Ni wakati muafaka Watanzania kuipongeza serikali na wananchi wazalendo wa Msomera Tanga kwa kuinusuru hifadhi ya Ngorongoro kupotea

Ni wakati muafaka Watanzania kuipongeza serikali na wananchi wazalendo wa Msomera Tanga kwa kuinusuru hifadhi ya Ngorongoro kupotea

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Wananchi wazalendo wa msomera mkoani Tanga, ambao hapo kabla walikua wakiishi ndani ya hifadhi ya Taifa ngorongoro, ambapo baadae kwa kushauriana na mamlaka za serikali, na kwa hiyari na utashi wao, Lakini pia kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa, na urithi wa vizazi vijavyo, wananchi wale waTanzania wazalendo walikubali kuondoka kutoka hifadhini na kwenda kuishi katika eneo mbadala walilotengewa huko msomera mkoani Tanga..

Wananchi hawa wazalendo nchini, kaya zaidi ya elfu moja, zenye watu zaidi ya elfu nane, walikubali wito wa Serikali wa kuondoka maeneo yale, ili kuepusha uharibifu wa mazingira ya hifadhi na kutunza mali asili katika eneo hilo ambazo zilikua zimaanza kuharibika na zilikua hatarini zaidi kupotea na kutoweka kabisa...

Na kwa hatua za kisheria na kikatiba ilizichukua serikali, eneo la hifadhi ya Taifa ya ngorongoro hakuna tena watu wanaishi ndani yeke..

Wavamizi wa hifadhi zote za Taifa nchini watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria, ili kuilinda na kutunza maliasili za Taifa kwa maslahi mapana ya waTanzania wote...🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Screenshot_20240815-002243~2.jpg
 
Mimi mnipe tu mgao wangu. Siyo mnauza tu raslimali zetu, halafu hela mnatumbua wenyewe.
keki ya Taifa ni kwa maslahi mapena ya Taifa,

sote tunafaidi hiyo kwenye huduma bora za afya, miundombinu umeme na maji ya uhakika, elimu bure n.k🐒
 
Mkuu, hivi kati ya wamasai wanaofukuzwa, na waarabu wanaouziwa maeneo kuna tofauti yoyote ya ubinadamu wao?
hakuna na hayupo mtu yeyote Tanzania aliefukuzwa popote nchini...

waliokua wakiishi ndani ya hifadhi ya Taifa ya ngorongoro wote wamehamia msomera mkoani Tanga na wanaishi huko raha mustarehe sana. hakuna tena watu katika hifadhi 🐒
 
Wewe utakuwa miongoni mwa wachache waliopelekwa Dubai nadhani hivyo,si bure.waliondoka wenyewe wakati waliobaki wanaandamana, katiba inatakiwa kufumiliwa upya kabisa au kupata mpya ya wananchi.
 
😂😂 Kunusuru nini weye, Sema wajomba hawataki usumbufu kwenye vitalu vyao🤔😂 wanataka wajimwae mwae wenyewe. Kwa mafweza waliotoa😂😂😂 hata Mimi ningewasahau Wallah.
 
Wewe utakuwa miongoni mwa wachache waliopelekwa Dubai nadhani hivyo,si bure.waliondoka wenyewe wakati waliobaki wanaandamana, katiba inatakiwa kufumiliwa upya kabisa au kupata mpya ya wananchi.
ndrugu zango,
nayasema haya kwa uwazi hivi ni kwa maslahi mapana ya waTanzania wote,

na mbona Dubai tena, kulikoni?
tujifunze kuwa wazalendo kwa Taifa na kuwa wakweli 🐒
 
Back
Top Bottom