Ni sahihi TBC kuonyesha michuano ya CAF Champions League?

Ni sahihi TBC kuonyesha michuano ya CAF Champions League?


Hapo utakuta ulilipia ili uone halafu rafiki yako akakupigia kukuraarifu TBC wanaonesha bure kabisa. Roho mbaya hapo unatamani upige ukuta ngumi.
 
Mbona umewasemea Azam tuu wakat kuna Dstv pia. Any way toka nimenunua kisimbuzi cha Azam mwaka 2017 sijawah pitisha mwezi bila kulipia na huwa nalipq kile cha bei ya juu ambacho kwa sasa ni 35k na sijawah kuona cha maana walichonacho Azam... Acha tibisii wawape watz burudan
Hujawahi kupitisha mwezi bila kulipia Kisha unasema hujaona Cha maana aisee!!
 
Imagine wewe ndio mmiliki wa Azam TV halafu unasikia TBC wanaonesha bure michuano mikubwa ya CAF CHAMPIONS LEAGUE tena kupitia kisumbusi chako hicho hicho ambacho wewe una wataka watu walipie elfu 24 kuona mechi hizo!

Kibiashara limekaaje hili? Ingekuwa wewe ndio mmiliki wa Azam TV ungefanya nini?

Anauliza mdau kutoka X.
siwezi kuangalia mpira kupitia tbc bora tuu nilalee
 
Kama vipi TBC nayo irushe ligi kuu, kama ni mitambo hatakosa, watangazaji mahiri inayo
 
Anauliza mdau wa X au wauliza wewe...?

TBC ni televisheni ya umma, ipo huru kuonesha kila mchezo uwe wa CAF, UEFA, FIFA n.k kama tu ikikidhi vigezo vya vibali...
ikidhi tu hivyo vigezo tupate burudani kupitia tv ya umma, tumechoka na utemi wa azam ni ghali sana kifurushi chake kwa mwezi
 
Hivi kuiona Tbc sio lazima uwe umelipia king'amuzi husika? Sijawahi kufuatilia
 
Mipira ya Africa ya ndani yote TV za Taifa zina haki ya kuonyesha mipira yote sema wale Dstv walikua wanatoa rushwa kubwa kwa baadhi ya Nchi zisiwe zinaonyesha ili wao wauze wiki iliyopita pana wakuu wawili wameacha kazi kwa kashfa hiyo SA Mult Choice sema hii haki wengi walishaisahau wanaona sio haki yao maana FIFA na CAF wanatoa pesa kusapoti tuone Mpira kupitia TV ya Taifa..
 
Mipira ya Africa ya ndani yote TV za Taifa zina haki ya kuonyesha mipira yote sema wale Dstv walikua wanatoa rushwa kubwa kwa baadhi ya Nchi zisiwe zinaonyesha ili wao wauze wiki iliyopita pana wakuu wawili wameacha kazi kwa kashfa hiyo SA Mult Choice sema hii haki wengi walishaisahau wanaona sio haki yao maana FIFA na CAF wanatoa pesa kusapoti tuone Mpira kupitia TV ya Taifa..
mabepari yanataka yahodhi matangazo yote ya mpira tv za taifa zisioneshe
 
Imagine wewe ndio mmiliki wa Azam TV halafu unasikia TBC wanaonesha bure michuano mikubwa ya CAF CHAMPIONS LEAGUE tena kupitia kisumbusi chako hicho hicho ambacho wewe una wataka watu walipie elfu 24 kuona mechi hizo!

Kibiashara limekaaje hili? Ingekuwa wewe ndio mmiliki wa Azam TV ungefanya nini?

Anauliza mdau kutoka X.
Ulitaka tuangalie kupitia kwenye domo lako?
 
Ukifikiria hivyo sana utajijuwa wewe!
Utaanza kuuliza kwanini yule ana mke mzuri kuliko Mimi wakati wangu namhudumia kuliko yeye..
Utaanza kujiumiza kwanini yule ana gari nzuri wakati Hana kazi kama yangu?!
Acha roho mbaya ndugu....
 
Imagine wewe ndio mmiliki wa Azam TV halafu unasikia TBC wanaonesha bure michuano mikubwa ya CAF CHAMPIONS LEAGUE tena kupitia kisumbusi chako hicho hicho ambacho wewe una wataka watu walipie elfu 24 kuona mechi hizo!

Kibiashara limekaaje hili? Ingekuwa wewe ndio mmiliki wa Azam TV ungefanya nini?

Anauliza mdau kutoka X.
Inategemea na leseni inatolewaje.

Mfano Epl mwenye leseni Kusini Jangwa la sahara ni Dstv, mtu yoyote atakayeonesha inabidi achukue leseni kwao.

Kama Leseni Ya Tanzania anayo Azam basi TBC wamenunua kwa Azam, kama Michuano haina Leseni exclusive basi wote Wawili wanaweza kununua Caf na Waka onesha.

Mwenye kauli ya mwisho ni Caf wenyewe na sio Azam.
 
Back
Top Bottom