Ni Ubatili Mtupu Mpaka Basi!. CC ya CHADEMA ilipata wapi mamlaka?. Baraza Kuu halina mamlaka hiyo!. Je, inawezekana CHADEMA ni chama majanga ila?

Nilijua tu utakimbilia kwenye kichaka chako cha Karma, anyway, eti Wengine wameingizwa tuu ngachoka!!!!!
 
Jamaa ameamua tu kujiondoa ufahamu ndugu yangu
 
Hivi ni vita kati ccm na vyama vyenye nguvu na lengo ni kuvidhoofisha kwa hofu ya kupokonywa mamlaka.
Ccm walianza na NCCR, kisha CUF na sasa CHADEMA.
CHADEMA wamefuta katiba yao kisheria kwa nini wengine washupae kiasi hiki. Tuwaangalie sana hawa mamluki wa ccm wanaoshupaza mashingo.
 
Mwalimu na Mwanafunzi wake wote ni Vilaza
 
 
Pascal Mayalla Zitto aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu alifukuzwa kwa katiba hii hii.

View attachment 2226519
Kwa mantiki hii, Kamati Kuu ya Chadema haikuwa na mamlaka siyo ya kumfukuza Halima Mdee bali haikuwa na mamlaka hata ya kumsimamisha. Mamlaka hayo ni ya Baraza Kuu. Asante Mayala kwa kutufungua macho. Kilichofanywa juzi na Baraza ni kusikiliza rufaa ya akina Mdee na wala si kusikiliza shauri kama mamlaka ya nidhamu. Kamati kuu ilishaipora mamlaka hayo. Duuu chama ovyo kabisa!
 
Naheshimu unachosema, ila hujajibu swali langu la msingi. Je kati ya makundi hayo mawili nani alianza kutokufata na kuheshimu Katiba ya chama chao? Je ni wale ambao hawakufata taratibu za chama kujiteua kuwa wabunge wa upendeleo ama viongozi na mababraza ya chama yaliyowafukuza uanacha kwa kutokufata katiba na taratibu za chama?
 
Wanabodi,

Kama Chadema ndio chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, jee tunaupinzani wowote wa kweli ambao ni serious, capable, credible, na reliable, wenye the ability and the capabilities wa kuiondoa CCM madarakani?!.

Paskali
Tukio la Chadema la keshokutwa Jumatano, tarehe 8 Machi, linakwenda kui transforms Chadema into maturity.
Update
Hatimaye Chadema wameacha kushupaza shingo na wamekubali matokeo!, kwa kuufuata ushauri wa bandiko hili CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Nimepokea taarifa, hii kutokea twitwani Kisha nikasoma na bandiko hili humu JF Tundu Lissu: CHADEMA tumeanza kupokea Ruzuku

Chadema wameufuata ushauri wa bandiko hili, waneacha ujinga wa kujifanya hawayatambui matokeo ya uchaguzi wa 2020!, sasa wameacha kushupaza shingo, wameyatambua matokeo kimya kimya!, wamewasamehe mashujaa hawa kimya kimya msamaha ambao utatangazwa rasmi siku ya Jumatano tarehe 8 Machi na Mwenyekiti wa Chadema, mbele ya Rais Samia!.

Iliwa kusemwa kuwa hakuna mkate mgumu wowote mbele ya chai!, tayari Chadema imeisha anza kupokea ruzuku hivyo sasa ita survive!. Na ile kesi ya kina Halima Mdee na wale 19 iliyopo mahakamani itafutwa!.

Hongera sana Chadema, for doing the right thing!, mtabarikiwa, viongozi wenu watabarikiwa, chama chenu kitabarikiwa na Tanzania Itabarikiwa!.
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki CCM kwa kukubali reconciliation
Mungu ibariki Tanzania
Paskali
 
