Ni Taarifa gani nzuri au kitu kizuri ulishawahi kuipata/kupata ukamshukuru Mungu/Mwenyezi Mungu?

Ni Taarifa gani nzuri au kitu kizuri ulishawahi kuipata/kupata ukamshukuru Mungu/Mwenyezi Mungu?

Kuna taarifa nyingi ziliniacha na furaha kubwa kwani mengi sikuwahi hata kumuomba Mungu wala kuwazia kuwa nastahili.
Moja nilipofaulu form 6, nikiwa private candidate baada ya kushindwa kwenda shule kwa kukosa ada na nauli tu. Nikajiunga UDSM, nikapata shida kubwa(sitaki hata kukumbuka), hata sijui ilikuwaje nikamaliza Chuo, ukiniuliza siwezi hata kukumbuka ilikuwaje nikamaliza Chuo.
Ajabu la pili hata niliite ajabu, kabla ya wiki 1 kwa UE mwaka wa mwisho nikampoteza Mama yangu kipenzi, huyu ndio tumaini langu pekee lililokuwa limebaki ukiachia Mungu. Ilikuwa ngumu kurudi kufanya UE, ila nikarudi Chuo nikaingia kwenye paper nikijua nakamilisha idadi tu ya wanaotarajia kumaliza Chuo ila sitoboi.
Baada ya paper, nikarejea kijijin kwetu ili nikajipange kwenda kuripoti Ukerewe ambako nilipangiwa kwenda kama Mwalimu...Kwa wale wa 2009 wanajua tulikuwa tukipangiwa vituo hata kabla ya matokeo ya mwisho kama sikosei. Kabla sijaondoka nikapigiwa simu na rafiki yangu akaniambia kuna shirika wanatafuta Walimu, nikataka kumpotezea kwani nilijua hata GPA yangu haitakuwa kivutio. Ila jamaa alinisihi mno, kwani anajua uwezo wangu pamoja na muda mwingi kutoutumia darasani ila kwenye presentation aliona kitu kwangu.
Baada ya kufika Dar tu nikaulizwa nina passport ya kusafiria? Nikashangaa, nikapewa mtu pale uhamiaji akanifanyia utaratibu nikapata passport kesho yake nikaikabidhi kwa mhusika. Bila kuambiwa kitu, nikapelekwa Mikocheni nikawakuta wenzangu 7 tukawa 8.
Taarifa ikawa tunasafiri week ijayo kwenda nje kwa wiki 2 kujifunza mambo(nchi nitaihifadhi). Hapo niliamini Mungu ni mwenye huruma sana.
Nilirudi nikapewa ajira kwakweli sikuwahi kuamini kama nilistahili, ila ninachokiamini nilikuwa na uwezo mkubwa mazingira tu ndio yalikuwa magumu. Niliitendea haki kazi niliyopewa.
Nilizunguka Duniani mpaka mwaka 2016 hapo ndio nilipata jaribu la maisha tena, nikiwa safarini nilipata ajali mbaya iliyopelekea mauti ya Mama wawili niliowapa lifti tu(RIP Wamama ), Nikapoteza matumaini tena, sikiweza kwenda kazini tena, pamoja na kupewa muda ila nilikuwa kama mtu aliyerukwa na akili.
Mwaka 2017 nikajaribu kuomba program fulani US, siku nilipopata Email na simu ya kuwa shortlisted nikakumbuka Mungu ananipenda mno kwani niliamini labda sina sifa na watu niliokutana nao kwenye interview niliamini wananizidi kuanzia matokeo ya darasani, Nikafanikiwa na kuwa finalist, ila ikawa nifanye TOEFL then tusubirie zaid ya miezi 5 mbele kujua nani na nani wataenda.
Nikaanza kula msoto, nikapoteza hata marafiki na ndugu mbona ukisikia kufulia ndio huko. Hili jambo sikumuambia mtu yoyote yule zaidi, kwahiyo aliyekuwa anajua ni wale finalist wenzangu tu ambao tumejuana tulipofikia hatua hiyo. So hakuna mtu anajua nasubiria bahat ya kutimkia US.
Ilipofika mwezi wa 9, natoka zangu kuswali, ile kuwasha simu nakutana na Email ilibidi niswali Sunna kwanza labda sijaona vizur, hatimae mimi ni miongoni mwa wanaoenda US...
Nini nataka kusema?? Kila gumu lina suluhisho mbele ya Mungu, katika taarifa nzuri nilizowahi kupokea, 90%sijawahi kutegemea wala kumuomba Mungu.
Mkuu hii shuhuda imenisikitisha na kufurahisha, yote kwa yote Mungu ni mwema nyakati zote(kulia na kucheka).
 
Katika siku nilizofurahi sana maishani mwangu basi ile ilikuwa ya kwanza,

Matokeo ya form 4 yametoka nimefaulu kwa daraja la kwanza peke yangu hapo shuleni lakini zaidi ya yote nilikuwa na ufaulu mkubwa kuliko mwanafunzi yeyote kwenye kata yangu. Atakaehisi ni chai au promo naomba aje PM ajionee
 
Advance pia tulikuwa na joint exams, nilibahatika kuwa mwanafunzi mwenye wastani mkubwa lakini division ya kawaida kwa wanafunzi wote wa michepuo ya Sayansi. Basi nikawa na vimba bichwaa kinoma.

