Elections 2015 Ni Tundu Lissu pekee(Sababu moja sifa kumi)

Ni ukweli usiopingika nderingosha, meningitis kuwa kwa sasa watamzania tunapaswa kuangalia shida kuu zinazotufanya tudorore na kuwa hapa. Nionavyo mimi miongoni mwa matatizo yetu makubwa kwa sasa ni matumizi ya sheria. Katiba tuliyonayo ina mapungufu lakini mapungufu yanazidishwa na utawala wa kutotumia hata hicho kikamilifu kidogo kilichopo. Na tutambue kuwa nchi yeyote duniani ukisikia inaendelea cha mwanzo ni kujenga nidhamu ambayo mwangalizi na msimamizi mkuu ni SHERIA. Hivyo ni muda muafaka wa kuwa na kiongozi anayejua sheria na mkamilifu wa kuisimamia. Hata haya ya UFISADI, MIKATABA, MADAWA YA KULEVYA, UONEVU TOKA VYOMBO VYETU VYA ULINZI NA UALAMA, KUBAMBIKIANA KESI, N.K hata katiba tuliyonayo ingeweza kuyakabili kwa kiasi kikubwa tatizo ni MSIMAMIZI WA SHERIA.
Tatizo la pili ni muelekeo wa uchumi wetu. Baada ya sheria kuleta nidhamu, litaibuka la pili vipato vyetu vitufikishe wapi? Hapa linakuja suala la kuwa na kiongozi wa juu ambaye ni mzalendo na mchumi. Tanzania tuna rasilimali za kutosha, zikisimamiwa na mchumi mzuri zinaweza kutuletea maendeleo ndani ya muda mfupi sana. Chukulia upande wa mapato tunayopoteza kupitia mikataba katika sekta ya madini. Hii pekee ikisimamiwa inaweza kuongeza zaidi ya nusu ya bajeti ya nchi.
Kwa kusema hivyo ni muda muafaka wa UKAWA kujipanga na kutuletea kiongozi wa juu mathalani Rais mzuri ktk sheria (TL) na PM awe kiongozi mwenye msimamo thabiti (SLAA) na waziri atakayehusika na masuala ya uchumi / fedha / viwanda awe ni mchumi (Prof. Lipumba). Ushaur kwa sasa ni huo, kwa hizo nafasi chache za juu.




 
Last edited by a moderator:

japo sina mahaba sana na hicho chama ila huyu mjamaa tundu lissu hakika namkubali mno na ni mwanasiasa wa kizazi hiki ambaye yupo very competent na kubwa zaidi ana kitu cha ziada cha kuwa na akili sana ambazo pia anajua kuzitumia ipasavyo ila ktk suala la yeye kuwa rais hapa nadhani ndiyo nitapishana na wewe. kwa features zake za kibinadamu na kihaiba hawezi na hafai kuwa rais ila nikisikia tundu lissu ni waziri mkuu au waziri wa sheria na katiba au mshauri mkuu wa rais kwa masuala ya sheria nitamuunga mkono kwa asilimia zote 100%. hongereni chadema kwa kuwa na mtu kama tundu lissu na ninamkubali kwa kiasi kikubwa tu na namwomba asichoke kusema ukweli kwa watawala.
 
CHADEMA inahitaji mtu nje ya wabunge waliopo ndio agombee urais. Ushindi wa kiti cha Urais ni probability bila kujali uwezo au uzalendo wa mtu. Kumpoteza Lissu kwenye panel ya wabunge ni pengo kubwa kwa chama. Tumeona hilo Kwa kumpoteza Dr Slaa. Tusirudie makosa yale tena. Uhakika wa ushindi kwa Upinzani kwenye kiti cha urais ni 2020 na hii itategemea sana ongezeko la idadi ya wabunge 2015. Nafasi kubwa kwa sasa kwa upinzani ni kuongeza idadi ya wabunge. Maoni yangu Lissu akatetee jimbo lake. Ikitokea upinzani ukashinda kiti cha urais basi atakuwa na nafasi kubwa kuhudumia watanzania kwa nafasi ya uwaziri au AG
 
Dr.Slaa alisema Tundu Lissu ndani yake kuna Dr.Slaa kumi (10).
Maneno hayo aliyatamka Dr. Slaa mwenyewe wakati anaikosa nafasi ya kuwa mbunge mwaka 2010 .
 
namkubali sana tundu lisu .Anaweza tupeleka tunapotaka. yupo serious kweli na watanzania. Naomba ukawa wamupe nafas jamaa .
 