Paskali unanitia mashaka kwenye uelewa wako wa mambo, wewe ni mwanasheria lakini unakuwa kama mimi ambaye si mwanasheria na ninashaka tukija kwako kwa usuluhishi baada ya kugombana na mke wangu utanizabua makofi kwa kuwa legelege!
Paskali muungwana siku zote yuko tayari kwa usuluhishi na unapoingia kwenye suluhu hauangalii yaliyopita ndiyo sababu mzee Mandela pamoja na ukatili ulikithiri waliofanyiwa weusi hakuangalia hayo japo wewe ulimuona si mpigania haki wa kweli, alirambishwa asali! Kheri ya kuramba kwake asali leo Afrika Kusini iko ikiwa nchi imara yenye umoja. Kheri ya Chadema kuramba asali leo watanzania wote pamoja na usiowapenda wanahaki ya kujumuika wakati wowote, tulishuhudia mama akiwapungia mkono usiowapenda pale KIA mpaka Arusha mjini badala ya tuliyoyazoeya ya askari kurusha mabomu na risasi zilizomuua Akwilina huku hajui nini kilikuwa kinaendelea eneo lile la tukio! Paskali, muungwana huwa hafurahii kuona yeye anakumbatiwa akilishwa mvinyo huku wasio wa mamayake wakihenyeshwa kwa ukatili wa mama yake, nasikitika kuona uovu ule unaupenda huku kwako suluhu ni shubiri.
Kubali usikubali ukiingia kwenye suluhu ujue umeingia kwenye nipe nikupe, yaani utapoteza unachokipenda na utapewa usichokipenda, yaliyopita si ndwele tugange yajayo, wadharau lakini utu umerudi nchini.
 
Nimeisoma hukumu, 1. Mahakama zetu zinarudia makosa yale yale ya ukosefu wa kutenda haki kwa sababu ya legal technicalities, kuwa Mahakama haiwezi kutoa uamuzi wa kitu ambacho hakikuombwa!.
2. Wabunge hawa 19 wa Chadema, walivuliwa uanachama wao kinyume cha katiba ya JMT na kinyume cha haki kwa kutokusikilizwa, kinyume cha katiba ya Chadema kwa kukiuka sheria, taratibu na kanuni!.
3. Kikao cha CC ya Chadema, kilichowatimua kilikaa kama a kangaroo court na kutoa maamuzi ya kikangaroo!.
4. Katiba ya Chadema inasema mwanachama kabla hajafutwa uanachama, kwanza atatumiwa hati ya mashitaka kwa maandishi by despatch, kisha atapewa siku 14 za kujibu mashitaka. Chadema hawakuandaa hati zozote za mashitaka!. Hili Mahakama ilipaswa ilione!.
5. Baada ya watuhumiwa kupewa hati ya mashitaka, ndipo kikao cha CC kinaitishwa kama mamlaka ya nidhamu, kusoma majibu ya mashitaka, na ndipo kinawaita washikiwa na kuwasikiliza. Hili halikufanyika!.
6. Baada ya wabunge 19 wa Chadema kuapishwa, hapa Chadema waliposwa kufanya kitu kinachoitwa a due process ya nidhamu na sio zile Zimamoto za kikangaroo!. There was no emergency of whatsoever!. Mahakama ilipaswa ilione hili!.
7. Uthibitisho wa hakukuwa na any emergency ya kuitisha CC, ni the time taken, kuitisha kikao cha Baraza Kuu!.
8. Baada ya kuitishwa kikao cha Baraza Kuu, kitu cha kwanza kwa Baraza Kuu Chadema kuangalia ni uhalali wa kikao cha CC, pili jee katiba, sheria, taratibu na kanuni za mamlaka ya nidhamu ya Chadema zilifuatwa?.
8. CC ya Chadema ni mamlaka halali ya nidhamu ya wabunge wa Chadema, lakini CC ya Chadema sio mamlaka ya nidhamu ya Halima Mdee ambaye ni Mwenyekiti wa Bawacha!, Mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu!, CC ya Chadema ilipata wapi mamlaka ya kumtimua Halima Mdee?!. Kikao cha Baraza Kuu kilipaswa hili kukuona!.
9. Japo kikao cha Baraza Kuu Chadema kiliitishwa kihalali kama mamlaka ya rufaa ya wabunge wa Chadema, lakini kitendo cha kikao hicho kubariki uamuzi wa CC kuwatimua bila kufanya mapitio yoyote, ni uthibitisho wa Chadema bado ni chama kichanga, mfano kingechukua nchi ile 2015!, it would have been disastrous!.
10. Kitendo cha Baraza Kuu kubariki maamuzi ya kikangaroo ya CC ya Chadema, kilifanya niyaite maamuzi yale pia ni ya kikangaroo, na kitendo cha Mahakama Kuu kuyabari maamuzi ya kikangaroo, Mahakama Kuu yetu nayo has joined the team!.
A Way Forward
1. Kwa vile Mahakama imekubali kuwa Chadema imewatimua hao 19 kihalali, japo uamuzi wa Baraza Kuu umepinduliwa, sasa Chadema isikate tena rufaa, kupinga uamuzi huu, bali iitishe kikao cha Baraza Kuu, ASAP, kifanye a due process, hili la wabunge 19 liishe, wabunge hao 19 wavuliwe ubunge wao, Chadema wapeleke majina 19 mengine, wateuliwe waapishwe, tuwe na Bunge la vyama vingi!.

