Ni vipi Mungu anahusika kuwaleta duniani watu wanaozaliwa na ulemavu unaofanya maisha yao kuwa Jehanamu, Ni baraka yake kuwa hivyo ?

Ni vipi Mungu anahusika kuwaleta duniani watu wanaozaliwa na ulemavu unaofanya maisha yao kuwa Jehanamu, Ni baraka yake kuwa hivyo ?

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Nimechoka na majibu ya mkato kwamba mambo ya Mungu tumwachie Mungu mwenyewe, hili jibu haliwezi kamwe kutosha kwa maisha magumu wanayopitia walemavu, Ufafanuzi unahitajika !!

Wanasema kila kitu ni utukufu wa Mungu, watu wote wanaozaliwa wameumbwa kwa baraka yake, Kwa walemavu je ni baraka kwa magumu wanayoyapitia kiasi cha kuifanya dunia kuwa jehanamu kwao?

Nayaongea haya kwa uhalisia na wala si kiburi cha uzima, watu hawa wanateseka sana hapa duniani, Wenye hali hizi waliofanikiwa kiuchumi wapo ila ni wa kuhesabika na jihudi walizotumia laiti wangekuwa wazima basi wangefanikiwa mara 10 zaidi.

Mtu anazaliwa haoni, yani hata kusoma Biblia / Koran hawezi

Mtu anazaliwa hasikii, hata kwenda kanisani / Msikitini haambulii kitu

Mtua nazaliwa na ulemavu wa akili, ni changamoto

Mtu anazaliwa haoni wala hasikii, hapa hawezi kujifunza chochote maana njia zote za kupokea ujumbe zimezibwa

Mtu kazaliwa na magonjwa yenye maumivu makali / maisha yake ni maumivu tu
 
Wafia Dini mkuje hapa mtoe neno, na nafsi ya OP ipate kupona.
 
Mtu kuzaliwa maskini anaweza tumia nguvu ama bidii yake kujikomboa ila kwa walemavu hali huwa ni tofauti sana ?

Nashangaa sana hii ishu na ninaomba nifafanuliwe, Mungu anahusika na je ni baraka kuzaliwa hivi kwa mtu / mnyama ambae anaingia duniani bila hata dhambi ?

Walemavu ni wengi sana ila ni vile kwasababu inakuwa ngumu kwao kutoka ndio maana hata tunaowaona ni wachache,


Mtu anazaliwa haoni, hata biblia / koran kusoma ni ngumu

Mtu anazaliwa hasikii, hata neno la Mungu kanisani / msikini hawezi kusikia tena

Mtu anazaliwa haoni wala hasikii / yani hapa hawezi kufundishwa chochote

Mtu kazaliwa na magonjwa yenye maumivu makali / maisha yake ni maumivu tu
Mambo ya Mungu ni mastori tu!
 
Mtu kuzaliwa maskini anaweza tumia nguvu ama bidii yake kujikomboa ila kwa walemavu hali huwa ni tofauti sana ?

Nashangaa sana hii ishu na ninaomba nifafanuliwe, Mungu anahusika na je ni baraka kuzaliwa hivi kwa mtu / mnyama ambae anaingia duniani bila hata dhambi ?

Walemavu ni wengi sana ila ni vile kwasababu inakuwa ngumu kwao kutoka ndio maana hata tunaowaona ni wachache,

Nayaongea haya kwa uhalisia na wala si kiburi cha uzima

Mtu anazaliwa haoni, hata biblia / koran kusoma ni ngumu,

Mtu anazaliwa hasikii, hata neno la Mungu kanisani / msikini hawezi kusikia tena

Mtu anazaliwa haoni wala hasikii / yani hapa hawezi kufundishwa chochote

Mtu kazaliwa na magonjwa yenye maumivu makali / maisha yake ni maumivu tu
Dunia yenye walemavu iko logically consistent na dunia ambayo haijaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Mungu huyo, angalau kidhana, ana upendo na rehema kubwa sana kiasi kwamba asingeumba dunia ambayo ulemavu unawezekana kuwepo.

Ukiona dunia ina ulemavu, huo ninushahidi Mungu huyo hayupo.

Ukishaelewa Mungu huyo hayupo, ulemavu unakuwa si tatizo, unakuwa kitu kinachotokea naturally tu, kwa sababu nature si lazima itoe matokeo mazuri na wala haijali.

Ukitaka kumuweka Mungu kama muumba wa dunia, habari za watu kuzaliwa walemavu, watoto kufa wachanga, na mabaya yote ya duniani, zinakuwekea contradiction kubwa sana kuhusu uwepo wa huyo Mungu.
 
Kwann huja jiuliza kuwa ni kwann kuna walemavu walio fanikiwa kuliko ww mwenye viungo vyote?
 
Kwann huja jiuliza kuwa ni kwann kuna walemavu walio fanikiwa kuliko ww mwenye viungo vyote?
Wapo lakini ni wachache sanaaaaa!!!

Na bidii waliyotumia laiti wangekuwa ni wazima basi ingekuwa ni mara kumi.

Ni kama vile Mo au Bakhresa wangekuwa na ulemavu wangeweza kufanikiwa ila sio katika level walizofikia wakiwa wazima
 
Wewe huwa unawaza hivyo Kwa upande wako lakini Mim huwa nawaza hivi kama kwenye jamii ya kawaida watoto wenye ulemavu wanazaliwa wengi Tu,kwanini katika jamii za kimasai watoto wa namna hii huwa hawapo,
Huw nawaza sana
 
Wewe huwa unawaza hivyo Kwa upande wako lakini Mim huwa nawaza hivi kama kwenye jamii ya kawaida watoto wenye ulemavu wanazaliwa wengi Tu,kwanini katika jamii za kimasai watoto wa namna hii huwa hawapo,
Huw nawaza sana
Wanawaua
 
Wewe huwa unawaza hivyo Kwa upande wako lakini Mim huwa nawaza hivi kama kwenye jamii ya kawaida watoto wenye ulemavu wanazaliwa wengi Tu,kwanini katika jamii za kimasai watoto wa namna hii huwa hawapo,
Huw nawaza sana
Karibu kila Kabila zamani hata kwa wazungu, tamaduni zilikuwa ni Kuwaona wenye ulemavu ni mkosi hivyo zilitumika njia za kuwapoteza.

Dunia ya sasa imeelimika
 
Duuh ni sahihi kweli hii na kama si sahihi kwanini uovu huu haukemewi hadharani
Huwa ni siri za familia hizo na ni kimya kimya.

Hii ilikuwa ni tamaduni za zamani si kwa waafrika wala wazungu wala waarabu, Mtoto akizaliwa na ulemavu waliona ni mkosi unaohitaji kuondolewa.

Kwa sasa dunia walau imestaarabika
 
Mungu Anatuonesha utukufu wake kk viumbe wake ya KwaMBA yeye ndiye mkamilifu,na wewe unae jiona mkamilifu angeweza kukuumba ukawa mlemavu na mlemavu akawa mzima.
Hivyo ukamilifu ni wake Mungu pekee.
 
Back
Top Bottom