Mr George Francis
JF-Expert Member
- Jun 27, 2022
- 234
- 376
Jioni ya jana nikiwa natoka katika harakati zangu za kila siku niliamua kufaya mazoezi kwa kutembea kwa miguu tokea kazini hadi nyumbani tofauti na nilivyozoea malanyingi huwa napanda usafiri wa umma asubuhi na jioni kwasababu sina chombo binafsi cha usafiri.
Nikiwa nakatiza katika mitaa karibu kidogo tu na nyumbani nikaona kuna zogo kubwa sana nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa. Kauli nilizokuwa nazisikia tangu nikiwa mbali zilinifanya nisogee karibu nikajionee mwenyewe kuna tukio gani maeneo yale.
Mala wengine wanasema "haiwezekani hawa lazima wafungwe!" Wengine wanasema "mwenyekiti nae afungwe anawafuga sana washenzi kama hawa."
Kiukweli sikuelewa, nilipata hamasa zaidi ya kwenda kushuhudia kitu gani hasa kimetokea.
Kufika naona Mama Jacqueline na mumewe wamezingirwa na umati mkubwa wa watu, wengine wakiwapiga na wengine akizuia wasipigwe basi ni vurugu mtindo mmoja. Huku Jacqueline ameshikwa na mama mmoja aliyekuwa anajitahidi kumfuta machozi na kumwambia asilie Mungu atamsaidia.
Nilimuangalia Jacqueline kwa umakini zaidi nikaona hayupo sawa, damu zinachuruzika miguuni, nikamuuliza yule mama aliyesimama nae, "vipi huyo mtoto amepatwa na jeraha gani?"
Akanijibu kwa kifupi,
"Yani we acha tu kaka yangu Dunia hii ina maajabu mengi."
Nikamalizia kusema
"na haya ndio maajabu yenyewe."
Japo bado nilikuwa sijaelewa ni kitu gani hasa kilichotokea.
Niliamua kumpandisha sketi yake kidogo yule mtoto ili nione jeraha lenyewe linalotoa damu, yule mama ndio akaniambia
"Hapana, usimfunue zaidi hautaona. Huyu mtoto amelawitiwa na baba yake wa kambo."
Nilishangaa sana
"Sasa mtoto amefanyiwa ukatili kama huu na bado mpo hapa! Ebu tumpeleke hospitali haraka iwezekanavyo."
Nilisaidiwa na watu wachache kumkimbiza mtoto Jacqueline hospitali huku tukiwaacha watu wengine pale ili wafanye taratibu za kuwafikisha watuhumiwa katika kituo cha polisi kwa taratibu nyingine za kisheria.
Kufika hospitali, walikataa kutoa huduma yoyote hadi wapate PF3 au report maalumu kutoka kituo cha polisi inachothibisha kutokea kwa tukio lililopelekea majeraha kwa mtoto yule.
Tumeambiwa hilo ni takwa la kisheria hivyo hawawezi kufanya vile tunavyotaka sisi, kwani vinginevyo watakuwa wanakiuka sheria na maadili ya kazi au taaluma yao kwa ujumla. Ilibidi tuendelee kusubiri tu, hakuna namna.
Wazazi walifikishwa kituo cha polisi na report maalumu ikaandaliwa na kuletwa hospitali. Lakini kipindi tunasubiri huduma nilipata nafasi ya kuzungumza na Jacqueline mtoto wa miaka nane (08).
Mtoto huyu alinisimulia mambo mengi sana, mambo ya kutisha kiasi ambacho kama ningeyajua hayo kabla ya kumleta hospitali pengine na mimi ningetakiwa kwenda jela kwa kosa la mauaji. Kwa hasira nilizonazo nahisi ningepiga wale wazazi wake kiasi hata cha kuua kwa ushetani waliokuwa wakiufanya kwa mtoto Jacqueline.
Jacqueline amenileza kuwa, baba yake mzazi alifariki tangu akiwa na miaka mitatu. Mwaka mmoja baadae mama yake aliolewa na huyu baba mwingine tajiri aliyekosa akili wala chembe ya ubinadamu. Kwa uchungu sana Jacqueline ananiambia.