2. Chadema wakifanya tuu dillydalling kukaa rufaa, inakula kwao!. By the time rufaa inasikilizwa, ndipo kifuate kikao cha Baraza Kuu, I'm afraid the time left before the next election is too little too late, ikibaki muda wa chini ya miezi 12 kabla ya muda wa uhai wa Bunge kuisha, hakuna uchaguzi wowote wala uteuzi wowote wa wabunge wapya!.
3. Tena nashauri kikao hicho cha Baraza Kuu, pia sasa ndio kimtimue rasmi Halima Mdee, kwasababu ndio mamlaka yake ya nidhamu, kikifuatiwa Mkutano Mkuu kuthibitisha. Hapa najua changamoto ni fedha!, kule kwenye kile chungu, zilikopatikana zile fedha za kugharimia Baraza Kuu lile, kile chungu bado kipo, na zile fedha bado zipo, Chadema wakifanya kama walivyofanya, fedha za kugharimia kitagharimia vikao vyote viwili, zitatoka, na tena Chadema inaweza ku take advantage ya kupiga ndege wawili kwa jiwe moja kwa mtu kupumzishwa kwa heshima na dereva mpya kupatikana!.
Paskali.
 
Kaka hapo umechemka umeandika kihisia kwa chama chako!
 
Mbona CHADEMA ya wakati wa baba mkwe kilikuwa kipo sawa? Huyu mrithi aongee na mwasisi wa chama waone wapi wanakosea... hii mali ya urithi naona itapotea.
 

What exactly is your problem Mr Pascal Mayalla?

Mahakama imethibitisha kuwa CHADEMA walitekeleza wajibu wao accordingly ktk kulinda nidhamu ndani ya chama chao na kwa mujibu wa kanuni na taratibu zao za kichama + katiba ya JMT.

Mahakama imesema hawajakiuka haki yoyote ya hawa kina mama. Wao ndio aidha kwa makusudi au kwa jeuri tu walishindwa kutumia haki yao ya asili kwenda kujitetea kwa makosa yao. CHADEMA walifanya waliyopaswa kufanya kwa usahihi kabisa..

KWA HIYO;

Mimi moja kwa moja nakuona wewe ni "mnafiki" fulani hivi. Kwa sababu hapa hata hutetei HAKI kwa ujumla wake. Bali unatetea maslahi yako na tumbo lako tu.(niwie radhi kwa kutumia lugha hii. Hata hivyo huu ndio ukweli kukuhusu wewe nami nimeona lazima nikuambie)

Na nakuambia hivi kwa sababu ungekuwa kweli wewe Pascal Mayalla unatetea HAKI kwa ujumla wake, basi kwa sasa ulipaswa uongoze mjadala wa kwanini Bunge chini ya kiongozi wake mkuu Spika Dr Tulia Ackson na kabla ya hapo Job Ndugai halichukui hatua dhidi ya kinamama hawa kwa mujibu wa sheria na katiba ya JMT.

Najiuliza ni kwanini huwezi kuona kuwa tatizo na kiini cha tatizo hili kipo ndani ya CCM na serikali yake kiasi cha kufikia hatua ya katiba ya nchi kuvunjwa na kukiukwa waziwazi.?

Ni ujinga kudhani kuwa mambo haya chanzo chake ni CHADEMA na kuamua kuwa kipofu tu wa kuona matatizo ya nchi yalipo.

Ndugu yangu Pascal Mayalla, kuijadili CHADEMA kuhusu hawa kinamama kuwa hawakufanya hili au lile ni ujinga na upumbavu.

