Uchaguzi 2020 Ni wakati gani JWTZ inapaswa kuingia mtaani kushiriki shughuli za kisiasa na kutuliza ghasia?

Uchaguzi 2020 Ni wakati gani JWTZ inapaswa kuingia mtaani kushiriki shughuli za kisiasa na kutuliza ghasia?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Zamani tulikua tunafundishwa majukumu ya ulinzi yalivyogawanyika. Kwa kumbukumbu zangu mgawanyo ulikuwa hivi:
1. Usalama walikua na jukumu la kukusanya kuchakata na kushare taarifa kwa jamii na vyombo vingine kuhusu viashiria mbalimbali vya uvunjifu wa amani au fursa ambazo Kama nchi tunapaswa kuziona na kuzipigania. Walihusika kukusanya taarifa kuhusu diplomasia ya kimataifa , uchumi nk na kusambaza taarifa kwenye mamlaka husiku kwa ajili ya kufanyiwa kazi. Hawa kwa Ulimwengu wa Sasa tunaweza sema ni search engine au Google ya nchi, kila taarifa unaweza ipata.

2. Polisi walikabidhiwa ulinzi wa raia na Mali zao

3. JWTZ walikabidhiwa ulinzi wa mipaka dhidi ya maadui wa nje wanaotaka kulivamia taifa letu.

4. Uhamiaji walipewa udhibiti mipakani kuchuja wa kuingia na kutoka.

5. Magereza ilikua sehemu yakuhifadhi watuhumiwa na wahalifu pamoja na kuwafunza namna yakuachana na uhalifu, kurekebisha tabia.

Lakini baadaye kikaongezeka chombo kingine kinaitwa TAKUKURU kinachofuatilia usalama wa rasilimali Mali zetu,maadili na utoaji huduma pamoja na kudhibiti rushwa na viashiria vyake.

Aidha, vyombo vyote hivi vina uniform ambazo nikisoma kwenye websites na machapisho mbalimbali online zimeainishwa vyema kabisa kwa ajili ya mwananchi kujua na kumtambua vyombo vyetu japo katika mazingira flani ndani ya vyombo wapo Askari kanzu.

Lengo langu kuu ni kuhusiana clip inayosambaa ikielezwa ni ya Zanzibar na hata hapa janvini ipo. Clip ile inaonyesha askari mwenye nguo za JWTZ, Polisi na uniform nyeusi ambazo hazijasajiliwa kwenye chombo chochote kwa mujibu wa uniform za taasisi zetu. Lakini pia uniform uvaliwa na watu nadhifu na kwa unadhifu. Ukiangalia hii clip unabaini hawa wenye uniform nyeusi wamenyoa mnyoo usioendana na vyombo vyetu lakini pia mitutu ya slaha walizoshika imeelekezwa kwa raia kinyume kabisa na ukubwa na nguvu ya raia waliolengwa. Sasa basi, naomba tuelimishane kwa lengo lakujifunza

1. Ni wakati gani JWTZ anaingia mtaani kukabiliana na raia?
2. Hizi uniform nyeusi ni za Jeshi gani?
3. Vyombo vyetu vipo tayari kukubaliana na taarifa chafu kwamba hizi ni uniform za Butundi? Kwanini tusilitolee majibu kuvisafisha vyombo vyetu kutoka kwenye maneno ya watu wasiovitakia mema vyombo hivi?
4. Zanzibar ipo vitani?
 
Jeshi halipangiwi na raia nini cha kufanya, liko kwa kazi moja tu kuhakikisha nchi unakuwa salama muda usiku na mchana 24/7

Wewe endelea na maisha yako kama Jana juzi na Leo na wao waache waendelee na majukumu yao Aisha mipakani makambini au mitaani wewe yahakuhusu
 
Ukiingia tu Zanzibar airport au bandarini wanajeshi na mitutu wapo na wanaongoza watu utasikia " we mjinga pita kule usisimame hapo panga mstari. Yaani never seen before. Afadhali uchaguzi usiwepo kabisa tuishi tu kama mifugo.
Hiyo ni kazi yao wakati wanaoona wao unafaa hutakiwi kujadili Hilo, kipindi hiki kama hujui ndio kipindi kigumu Sana kwa viongozi wa ulinzi kitaifa, lolote linaweza kutokea

Acheni watu wafanye kazi zao nyie zinawahusu nini mpaka mnauliza uliza
 
Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2015, kura za madiwani pamoja na kura za Wabunge na Rais baada ya kujumlishwa na kuandikwa katika fomu za matokeo, wasimamizi walizipeleka katani ili ziunganishwe na kupata matokeo ya jumla kwa kata husika. Baada ya hapo, nakala halisi za matokeo hayo zilipelekwa jimboni ili kuunganishwa na kupata jumla kwa jimbo huku nakala zingine wakipewa mawakala.