God was/is indeed good
 
Katika siku nilizofurahi sana maishani mwangu basi ile ilikuwa ya kwanza,

Matokeo ya form 4 yametoka nimefaulu kwa daraja la kwanza peke yangu hapo shuleni lakini zaidi ya yote nilikuwa na ufaulu mkubwa kuliko mwanafunzi yeyote kwenye kata yangu. Atakaehisi ni chai au promo naomba aje PM ajionee
Kipanga mwenyewe, safi sana mkuu
 
Hello wakuu,
Habari ya weekend, hivi ni taarifa gani nzuri ulishawahi kupata ukaishia kumshukuru Muumba, Mimi nakumbuka kwenye matokeo ya std 7 st Kayumba, nilichaguliwa kidato cha kwanza kwenda boarding school, na mtaani kwetu ilikua ukifaulia mbali kidogo au boarding unaonekana noma,sasa nakumbuka darasani kwetu niliwawakilisha kwenda hako kaboarding school, sijui hata ilikuaje maana sikua kipanga hivo ukilinganisha na wengine🙏 nauli from home to hiyo shule ilikua TZS 500 tu kwa daladala au unaweza kutembea kwa miguu tu😂😂 ila furaha yake si mchezo.

Baada ya kumaliza chuo, msoto kidogo mtaani(broke), huku nikipambana na interviews na kusambaza CVs, interviews zingine nyingi tu nilikua nafeli🤭 nakumbuka siku niliyopigiwa simu kwamba, umepata kazi uje kucheki mkataba, Aisee nilijiskia vizuri mno.

Ni mengi mazuri Muumba ametutendea, ila karibu ushare na sisi lolote utakalojisikia.
Happy week ending wote.
Sasa hizi zote zitakuwa cha mtoto siku mshenga wako nakamilisha lile jambo letu la wewe kuitwa mrs ........🤣🤣🤣🤣
 
Kuna taarifa nyingi ziliniacha na furaha kubwa kwani mengi sikuwahi hata kumuomba Mungu wala kuwazia kuwa nastahili.
Moja nilipofaulu form 6, nikiwa private candidate baada ya kushindwa kwenda shule kwa kukosa ada na nauli tu. Nikajiunga UDSM, nikapata shida kubwa(sitaki hata kukumbuka), hata sijui ilikuwaje nikamaliza Chuo, ukiniuliza siwezi hata kukumbuka ilikuwaje nikamaliza Chuo.
Ajabu la pili hata niliite ajabu, kabla ya wiki 1 kwa UE mwaka wa mwisho nikampoteza Mama yangu kipenzi, huyu ndio tumaini langu pekee lililokuwa limebaki ukiachia Mungu. Ilikuwa ngumu kurudi kufanya UE, ila nikarudi Chuo nikaingia kwenye paper nikijua nakamilisha idadi tu ya wanaotarajia kumaliza Chuo ila sitoboi.
Baada ya paper, nikarejea kijijin kwetu ili nikajipange kwenda kuripoti Ukerewe ambako nilipangiwa kwenda kama Mwalimu...Kwa wale wa 2009 wanajua tulikuwa tukipangiwa vituo hata kabla ya matokeo ya mwisho kama sikosei. Kabla sijaondoka nikapigiwa simu na rafiki yangu akaniambia kuna shirika wanatafuta Walimu, nikataka kumpotezea kwani nilijua hata GPA yangu haitakuwa kivutio. Ila jamaa alinisihi mno, kwani anajua uwezo wangu pamoja na muda mwingi kutoutumia darasani ila kwenye presentation aliona kitu kwangu.
Baada ya kufika Dar tu nikaulizwa nina passport ya kusafiria? Nikashangaa, nikapewa mtu pale uhamiaji akanifanyia utaratibu nikapata passport kesho yake nikaikabidhi kwa mhusika. Bila kuambiwa kitu, nikapelekwa Mikocheni nikawakuta wenzangu 7 tukawa 8.
Taarifa ikawa tunasafiri week ijayo kwenda nje kwa wiki 2 kujifunza mambo(nchi nitaihifadhi). Hapo niliamini Mungu ni mwenye huruma sana.
Nilirudi nikapewa ajira kwakweli sikuwahi kuamini kama nilistahili, ila ninachokiamini nilikuwa na uwezo mkubwa mazingira tu ndio yalikuwa magumu. Niliitendea haki kazi niliyopewa.
Nilizunguka Duniani mpaka mwaka 2016 hapo ndio nilipata jaribu la maisha tena, nikiwa safarini nilipata ajali mbaya iliyopelekea mauti ya Mama wawili niliowapa lifti tu(RIP Wamama ), Nikapoteza matumaini tena, sikiweza kwenda kazini tena, pamoja na kupewa muda ila nilikuwa kama mtu aliyerukwa na akili.
Mwaka 2017 nikajaribu kuomba program fulani US, siku nilipopata Email na simu ya kuwa shortlisted nikakumbuka Mungu ananipenda mno kwani niliamini labda sina sifa na watu niliokutana nao kwenye interview niliamini wananizidi kuanzia matokeo ya darasani, Nikafanikiwa na kuwa finalist, ila ikawa nifanye TOEFL then tusubirie zaid ya miezi 5 mbele kujua nani na nani wataenda.
Nikaanza kula msoto, nikapoteza hata marafiki na ndugu mbona ukisikia kufulia ndio huko. Hili jambo sikumuambia mtu yoyote yule zaidi, kwahiyo aliyekuwa anajua ni wale finalist wenzangu tu ambao tumejuana tulipofikia hatua hiyo. So hakuna mtu anajua nasubiria bahat ya kutimkia US.
Ilipofika mwezi wa 9, natoka zangu kuswali, ile kuwasha simu nakutana na Email ilibidi niswali Sunna kwanza labda sijaona vizur, hatimae mimi ni miongoni mwa wanaoenda US...
Nini nataka kusema?? Kila gumu lina suluhisho mbele ya Mungu, katika taarifa nzuri nilizowahi kupokea, 90%sijawahi kutegemea wala kumuomba Mungu.
Nanukuu