Kweli mkuu, anafaa sana kua AG

Kwenye nafasi ya AG Lissu anafit ila kwa mawazo yangu angefaa sana kwenye ile wizara ya nishati na migodi, kwani kwa umahili wake wa sheria na nasaba za kizalendo alizonazo angetusaidia sana kwenye mikataba mibovu.
 
...huna mahaba na chama anachotoka Lissu...na kwa maana hiyo huwezi kupenda yeye awe rais...maana akigombea urais TZ lazima atashinda..na hili ndilo linaloogopwa sana na watu wa ccm....maana Lissu anakubalika na kila mtu kwenye taifa hili.....Wengi wanatamani Lissu awe kiongozi wao...maana amedhihirisha hili si kwa maneno bali kwa vitendo...Woga wako kwa Lissu kugombea urais TZ hauna tofauti na uoga wa rais JK pale aliposema bora Slaa awe rais kuliko Lissu awe mbunge....
 
tundu ni zaid ya mwanasiasa ni zaid ya mwanaharakat kwa tanzania yetu ya leo,ambayo imejaa vioja na hata jk analitambua hilo, ni afadhar wana ccm {wabunge}30 wapotee ktk raman ya siasa kulko TUNDU maana anahtajka kwa nyakat za sasa.
 
Tundu lissu huyu jamaa namkubali sana tena sana. Hana mpinzani
 
Tundu lisu hana masters ana degree tu, pia hawezi wala hana sifa ya kuongoza nchi, amejaa matusi tu kichwani hafai kwa matumizi ya umma

We una matumizi yoyote ya umma? Au ni sehemu ya majizi yanayokwapua kutoka kwa umma? Lissu ni rais wa 5 wa Tz, jiandae kisaikolojia
 

We una uwezo upi? mropokaji ukimlinganisha na na nani? au hafai kuwa badala ya nani? mi naona anafaa ndani ya ukawa na ccm
 
Well said, tundu lisu ni mtendaji, hupaswi kugombea uraisi. Uraisi bado slaa anafaa kwasasa

Tundu lissu akitumika kama mtendaji katika serikali kutakuwa na ufanisi

Km una nia nzuri na mabadiliko ni hv: wote wanafaa lakini wote hawauziki sawa, so achana na huu wimbo
 

no comment.
 
Nafikiri Tundu Lissu angeendelea kuwa mbunge, uwezekano wa UKAWA kushinda sio mkubwa kiasi hicho, tuwe wakweli ila idadi ya wabunge lazima wataongeza, tena kubwa tu. Wajikite kwenye kuongeza idadi ya wabunge, upande wa urais asimamishwe yeyote ila si Tundu Lissu. Lissu inapendeza asimamishwe kama mgombea urais wakati uwezekano wa kuwa rais toka upinzani ni mkubwa. Endapo Lissu atagombea urais mwaka huu, na wakashindwa, ambayo nafikiri ndivyo itakavyokuwa, tutamkosa mtu kama huyu katika bunge ambalo nina uhakika litawaka moto zaidi. Tundu Lizzu agombee 2020 au 2025, atakuwa ameiva kabisaaa!! Kama ukawa watashinda mwaka huu, basi Tundu Lissu ateuliwe kama mwanasheria mkuu au waziri mkuu.
Tundu Lissu, tafadhari usigombee urais mwaka huu. Tunakuhitaji bungeni bado.
 

Dead wrong!hatuna muda mwingine wa kupoteza.acha woga
 
CHADEMA chukua tahadhari kwa mambo yanayoweza kuwagawa kwa kipindi hiki muhimu.
 
Ni heshima ya pekee ambayo anaendelea kujijengea mtumishi huyu wa wana singida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…