Nichagulieni gari kwa bajeti ya Milioni 10

Nichagulieni gari kwa bajeti ya Milioni 10

Ngoja madalali wakufuate PM, watakung'ang'ania hadi utajuta kutoa tangazo, hafu wengi gari ni vimeo kuwa makini
Shikamoni waheshimiwa,
Mimi sijawahi kumiliki gari tangu nizaliwe.

Kazi yangu ni kuuza duka la Mangi,
Kipato changu ni wastani wa Laki 5 kwa mwezi (hakiko imara kabisa; kinaweza kupungua au kuongezeka kidogo kutegemea na hali ya biashara).

Nimedunduliza hela kwa miaka miwili nimepata milioni kumi.
Lengo langu nipate gari la kutembelea mjini na mimi.

Sasa ninachoomba waheshimiwa,
Nichagulieni gari kwa kuzingatia kipato changu hapo juu.

Kuna watu wataniuliza maswali ya kitaalamu hapa,
Mara Injini silinda sita, mara cc za mafuta,
Mimi sina ujuzi huo.

Mimi ninachotaka mnichagulie gari dogo lolote,
Mimi nitaendesha tu ili mradi litoke Japan na mpaka kulipia gharama zote na kuanza kuliendesha kwa uhuru isizidi kiasi tajwa hapo juu.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We Udochi naona kuna watu wanakushauri vizuri wengine vibaya. Sasa fuata ushauri wangu.
Toyota Ist 1490cc itakufaa kwa sababu kwanza bajeti yake ndio hiyo milioni 9.5 mpaka 10.5m
Kwa ulaji wa mafuta utaiweza na Ac pia unawasha.
Kwa vile ni mjasiriamali hata bidhaa zako za dukani unaweza kununua kutoka labda pale kwa Moshiro Kinyerezi kuzipeleka huko mjini kwako unakouzia bila tabu na petrol ikatumika ya wastani tu.
Usinunue Noah, Brevis, Mark 2 Grande zitakufilisi wala Vitz pia usinunue.

Na hiyo Ist mil 9.5 mpaka 10.5 unazipata hapahapa Dar wala usihangaike kuagiza.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watafutwe kimomwe motors watakuchagulia na kukuagizia gari safi.wapo Facebook, tweeter, ofisi ziko magomeni mapipa, pembeni ya stand ya mwendokasi upande wa kulia ukiwa unaelekea kariakoo.
Shikamoni waheshimiwa,
Mimi sijawahi kumiliki gari tangu nizaliwe.

Kazi yangu ni kuuza duka la Mangi,
Kipato changu ni wastani wa Laki 5 kwa mwezi (hakiko imara kabisa; kinaweza kupungua au kuongezeka kidogo kutegemea na hali ya biashara).

Nimedunduliza hela kwa miaka miwili nimepata milioni kumi.
Lengo langu nipate gari la kutembelea mjini na mimi.

Sasa ninachoomba waheshimiwa,
Nichagulieni gari kwa kuzingatia kipato changu hapo juu.

Kuna watu wataniuliza maswali ya kitaalamu hapa,
Mara Injini silinda sita, mara cc za mafuta,
Mimi sina ujuzi huo.

Mimi ninachotaka mnichagulie gari dogo lolote,
Mimi nitaendesha tu ili mradi litoke Japan na mpaka kulipia gharama zote na kuanza kuliendesha kwa uhuru isizidi kiasi tajwa hapo juu.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom