Kafulila ni mwanaccm tangu zamani huko Upinzani alienda kazi maalum tuKwa kitengo alichopewa kilivyo na pesa na hakina stress za siasa kamwe hawezi kurudi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kafulila ni mwanaccm tangu zamani huko Upinzani alienda kazi maalum tuKwa kitengo alichopewa kilivyo na pesa na hakina stress za siasa kamwe hawezi kurudi
Ni kwa Mzalendo baada ya MzalendoUmetoka kwa mama sasa hivi upo kwa Kafulila!
Yajayo yanafurahisha..!🤸
Tutafika tu safari bado ni ndefu Mwamshamba ni jembe la kizalendoMbona wewe ndiye una utoto na ujinga mwingi tu unataka kujifanya kiranja wa humu jukwaani.
Jamaa akirudi atawadhibiti sana UpinzaniNingependa sana Kafulila arudi bungeni, alichangamsha sana bunge wakati ule.
Sasa Kafulila anahusikaje hapa kwa Lucas Mwashambwa ?Unamharibia na wewe mleta mada unajiharibia
Taratibu za CCM haziruhusu kuanza kampeni mapema au hujui Hilo?
Unajifanya hujui eeeh!Sasa Kafulila anahusikaje hapa kwa Lucas Mwashambwa ?
Mwenye kosa ni huyo Kafulila au Mwandishi?
Nimebubujikwa na machoziNdugu zangu Watanzania,
Kila jambo na majira yake na wakati kwa kusudi maalumu chini ya mbingu. Nafikiri sote tunamfahamu vyema Mheshimiwa David Kafulila,tunafahamu uzalendo wake kwa Taifa letu,uchapa kazi wake, upendo wake kwa Wananchi. Tunafahamu vyema na kwa undani uwezo wake wa kujenga hoja na kuitetea hoja,tunafahamu bila shaka uelewa wake wa masuala mbalimbali hususani ya kiuchumi, biashara,fedha n.k.
Sote ni wazi tunakubaliana kwa pamoja kuwa Chuma David Kafulila ni mtu aliye muadilifu,muaminifu na mtu aliyenyooka kama rula kitabia.hanaga kupinda pinda. Ni mtetezi wa kweli wa Taifa letu kama ilivyo kwa mama yetu na Jemedari wetu Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan. Sote tunatambua ni mtu mnyenyekevu,mstarabu na mtulivu sana kiongozi.
Sote tunatambua kuwa ni mtu anayeacha alama za kiuongozi kila eneo anapopewa nafasi na kuaminiwa kutumikia Taifa lake.tumeona tangia akiwa mbunge,RAS Songwe,RC Simiyu na sasa mkurugenzi Mkuu wa PPP.
Hivyo naona ni wakati muafaka na sahihi na wakati wake wa kuweza kurejea Bungeni hapo mwakani panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu.ni wakati wa kulitumikia Taifa lake na kumsaidia Mheshimiwa Rais katika masuala mbalimbali ya kisera. Ni dhahiri sauti ya Chuma David Kafulila inahitajika Bungeni.ni muhimu watu aina yake wakawa sehemu ya bunge.
na kama ikimpendeza Jemedari wetu Mama Samia Basi anaweza kumvuta ndani ya Baraza lake la Mawaziri atakaloliunda mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi na yeye kuwa amepita na kushinda Urais kwa kishindoo.maana watanzania wanakiu kubwa sana ya kumpa kura za ndio kwa fujo kama shukurani kwa kazi kubwa aliyowafanyia.
