Ni tangazo lipi la biashara la TV au redio unalichukia/unalipenda?

Ni tangazo lipi la biashara la TV au redio unalichukia/unalipenda?

Matangazo yote ya Magodoro na matangazo yote yaliotaafsiriwa
 
Silipendi tangazo la chips snaksi, yule baba anaingia tu sebleni anaanza kumfokea house girl kala snacks za motto wakat kiuhalisia hata hakuona kama motto kadokolewa snaksi zake.

jingine la mpoki kuigiza kama Magu lile la 4G yan kaboa kinyama, though quality ya video nzuri but hajapatia ku act kama prezidaa

Nlilowah kulipenda ni lile la revola, mdada anulizwa tueleze siri ya mafanikio yako anajibu sio siri ni revola tu.....

jingine nlilipenda lile la zaman la tigo thumni, majamaa yamevaa kama watu wa mwaka 47 halaf wanaimba

jingine la redio lile la CRDB, wanaimba 'tusherekee mafanikio yetu, miaka 20 ya ubunifu wetu, bonge la nyimbo yani.

jingine cjui ni Barnaba yule anaimba namba za masafa ya redio one kila mkoa, ''cjui 91. 4 songeaaa, 97.8 kigomaaa this is radio one'', n.k,,,,n.k. kanyimbo katamu sana

lile la tigo la kuchanganyikiwa na mwanzo wa mwaka yani wanajmvi mnapoishia chuki zenu me ndo naanzia hapo, limenifika hapaaaa.....walitaka kumgeza yule baba alohojiwa na haki elimu akajibu vitu vya ajabu kule mtwara bt madaktari wakasema ule ni ugonjwa gani sijui jina lake limenitoka.

Coca cola na unillever (ommo, royco, blue band, n.k) ya Kenya nawakubali sana.
 
My best ever tv advert.....Honda the Cog
Lipo you.tube natumia simu nimeshindwa kuliweka hapa.
 
Silipendi tangazo la chips snaksi, yule baba anaingia tu sebleni anaanza kumfokea house girl kala snacks za motto wakat kiuhalisia hata hakuona kama motto kadokolewa snaksi zake.

jingine la mpoki kuigiza kama Magu lile la 4G yan kaboa kinyama, though quality ya video nzuri but hajapatia ku act kama prezidaa

Nlilowah kulipenda ni lile la revola, mdada anulizwa tueleze siri ya mafanikio yako anajibu sio siri ni revola tu.....

jingine nlilipenda lile la zaman la tigo thumni, majamaa yamevaa kama watu wa mwaka 47 halaf wanaimba

jingine la redio lile la CRDB, wanaimba 'tusherekee mafanikio yetu, miaka 20 ya ubunifu wetu, bonge la nyimbo yani.

jingine cjui ni Barnaba yule anaimba namba za masafa ya redio one kila mkoa, ''cjui 91. 4 songeaaa, 97.8 kigomaaa this is radio one'', n.k,,,,n.k. kanyimbo katamu sana

lile la tigo la kuchanganyikiwa na mwanzo wa mwaka yani wanajmvi mnapoishia chuki zenu me ndo naanzia hapo, limenifika hapaaaa.....walitaka kumgeza yule baba alohojiwa na haki elimu akajibu vitu vya ajabu kule mtwara bt madaktari wakasema ule ni ugonjwa gani sijui jina lake limenitoka.

Coca cola na unillever (ommo, royco, blue band, n.k) ya Kenya nawakubali sana.
Safi kabisa umenena vyema Yan mulemule
 
Tangazo la pilsner ice la sauti ya simba na nyau silipendi, kwanza linahamasisha ulevi na pili bia yenyewe low quality kama mataptap..

Tangazo la salama condoms la kitambo kama jamaa anamkinga mkewe na koti kwenye mvua ndo nalipenda..
 
Tangazo linalonipaga uchungu ni lile la ticha anatoka home nyumba mbavu za mbwa kisha anaenda skul watoto wamekaa hadi ubaoni huku wengine wamwkalia dawati ambalo wao ndo kama wanalibalance kisha wanasukumana mpaka chini.. Dah
 
Nachukia lile tangazo la timiza
Eti mi nimekopa zaidi ya laki
Sita sijui nimenunua vifaa vya bandi yangu
Kisha yule jamaa anaanza kuimba imba

Timiza timiza, yani likipita tu nahama kabisa hiyo channel
Naunga mkono hoja yako mkuu, hata mm nalichukia kupita kiasi yan
 
