Uchaguzi 2020 Ni wakati gani JWTZ inapaswa kuingia mtaani kushiriki shughuli za kisiasa na kutuliza ghasia?

Vipi kule Mtwara haikuwezekana hilo jeshi kuwahi kuthibiti lililotokea au ni kwenye siasa tu?
Kwani wanaendelea na chokochoko tena huko? Wengine tayari wameshanyang'anywa silaha haraka haraka! Nasikia na wewe wanakutafuta kuhusiana na matukio kama hayo!
 
Ukiingia tu Zanzibar airport au bandarini wanajeshi na mitutu wapo na wanaongoza watu utasikia " we mjinga pita kule usisimame hapo panga mstari. Yaani never seen before. Afadhali uchaguzi usiwepo kabisa tuishi tu kama mifugo.
Halafu wanalazimika nyongeza za mishahara
 
Hata pale linapoona Kuna uwezekano nchi ikaingia vitani kwasababu ya wapuuzi wachache.Ni lazima ulidhibiti tatizo kabla halijawa kubwa.
Why hizo nguvu wasizielekeze mtwara kwa islamic state kuliko kudili na wasio hata na rungu
 
Ni kweli jukumu la msingi la JWTZ ni kulinda dhidi ya maadui wa nje. Lakini wao ni sehemu ya vyombo vya ulinzi na usalama. Kama ikibidi kusaidia ndani ya nchi wanasaidia, hata polisi siku nchi ikiingia vitani wanaitwa kwenda kusaidia.

Huwezi kuangaika kulinda ukuta wakati nyumba inawaka moto.
 
Ujumbe wa Vijana wa ACT Wazalendo kwa Mkoloni Mweusi

Njoo uone mji wa Zanzibar ulivyo shwari kwa sasa hivi hakuna chokochoko yoyote kesho ni kupiga kura na kwenda nyumbani kwako.
 
Baada ya tume kukabwa Koo na polisi kushindwa kwa hoja na haki... Sasa wanataka msaada wa jwtzz...

CCM Wana Hali mbaya... Makada wapo hawajielewi..
Pamoja na Majeshi na Wasiojulikana Polisi na wenzao Vijana shupavu wa ActWazalendo wafikisha Ujumbe
 
Upuuzi tu....

Povu la nn... Matusi ya nn...
Huna hoja.. !!!
Hakuna tusi hapo au lugha ya mabeberu inakupiga chenga! Hopeless siyo tusi mkuu wala slavery mentality siyo tusi. Please be informed accordingly!!
 
Upepo wa mabadiliko hauzuliki kwa mabomu bali kwa maridhiano, uzuri wanaowategemea awajawaongezea mishahara 5 yrs hapa patamu tuone watakavyogeukwa awatoamin
 
Mkuu ikiwa kuna viashiria vyovyote vya uvunjigu wa amani ya nchi, tilia umuhimu neno hili ''UVUNJIFU WA AMANI YA NCHI'' majeshi yote kwa pamoja ambayo ni JWTZ, POLISI, MAGEREZA, UHAMIAJI NA JESHI LA AKIBA (MGAMBO) wanalo jukumu la kushirikiana na kuhakikisha amani ya nchi inarejea katika hali yake ya kawaida.

Amani ikirejea katika mstari kila jeshi litaendelea na majukumu yake. Nadhani umeelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…