" Baba alianza kuniingilia ukeni muda mrefu tangu mwishoni mwa mwaka wa juzi. Ilikuwa ni kipindi cha likizo shuleni. Nilimwambia mama lakini mama alinipiga na kuniambia niache ujinga, baba hawezi kufanya hivyo, labda nimefanya na mtu mwingine huko mtaani arafu namsingizia baba. Baba nae alinipiga eti akidai namdharirisha."
Jacqueline anaendelea kusema,
"Kuna siku baba alinivuta chumbani kwake, mama alikuwa ametoka lakini alirudi ghafra na kumkuta baba akiwa juu yangu, huku akiniziba mdomo nisipige kelele. Niliishiwa pumzi nikahisi nakufa.
Siku ile nilijua sasa mama atakuwa upande wangu kunitetea lakini hakufanya hivyo. Nilirejea chumbani kwangu, baadae mama nae akaja chumbani kwangu na kunisihi nisimwambie mtu yoyote kwani nitamtia aibu yeye pamoja na mume wake yaani baba yangu wa kambo."
Jamani Dunia ina mambo hii. Ndugu msomaji endelea kusoma tafadhali. Jacqueline anaendelea kueleza
"Mama ameniambia, huoni hapa tunaishi kwenye nyumba ya kifahari, tunakula vizuri, tunalala pazuri, tuna magari mazuri ya kutembelea!! Huoni mwanangu kama ukithubutu kumwambia mtu yeyote basi baba yako atafungwa? Lakini pia hata sisi hapa ndugu zake watatufukuza kwasababu sina mtoto nae, wewe ndio mtoto wa pekee. Mama alinisihi zaidi nivumilie."
Duh! Anaendelea kusema
"Kuna siku nilimwambia Madame Glory, mwalimu wetu wa darasa ambae ni rafiki na mama yangu. Nilidhani atawaambia walimu wenzake ili wajue namna ya kunisaidia lakini hakuwaambia. Jioni tulivyotoka shule alinipeleka kwa mwenyekiti wa mtaa lakini walishauriana waachane na mambo hayo, kwani hayawahusu, mimi waliniambia tu nisiwe na wasiwasi, watamuita baba ili wamkanye aache tabia mbaya lakini hata hivyo sikuona mabadiriko yoyote niliendelea kuteseka tu."
Dah! Hapo niligundua uwezo mkubwa wa ufahamu wa mtoto Jacqueline, kwani anasimulia kwa umakini kama vile anayeongea ni mtu mzima, kumbe ni mtoto wa miaka nane tu.
Jacqueline anazidi kutokwa machozi, anakohoa kidogo kisha anaendelea kunisimulia,
"Leo hii ndio baba ame.... amenilalia na kuniingiza kwa nyuma."
Hapo akaanza kulia kwa uchungu sana, nikakosa namna ya kumbembeleza.
Kisha kwa sauti ya chini na kwa shida sana akaniambia maneno ya mwisho niende nikawaambie wazazi wake,
"Mama yangu, mwanao nakufa, najua sitapona. NI SAWA UMENIZAA, LAKINI UMEFUPISHA MAISHA YANGU. Mwambie na baba kuwa naenda kumwambia Mungu juu ya ubaya wote mlionifanyia"
Nurse mmoja alikuja kunitoa kwenye chumba alicholazwa Jacqueline akisubiri matibabu. Aliniambia PF3 imeshafika hivyo tunaomba utoke nje ili tuanze kumuhudumia.
Hazikupita hata dakika tatu nurse yuleyule alikuja kuniambia, mgonjwa wetu amepoteza maisha. Niliumia kupita kiasi kana kwamba mimi ndio baba halisi wa mtoto Jacqueline.
Dunia ina watu wa ajabu sana. Kuna mambo yanaumiza sana, lakini acha niishie hapa. Nashindwa kuendelea kuandika mengi zaidi kuhusu maisha ya mtoto Jacqueline.
Ni kweli watoto wengi katika jamii zetu wanapitia magumu kama haya. Jamii tushirikiane kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.
