Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Tangeni bila shaka[emoji16] siku ya jumapili wanashuka milimani kuja kugonga kitimoto
Nilipanda mlima uluguru nikakuta waluguru huko juu Tena wanavijiji vyao Hali ya hewa ilikuwa nzuri ila huduma za kijamii Hadi uteremke mlima, binafsi nilishuka miguu inatetemeka na maumivu makali mno. Mpaka Leo nawashangaa watu Kule wanavyoishi
 
Nenda Morogoro shuka msamvu, chukua bodaboda akupeleke hadi shule ya msingi kikundi, nauli 1500.
Ukifika pale angalia mlimani kule watu wamejenga mlimani yaani. Sasa unajiuliza hawa watu hata mabati walipelekaje kule!
 
kijiji cha tanganyika,kata ya masagati tarafa mlimba wilaya ya kilombero .nikipangiwa kule kituo cha kazi mwaka 1999 nikarudi kumshukuru DED kwa kazi.nikarudi zang Dar .aise Kule watu alikuwa wanaishi kama mazombie hakuna huduma ylza jamii hata moja hadi uende mlimba 150km Dahhh ila nasikia mambo siku hizi yamebadilika Luna kula kitu japo afadhari.
Mkuu uko ndiyo kwenye fursa ungewekeza kwenye ardhi
 
Kijiji cha Kitapi, kipo wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani. Kipindi nimehamishiwa kikazi nimekuta maji ni kuchota visima vifupi, barabara imefunikwa na manyasi, hakuna mtandao wa simu hadi upande kwenye miti, nyumba zipo mbalimbali na zipo msitu, huduma ya soko ni kuanzia saa kumi Jioni hadi saa kumi na mbili jioni mchana watu wapo shamba, giza linaanza saa kumi na moja jioni kwa sababu ya msitu mnene, hakuna bodaboda zaidi ya zinazokuja na kutoka, mvua ikinyesha hakuna safari tena sababu ya utelezi na matope, husikii muungurumo wa gari kwa sababu gari pekee ni wakati wa mitihani ya darasa la saba.
Tusilaumu Serikali kununua V8
 
Habari za muda huu wanajf.

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji Cha Baranga kata ya sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndo kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu , jua kali ndo kwao, vurugu Sasa ndo chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafikina timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa Sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa namgogoro wa mpaka wa shamba Kati ya ukoo na uko huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu Nini?
Katikati ya mpanda na kigoma kuna pori wanauza chakula
 
Vijiji vya Vunta na Kidunda, Hedaru, wilaya ya Same.

Ni vijiji vilivyo milimani - ktk Safu ya milima ya Usambara.
Ukitokea Mombo, kabla ya kufika Hedaru, unakata kulia na kuanza songombingo la kupanda mlima kuelekea vijiji hivi.
Issue hapa ni barabara ya vumbi yenye slope kubwa ajabu! Dereva akifanya kosa kidogo tu, mmekwisha kwani gari litaserereka bondeni takribani mita 600 - 800 hadi litakapogonga mwamba na kusimama! Bila gari imara lenye 4-W, huwezi kwenda kule.
Wakati wa kurudi toka Vunta, nilimuuliza mwenyeji wangu kuwa kwanini hawa Wapare waliamua kwenda kuishi sehemu hatarishi kama zile? Aliniambia kuwa, Wapare walikimbilia kwenda kule kwa ajili ya maficho kutokana na vita kati yao na maadui zao pamoja na maasidi wao - Wachagga. Ilikuwa zamani sana kabla ya ujio wa Wakoloni.
Baadaye waliweka makazi mpaka leo.
 
Back
Top Bottom