Ni vipi Mungu anahusika kuwaleta duniani watu wanaozaliwa na ulemavu unaofanya maisha yao kuwa Jehanamu, Ni baraka yake kuwa hivyo ?

Ni vipi Mungu anahusika kuwaleta duniani watu wanaozaliwa na ulemavu unaofanya maisha yao kuwa Jehanamu, Ni baraka yake kuwa hivyo ?

Kwani unafikiri alishindwa kutuwekea akili au kutukontrol tukawa ni watakatifu Tu .
Hapana
Mungu ametuacha hivi tulivyo ili Sisi wenyewe Kwa akili zetu timamu tutambue ukuu wake na kumuabudu.
Ukielewa KAZI ya shetani utajua ni kwanini unauliza maswali hayo.
 
Alishindwaje kuumba hizo species zenye kumtii yeye tu na zenye kufanya mema tu,

Badala yake Kaumba species zenye kufanya mema na maovu kwa wakati mmoja na yeye hutaka mema tu?????

Anaweza yote kweli huyo Mungu???
Free will, ukiamua kufanya kizuri unafanya na ukiamua kufanya kibaya huzuiwi.

Ila bado tunarudi pale pale kuhusu suala la walemavu ni mzozo
 
Hakuna kitu katiri duniani Kama mungu, chunguza maisha ya wanyama mbugani utaniambia,

Hakuna kitu yenye roho mbaya duniani Kama mungu,muulize farao,waulize sodoma kawaulize gomora,waulize wenyeji wa kanaani,walicho fanywa na waisral

Hakuna kitu chenye wivu duniani Kama mungu kawaulize waizrael wakiwa jangwani baada ya kujifanyia ng'ombe wa shaba na kumwabudu mungu aliwa fanya Nini?

Mungu alimpiga ugumba Sara akaja kumpa mtoto akiwa na miaka 90

Mungu alimpiga upofu zakayo ili yesu mwanae aje achukue maujiko

Mungu alimuumba adamu akiwa mkamilifu aliishi vema na kufuata Sheria zake lakini akaona sio poa akamletea Eva ili amwangushe na Adam akapewa rb ya maisha

Mungu aliuwa watu wote sodoma na gomora. Kisha akamwacha yule mzee luthu na mabinti zake wawili tu

sjui ili iweje? Yani baba na mabinti na hakuna mwanaume mwingine mabinti wakala chakula Cha mama yao AF ni dhambi binti kutembea na mzazi mpaka leo

Lakini mungu ni mwenye upendo

Mungu ni mwenye rehema

Mungu ni nuru yetu na tuifwate🙏🙏🙏
Kuna watu dunia hii wanakuwa kukufuru.
Na hayo yote unayoyadai unajua anaekupa pumzi ya kuendelea kukufuru ni Nani.
Ukilijua Hilo basi mrejee Mungu wako na umtake msamaha maana yeye ni mwingi wa kusamehe.
 
Kila jambo kwa utukufu wa Mungu pamoja na sababu zake husika.Na pia sio ulemavu tu hata kupata au kukosa baadhi ya vitu/ watu tunavyovipenda katika maisha ni kwa sababu ya Mungu alishatangulia mbele na kuona.Kuna kisa kimoja cha Padri aliyekuwa na nguvu ya uponyaji, kuna bubu alimfuata akimuomba amponye ila alimwambia uliumbwa hivyo kwa mapenzi ya Mungu na ungalipewa uwezo wa kuongea ungetumia kuwadhuru wengine hivyo ni vyema kubaki kama ulivyo.Aliponya wengine ila yule bubu hakumponya.
 
Kwamba ilikuwa ni lazima kazi zake zidhihirike kupitia hao walemavu? Yaani walemavu na wale wote wenye madhila kama hayo ndiyo watolewe kafara/wabebe gharama za kudhihirisha hizo kazi kwa watu wengine?
dunia bado haijaeleweka hii,, Anyway bigup kwa akili kubwa🙏🙏🙏
 
Kwamba ilikuwa ni lazima kazi zake zidhihirike kupitia hao walemavu? Yaani walemavu na wale wote wenye madhila kama hayo ndiyo watolewe kafara/wabebe gharama za kudhihirisha hizo kazi kwa watu wengine?
Nani kakwambia wametolewa kafara?
 
Mungu hakuwaumba wanadamu wakiwa na ulemavu. Ulemavu ni matokeo ya dhambi ya Adamu na Hawa walipomkataa Mungu

Waroma 5:12 BHN​

12. Kwa njia ya mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, nayo ikasababisha kifo. Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu, kwa maana wote wametenda dhambi.


Mungu anatutakia mema sikuzote

Isaya 35:5Biblia Habari Njema (BHN)​

Hapo vipofu wataona tena,na viziwi watasikia tena

Ufunuo 21:3-4 BHN​

3. Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Maskani ya Mungu kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.

4. Yeye atayafuta machozi yao yote; maana kifo hakitakuwako tena, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!”
Yaani dhambi ya mtu mmoja iwadhuru wasio na hatia?
 
Tuache tabia ya kumpakazia Mungu "eti ni mapenzi yake" tutafute chanzo chake!! Mf. Mtu anakuwa taahira ! Hapo hakuna kamchezo ka binadamu? What is the source of evil in the universe?
 
Wapo lakini ni wachache sanaaaaa!!!

Na bidii waliyotumia laiti wangekuwa ni wazima basi ingekuwa ni mara kumi.

Ni kama vile Mo au Bakhresa wangekuwa na ulemavu wangeweza kufanikiwa ila sio katika level walizofikia wakiwa wazima
Kama ndo hivyo basi wasio kuwa na ulemavu wowote wote wangekuwa matajiri.
 
Kuna watu dunia hii wanakuwa kukufuru.
Na hayo yote unayoyadai unajua anaekupa pumzi ya kuendelea kukufuru ni Nani.
Ukilijua Hilo basi mrejee Mungu wako na umtake msamaha maana yeye ni mwingi wa kusamehe.
Chanzo Cha yote ni mungu shetan majini vimbwenga nk chanzo ni mungu
 
Dunia yenye walemavu iko logically consistent na dunia ambayo haijaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Mungu huyo, angalau kidhana, ana upendo na rehema kubwa sana kiasi kwamba asingeumba dunia ambayo ulemavu unawezekana kuwepo.

Ukiona dunia ina ulemavu, huo ninushahidi Mungu huyo hayupo.

Ukishaelewa Mungu huyo hayupo, ulemavu unakuwa si tatizo, unakuwa kitu kinachotokea naturally tu, kwa sababu nature si lazima itoe matokeo mazuri na wala haijali.

Ukitaka kumuweka Mungu kama muumba wa dunia, habari za watu kuzaliwa walemavu, watoto kufa wachanga, na mabaya yote ya duniani, zinakuwekea contradiction kubwa sana kuhusu uwepo wa huyo Mungu.
Ahsanteeee.
 
Back
Top Bottom