Ikumbukwe hapa ilikuwa ni rahisi kudhibiti ikiwa kutatokea nyongeza ya VITUO HEWA vya kupigia kura.

LAKINI MWAKA 2020;

Baada ya kura kuhesabiwa na kupata matokeo ya kituo husika,ni matokeo ya MADIWANI tu yatakayounganishwa katani lakini matokeo ya WABUNGE NA RAISI kwa kila kituo, HAYATAUNGANISHWA KATANI badala yake yatapelekwa jimboni kuunganishwa.

IMG_20201026_193517.jpg



TATIZO LINAWEZA KUTOKEA:
Tatizo hili linaweza kuwa kuongeza vituo hewa endapo mawakala hawatakuwa na orodha ya vituo vyote vya jimbo na ikiwa hawatakuwa makini wakati wa kujumlisha kura.

VYAMA VYOTE VYA SIASA, CHUKUA TAHADHARI.
Malalamiko FC!
 
Jeshi kulinda amani nchini kwake?

Mimi ninavyojua ni walati nchi imeingia vitani ...
Hata pale linapoona Kuna uwezekano nchi ikaingia vitani kwasababu ya wapuuzi wachache. Ni lazima ulidhibiti tatizo kabla halijawa kubwa.
 
Watu wakishachoka na Dhulma na ukosefu wa HAKI
Unasubiriwa kesho kura zinaanza kupigwa Zanzibar karibu sisi tupo tayari Zanzibar tayari kupokea ushindi wa kishindo babu Maalim lazima apigwe chini.
 
Zamani tulikua tunafundishwa majukumu ya ulinzi yalivyogawanyika. Kwa kumbukumbu zangu mgawanyo ulikuwa hivi:
1. Usalama walikua na jukumu la kukusanya kuchakata na kushare taarifa kwa jamii na vyombo vingine kuhusu viashiria mbalimbali vya uvunjifu wa amani au fursa ambazo Kama nchi tunapaswa kuziona na kuzipigania. Walihusika kukusanya taarifa kuhusu diplomasia ya kimataifa , uchumi nk na kusambaza taarifa kwenye mamlaka husiku kwa ajili ya kufanyiwa kazi. Hawa kwa Ulimwengu wa Sasa tunaweza sema ni search engine au Google ya nchi, kila taarifa unaweza ipata.

2. Polisi walikabidhiwa ulinzi wa raia na Mali zao

3. JWTZ walikabidhiwa ulinzi wa mipaka dhidi ya maadui wa nje wanaotaka kulivamia taifa letu.

4. Uhamiaji walipewa udhibiti mipakani kuchuja wakuingia na kutoka.

5. Magereza ilikua sehemu yakuhifadhi watuhumiwa na wahalifu pamoja na kuwafunza namna yakuachana na uhalifu, kurekebisha tabia.

Lakini baadaye kikaongezeka chombo kingine kinaitwa TAKUKURU kinachofuatilia usalama wa rasilimali Mali zetu,maadili na utoaji huduma pamoja na kudhibiti rushwa na viashiria vyake.

Aidha, vyombo vyote hivi vina uniform ambazo nikisoma kwenye websites na machapisho mbalimbali online zimeainishwa vyema kabisa kwa ajili ya mwananchi kujua na kumtambua vyombo vyetu japo katika mazingira flani ndani ya vyombo wapo Askari kanzu.

Lengo langu kuu ni kuhusiana clip inayosambaa ikielezwa ni ya Zanzibar na hata hapa janvini ipo. Clip ile inaonyesha askari mwenye nguo za JWTZ, Polisi na uniform nyeusi ambazo hazijasajiliwa kwenye chombo chochote kwa mujibu wa uniform za taasisi zetu. Lakini pia uniform uvaliwa na watu nadhifu na kwa unadhifu. Ukiangalia hii clip unabaini hawa wenye uniform nyeusi wamenyoa mnyoo usioendana na vyombo vyetu lakini pia mitutu ya slaha walizoshika imeelekezwa kwa raia kinyume kabisa na ukubwa na nguvu ya raia waliolengwa. Sasa basi, naomba tuelimishane kwa lengo lakujifunza

1. Ni wakati gani JWTZ anaingia mtaani kukabiliana na raia?
2. Hizi uniform nyeusi ni za Jeshi gani?
3. Vyombo vyetu vipo tayari kukubaliana na taarifa chafu kwamba hizi ni uniform za Butundi? Kwanini tusilitolee majibu kuvisafisha vyombo vyetu kutoka kwenye maneno ya watu wasiovitakia mema vyombo hivi?
4. Zanzibar ipo vitani?
Tumekabidhi nchi kwa washamba na limbukeni wa madaraka
 
Back
Top Bottom