasa muda ambao hayatoki naona kijana anapata shida
 
Acha upotoshaji wewe lols et maziwa yakopo yanafanya watu wawe kama kaoge tangu lini???
 
Siyo sahihi kwa mtoto yeyote given that kafikisha miezi sita hapo unaweza kufanya hivyo....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…