Kweli kbs. Tangazo hovyo sana. Halina ubunifu wowote. Kuna na lile jingine la profesa chapati, yani buree kabisaaa!!.
Tangazo bora ni lile la Coca Cola la wale machali wawili, mtu na mdogo wake.. boooonge la tangazo asee. Mi mpaka nimeli download kwenye simu yangu
Nigga you need a brother figure......you got brother issues



Downloading a commercial psshh SMH
 
matangazo yote ya sabuni za unga
nayachukia sana kwa uongo uliopitiliza
halafu kuna lile la godoro host ni monalisa
na matangazo yote ya coca-cola sio kama mabaya yanapata air time ya kutosha mpaka yanakera
by the way for me coca-cola ndiyo kampuni inayotengeneza matangazo mazuri kupita kampuni yoyote ile duniani
Hahaha usiseme duniani na hujawah kuona tangazo la budweiser au mountain dew au apple......
 
Kuna tangazo la lake oil jamaa ni anapiga kelele kinoma...lile tangazo silipendi yaani kila nikilisikia kichwa kinauma
 
nilikuwa nayapenda sana matangazo ya "" Haki Elimuuu"' mfano lile la '' alright student - ah students'' Mengine yale ya Fataki, yaani nilikuwa nayapenda ; kuna tangazo moja Fataki anajifanya anajua sana kucheza bao '' eti yuko leo nakutwanga , cheza cheza sasa , cheza ! afu jamaa anamwambia ' tulishakustukia fatakiiii, hapa nia yetu tukupotezee tu kusubiri wanafunzi wa kike, afu lifataki linaondoka linalaumu; kazi kuharibia dili za wenzenu, lingine nalolipenda lile la Redio one - Haijalishi uko pande gani , kitaani ama nyumbani kipindi kiko hewani sikiliza... nisiyoyapenda yako kibao, moja ni lile la joti la tigo, sijui lulu anasema babu mi nilitaka ujibu swali la archmedes principle , silipendi
Huyo binti anaonekana shankupe fulani eti ....."Nisaidie homwork, nyambaff
 
Habar wadau,
Sanaa ya utengenezaji matangazo ya biashara Sasa hv imekua Sana na hata nchini kwetu si haba imeboreka Sana. Zamani matangazo ya biashara katika TV au redio ilikuwa ni kero kubwa kutokana na mengi kujali tu kuitangaza biashara husika Bila kumfanya msikilizaji kulipenda tangazo lenyewe

Kwa nchi za wenzetu matangazo haya huwa wanayajali Sana kiasi cha kuhakikisha yanavutia mno, Kwa wale watumiaji wa ving'amuz mtakuwa mnaona station za nje zilivyo na matangazo ya biashara ya kuvutia,mfano ukiwa unaangalia mpira Kwa supersports kabla ya mpira kuanza au halftime huwa Kuna matangazo ya biashara lakini yanavutia mno kiasi kwamba huwa ni sehemu ya burudani kuyatazama na huachoki.

Binafsi hapa Tanzania Kuna matangazo huwa siyapend balaa,mfano Kuna lile la timiza,yupo jamaa flan kashika gitaa kavaa viatu vya ajabu anaimba timiza timiza timiza ni mkombozi,silipendi kwelkwel,jingine la benk flan ni la redio yupo jamaa anaulizwa vitu na Dada flan yeye anajibu tofauti kama amechanganyikiwa,lengo la tangazo lilikuwa ni kulifanya lichekeshe lakini Kwa kuwa mwanaume yule anaongea Kwa kusoma skripti limekuwa baya tu,

Zaman clouds walikuwa na jamaa anayeigiza kikurya ktk matangazo ya redio niliyapenda Sana na yalikuwa yanachekesha mno. Juzjuz kulikuwa na tangazo la Tigopesa la mama wa nyumban yuko na mwanae mdogo yule mtoto siku anaanza kuongea anatamka ni tigopesa nililipenda Sana lile sikuwah kulichoka lakini limepotea ghafla, matangazo mengine nisiyoyapenda ni Yale ya mpoto dah siyapend kwelkwel.

Karibu mdau uchangie nawewe kuhusiana na tasnia hii ya matangazo ya biashara yapi yanakuboa na yapi unayapenda
49a560c81a72dd2754d45bc6bb2c6f1f.jpg
I hate this yaan huwa nazima tv ama kuhamisha chanel
 
Kuna moja la zamani la ukimwi nilikua nalipenda sana.watu wanataja majina yao (kama kujitambulisha)..mimi naitwa george,mary,agness...alaf mwishoni wanamalizia kwa kusema huwezi jua kati ya hao waliojitambulisha ni nani mwenye ukimwi
Nalipenda sana hili tangazo
 
Back
Top Bottom