BILA SHAKA UMEVUTIWA NA STORY HII YENYE MAFUNZO, HIVYO NAOMBA KURA YAKO TAFADHALI.
______________________
Mwandishi: Mr. George Francis
Simu: 0713736006
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Nikiwa nakatiza katika mitaa karibu kidogo tu na nyumbani nikaona kuna zogo kubwa sana nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa. Kauli nilizokuwa nazisikia tangu nikiwa mbali zilinifanya nisogee karibu nikajionee mwenyewe kuna tukio gani maeneo yale.
Mala wengine wanasema "haiwezekani hawa lazima wafungwe!" Wengine wanasema "mwenyekiti nae afungwe anawafuga sana washenzi kama hawa."
Kiukweli sikuelewa, nilipata hamasa zaidi ya kwenda kushuhudia kitu gani hasa kimetokea.
Kufika naona Mama Jacqueline na mumewe wamezingirwa na umati mkubwa wa watu, wengine wakiwapiga na wengine akizuia wasipigwe basi ni vurugu mtindo mmoja. Huku Jacqueline ameshikwa na mama mmoja aliyekuwa anajitahidi kumfuta machozi na kumwambia asilie Mungu atamsaidia.
Nilimuangalia Jacqueline kwa umakini zaidi nikaona hayupo sawa, damu zinachuruzika miguuni, nikamuuliza yule mama aliyesimama nae, "vipi huyo mtoto amepatwa na jeraha gani?"
Akanijibu kwa kifupi,
"Yani we acha tu kaka yangu Dunia hii ina maajabu mengi."
Nikamalizia kusema
"na haya ndio maajabu yenyewe."
Japo bado nilikuwa sijaelewa ni kitu gani hasa kilichotokea.
Niliamua kumpandisha sketi yake kidogo yule mtoto ili nione jeraha lenyewe linalotoa damu, yule mama ndio akaniambia
"Hapana, usimfunue zaidi hautaona. Huyu mtoto amelawitiwa na baba yake wa kambo."
Nilishangaa sana
"Sasa mtoto amefanyiwa ukatili kama huu na bado mpo hapa! Ebu tumpeleke hospitali haraka iwezekanavyo."
Nilisaidiwa na watu wachache kumkimbiza mtoto Jacqueline hospitali huku tukiwaacha watu wengine pale ili wafanye taratibu za kuwafikisha watuhumiwa katika kituo cha polisi kwa taratibu nyingine za kisheria.
Kufika hospitali, walikataa kutoa huduma yoyote hadi wapate PF3 au report maalumu kutoka kituo cha polisi inachothibisha kutokea kwa tukio lililopelekea majeraha kwa mtoto yule.
Tumeambiwa hilo ni takwa la kisheria hivyo hawawezi kufanya vile tunavyotaka sisi, kwani vinginevyo watakuwa wanakiuka sheria na maadili ya kazi au taaluma yao kwa ujumla. Ilibidi tuendelee kusubiri tu, hakuna namna.
Wazazi walifikishwa kituo cha polisi na report maalumu ikaandaliwa na kuletwa hospitali. Lakini kipindi tunasubiri huduma nilipata nafasi ya kuzungumza na Jacqueline mtoto wa miaka nane (08).
Mtoto huyu alinisimulia mambo mengi sana, mambo ya kutisha kiasi ambacho kama ningeyajua hayo kabla ya kumleta hospitali pengine na mimi ningetakiwa kwenda jela kwa kosa la mauaji. Kwa hasira nilizonazo nahisi ningepiga wale wazazi wake kiasi hata cha kuua kwa ushetani waliokuwa wakiufanya kwa mtoto Jacqueline.
Jacqueline amenileza kuwa, baba yake mzazi alifariki tangu akiwa na miaka mitatu. Mwaka mmoja baadae mama yake aliolewa na huyu baba mwingine tajiri aliyekosa akili wala chembe ya ubinadamu. Kwa uchungu sana Jacqueline ananiambia.