"Ila ninachoamini nilikuwa na uwezo mkubwa Ila mazingira Tu ndo yalikuwa magumu"

...."katika taarifa nzuri nilizowahi kupokea 90% sijawahi kutegemea Wala kumuomba Mungu."

Naam.
 
Mimi KAZI yangu ya kwanza badala ya kuwa na furaha nilijawa stress ilikuwa hivi :

Mwezi mmoja kabla ya kumaliza chuo nilifanya interview kwenye kampuni moja ya simu. Hadi namaliza chuo hawakuwahi kunitafuta.

Nilivyokuwa mtaani na harakati za kusambaza CV nikapata KAZI ya kujitolea kwenye NGO moja mikocheni Ila walikuwa wananipa pesa ndogo za kujikimu. Nilipiga pale kujitolea kama miezi 6. Baada ya hiyo miezi 6 nikapewa pre-contract kuwa nitaajiriwa rasmi baada ya miezi miwili ijayo huo mkataba haukuainisha mshahara utakuwa shilingi ngapi Ila nilikuwa najua mishahara ya pale. Mwanaume nikasaini nikaendelea Kula Hela zangu za nauli na kujikimu.

Baada ya wiki tatu toka nisaini ule mkataba WA awali WA kuajiriwa nikapigiwa simu na Ile kampuni ya simu kuwa nikaanze KAZI kesho yake haraka. Sitasahau Ile wiki nilikuwa na stress Sana tena Sana badala ya furaha.
Aisee!!
Hii case ni the same na yangu.

Ila Mimi zote ni Taasisi za serikali.
 
Sasa hizi zote zitakuwa cha mtoto siku mshenga wako nakamilisha lile jambo letu la wewe kuitwa mrs ........🤣🤣🤣🤣
Mshenga mwenyewe unatoa macho tu hadi mwaka unaisha tena😂😂.

I can't wait to be somebody's wife,a mother to his kids.🙏
 
Mshenga mwenyewe unatoa macho tu hadi mwaka unaisha tena😂😂.

I can't wait to be somebody's wife,a mother to his kids.🙏
Yaani huo mstari wa mwisho unanipa nguvu ya kukutafutia mume maana kweli unataka kuwa wife. Unanikumbusha mrembo Kelsea
Tena nae kapotea sijui kashapata kidume amemficha wikend hii sehemu
 
Kuendelea kuishi baada ya misukosuko ambayo kwa mtu mwingine angajitoa roho kabisa.

Kujaliwa moyo wa subira na uvumilivu
Hi Baba mwifa's Junior, katoto hakajambo? Pole na hongera kwa kulivuka hilo jaribu.
 
Yaani huo mstari wa mwisho unanipa nguvu ya kukutafutia mume maana kweli unataka kuwa wife. Unanikumbusha mrembo Kelsea
Tena nae kapotea sijui kashapata kidume amemficha wikend hii sehemu
Kwani naye Kelsea wewe ni mshenga? Hee 😂 tupo wengi kumbe
 
Yaani huo mstari wa mwisho unanipa nguvu ya kukutafutia mume maana kweli unataka kuwa wife. Unanikumbusha mrembo Kelsea
Tena nae kapotea sijui kashapata kidume amemficha wikend hii sehemu
Nipo, mambo?!
 
Nilivyochomoa third attempt baada ya kuihairisha mwaka wa pili kwa kujifanya nimezimia naumwa vibaya sana ili kuepuka retake maana probation ilikuwa nzito kama jiwe

Nikaja ifanya mwaka wa mwisho in September confrance hapo wenzangu wanavimba washa graduates mapema sisi wa sup tunasubiri matokeo Siku nafungua account nicheki tokeo hapo chuo kimeisha nakuta kitu kipo clear muhuni wa Manzese nina bachelor tayari

Nikaenda nunua kischana (konyagi ) kubwa nikaingia magheton nikajifungia
 
Back
Top Bottom