Natambua pia watu aina ya David Kafulila huwa wakati mwingine wanapigwa vita sana,kuchukiwa bila sababu ,kusingiziwa uongo,kupakwa matope,kusulubiwa na mikuki ya maneno ya kizushi na uongo na watu wenye uchafu na Makando kando au wasiopenda kusikia ukweli masikioni mwao. Lakini tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutupatia Rais Samia Jemedari wetu imara na shupavu ambaye yeye amejaa upendo mkubwa sana kwa watu wazalendo na wachapa kazi aina ya David Kafulila na ndio maana ameendelea kuwa naye na kumuamini mpaka kumpatia Ukurugenzi wa PPP. japo kuna watu hasa wabaya wa Kafulila wanatamani au wasingependa kuona akipata nafasi yoyote ile katika serikali ya Rais SAMIA maana inakuwa inawapa hofu na uoga mkubwa sana.
Watanzania tunapaswa kujenga utamaduni wa kuwatia moyo, kuwaunga mkono,kuwatetea ,kuwasemea wazalendo aina ya Daktari Mama Samia Suluhu na David Kafulila na wengine wengi.kwa kuwa wazalendo siku zote hupigwa vita ,kushambuliwa,kuumizwa,kutengenezewa ajali,kuchafuliwa na kuchukiwa sana bila sababu ya aina yoyote ile. Tumlinde na kumtetea Rais wetu na wale wote wanaoonyesha dhamira na muelekeo wa uzalendo kwa Taifa letu kwa dhati ya mioyo yao. David Kafulila Ni mzalendo na mchapakazi na anastahili kuungwa mkono.
Ngoja niweke kalamu yangu chini ili kutorefusha andiko na kuwachosha wasomaji.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
🤑🤑Tutafika tu safari bado ni ndefu Mwamshamba ni jembe la kizalendo
Kama Kuna maandiko mengi ameyaandika huyu bwana basi ni maandiko ya kumpigia debe mama 2025 unataka kusema ndio chama kitamkata mama jina hiyo 2025? 😂😂Unajifanya hujui eeeh!
Chawa endeleeni hivyo hivyo kumuharibia nafasi ndegere, siku akikatwa mkia wake msije tena hapa hapa JF kulia lia.
Hivi unaelewa unachoandika kweli wewe? Kafulila awadhibiti wapinzani kivipi sasa?Jamaa akirudi atawadhibiti sana Upinzani
Kafulila ni hoja Kwa hoja tangu enzi na enzi 2025 ni Bunge la Upinzani mwingi so lazima CCM pia itume vifaa vyenye hoja bungeniHivi unaelewa unachoandika kweli wewe? Kafulila awadhibiti wapinzani kivipi sasa?
Wewe bora ukaage kimya tu,nimekuuliza ni kwa jinsi gani Kafulila atawadhibiti wapinzani,au huelewi maana ya kudhibiti? Kumbe hii ndiyo ID yako mpya ndiyo maana naona aina yako ni ile ile unaulizwa maji unajibu pombe.Kafulila ni hoja Kwa hoja tangu enzi na enzi 2025 ni Bunge la Upinzani mwingi so lazima CCM pia itume vifaa vyenye hoja bungeni
ID ya nani?Wewe bora ukaage kimya tu,nimekuuliza ni kwa jinsi gani Kafulila atawadhibiti wapinzani,au huelewi maana ya kudhibiti? Kumbe hii ndiyo ID yako mpya ndiyo maana naona aina yako ni ile ile unaulizwa maji unajibu pombe.
Mimi kama mzalendo wa Taifa langu nina kiu ya kuona Mheshimiwa David Kafulila anaingia Bungeni hapo Mwakani.Sasa Kafulila anahusikaje hapa kwa Lucas Mwashambwa ?
Mwenye kosa ni huyo Kafulila au Mwandishi?
Mheshimiwa Kafulila Ni chuma kwelikweli kwa upande wa Hoja.Kafulila ni hoja Kwa hoja tangu enzi na enzi 2025 ni Bunge la Upinzani mwingi so lazima CCM pia itume vifaa vyenye hoja bungeni
Nahujafanya tatizo loloteMimi kama mzalendo wa Taifa langu nina kiu ya kuona Mheshimiwa David Kafulila anaingia Bungeni hapo Mwakani.
🤣🤣🤣🤣🤣Nahujafanya tatizo lolote