" Baba alianza kuniingilia ukeni muda mrefu tangu mwishoni mwa mwaka wa juzi. Ilikuwa ni kipindi cha likizo shuleni. Nilimwambia mama lakini mama alinipiga na kuniambia niache ujinga, baba hawezi kufanya hivyo, labda nimefanya na mtu mwingine huko mtaani arafu namsingizia baba. Baba nae alinipiga eti akidai namdharirisha."
Jacqueline anaendelea kusema,
"Kuna siku baba alinivuta chumbani kwake, mama alikuwa ametoka lakini alirudi ghafra na kumkuta baba akiwa juu yangu, huku akiniziba mdomo nisipige kelele. Niliishiwa pumzi nikahisi nakufa.
Siku ile nilijua sasa mama atakuwa upande wangu kunitetea lakini hakufanya hivyo. Nilirejea chumbani kwangu, baadae mama nae akaja chumbani kwangu na kunisihi nisimwambie mtu yoyote kwani nitamtia aibu yeye pamoja na mume wake yaani baba yangu wa kambo."
Jamani Dunia ina mambo hii. Ndugu msomaji endelea kusoma tafadhali. Jacqueline anaendelea kueleza
"Mama ameniambia, huoni hapa tunaishi kwenye nyumba ya kifahari, tunakula vizuri, tunalala pazuri, tuna magari mazuri ya kutembelea!! Huoni mwanangu kama ukithubutu kumwambia mtu yeyote basi baba yako atafungwa? Lakini pia hata sisi hapa ndugu zake watatufukuza kwasababu sina mtoto nae, wewe ndio mtoto wa pekee. Mama alinisihi zaidi nivumilie."
Duh! Anaendelea kusema
"Kuna siku nilimwambia Madame Glory, mwalimu wetu wa darasa ambae ni rafiki na mama yangu. Nilidhani atawaambia walimu wenzake ili wajue namna ya kunisaidia lakini hakuwaambia. Jioni tulivyotoka shule alinipeleka kwa mwenyekiti wa mtaa lakini walishauriana waachane na mambo hayo, kwani hayawahusu, mimi waliniambia tu nisiwe na wasiwasi, watamuita baba ili wamkanye aache tabia mbaya lakini hata hivyo sikuona mabadiriko yoyote niliendelea kuteseka tu."
Dah! Hapo niligundua uwezo mkubwa wa ufahamu wa mtoto Jacqueline, kwani anasimulia kwa umakini kama vile anayeongea ni mtu mzima, kumbe ni mtoto wa miaka nane tu.
Jacqueline anazidi kutokwa machozi, anakohoa kidogo kisha anaendelea kunisimulia,
"Leo hii ndio baba ame.... amenilalia na kuniingiza kwa nyuma."
Hapo akaanza kulia kwa uchungu sana, nikakosa namna ya kumbembeleza.
Kisha kwa sauti ya chini na kwa shida sana akaniambia maneno ya mwisho niende nikawaambie wazazi wake,
"Mama yangu, mwanao nakufa, najua sitapona. NI SAWA UMENIZAA, LAKINI UMEFUPISHA MAISHA YANGU. Mwambie na baba kuwa naenda kumwambia Mungu juu ya ubaya wote mlionifanyia"
Nurse mmoja alikuja kunitoa kwenye chumba alicholazwa Jacqueline akisubiri matibabu. Aliniambia PF3 imeshafika hivyo tunaomba utoke nje ili tuanze kumuhudumia.
Hazikupita hata dakika tatu nurse yuleyule alikuja kuniambia, mgonjwa wetu amepoteza maisha. Niliumia kupita kiasi kana kwamba mimi ndio baba halisi wa mtoto Jacqueline.
Dunia ina watu wa ajabu sana. Kuna mambo yanaumiza sana, lakini acha niishie hapa. Nashindwa kuendelea kuandika mengi zaidi kuhusu maisha ya mtoto Jacqueline.
Ni kweli watoto wengi katika jamii zetu wanapitia magumu kama haya. Jamii tushirikiane kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.
BILA SHAKA UMEVUTIWA NA STORY HII YENYE MAFUNZO, HIVYO NAOMBA KURA YAKO TAFADHALI.
______________________
Mwandishi: Mr. George Francis
Simu: 0713736006
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Upvote
11