Kwa sababu, pamoja na mahakama kukaa na kuchelewesha maamuzi ya kesi hii kwa takribani miaka 2+ kwa makusudi tu ili kuchelewesha tu HAKI, lakini hatimaye imeamua japo kwa kujiumauma hivyo hivyo na ime justify kuwa, there's no problem na process yote kwa ujumla wake ktk kushughulukia nidhamu ya wanachama wake hawa kinamama.

So, Mr Pascal Mayalla, stop these nonsense. Na badala yake tujiulize ni kwanini Bunge chini ya Spika Dr Tulia Ackson wanakiuka katiba na sheria za nchi kwa kulinda uhalifu huu wa kisheria na kikatiba?

Dr Tulia Ackson (and before her was Job Ndugai) wanaulinda uhalifu huu kwa maslahi ya nani eti?
 
ZIKO WAPI PESA ALIZOTOA MZEE MUSTAPHA SABODO KWA AJILI YA UJENZI WA OFISI KUU YA CHADEMA?
Mkuu Renegade , mpaka jamaa huyu kachomoka hili swali halikuwahi kupata majibu!.
BILIONEA SABODO AFARIKI DUNIA..

Bilionea na Mchumi maarufu nchini, Mustafa Jaffer Sabodo amefariki Dunia leo alfajiri akiwa nyumbani kwakwe, Masaki jijini Dar es Salaam.

"Mzee amefariki leo alfajiri akiwa nyumbani. Taratibu za mazishi zinaendelea na atazikwa katika makaburi yaliyoko mtaa wa Bibi Titi Mohamedi karibu na CBE," amesema Danstan.

Marehemu Sabado alizaliwa mkoani Lindi na alikuwa akifanya biashara katika nchi za Ufaransa, India, Kenya, Sudan, Nigeria, Zimbabwe na Tanzania.

Atakumbukwa kwa mchango wake ulioanzisha Mwalimu Nyerere Foundation National Lottery alipotoa msaada wa Sh milioni 800. Alihusika katika utoaji wa misaada kadhaa iliyohusisha kilimo, ujenzi wa visima na kusaidia wenye uhitaji.
Sabodo atazikwa leo saa 4:30 usiku.
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un.
“We surely belong to Allah and to Him we shall return”
"Sisi sote ni wa Mola, na kwake tutarejea".

Paskali pia anakuaga!.
RIP Jaffar Sabodo.
 P
 
R.I.P Mustapha Sabodo, hakika alikuwa mzalendo wa kweli, katika mazingira magumu akiwa kama mfanyabiashara bila kuogopa hatima yake na chama cha CCM kikiwa kimeshika hatima ya serikali alikubali kuisaidia CHADEMA pasi na kuogopa hatima yake.
 
Wanabodi,

Kama Chadema ndio chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, je tunaupinzani wowote wa kweli ambao ni serious, capable, credible, na reliable, wenye the ability and the capabilities wa kuiondoa CCM madarakani?!.

Paskali
huu ubatili Chadema waliufanya kuwatimua hawa mashujaa 19 bila ushahidi wa jinai ya kughushi,utakuja kuigharimu Chadema!
Msikilize JJ Mnyika akijibu hoja zangu kuhusu forgery,kisha msikie Mhe。Ester Bulaya akizumzia uteuzi wao
Mhe。Bulaya amethibitisha hakuna jinai ndio maana Chadema hawajashitaki polisi!。

Ila mimi mwenzenu jamani, ni binadamu tuu, huyu mdada,sio tuu namkubali sana kichizi,bali kiukweli,pia nina 。。。,,na hakuna kosa lolote,kwa mtu yoyote,kum。。。 mtu mwingine yeyote,kwa sababu yoyote,au hata bila sababu yoyote, naomba nisimalizie!,, ila nimeanza kumzimikia long time ago toka yuko CCM Mbunge wa CCM, Esta Bulaya, ni mbunge pekee aliyesaini petition ya Zitto ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu! Chadema ikomppteza itakuwa imepoteza kitu kikubwa,na wasipoamua mapema kuwasamehe,hawa watatu,Halima Mdee,Ester Bulaya na Ester Matiko,watagombewa kama mpira wa kona na majimbo yao,wakosimama kupitia chama chochote,wana tusua!。
P
 
P kuanguka kwa kambi yako sasa unanunua maadui wapya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…