Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemkamata Joyce Mbaga maarufu kwa jina la Nicole Joyberry kwa tuhuma za kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu na kufanya biashara ya kuanzisha ma-group na kukusanya pesa kinyume na sheria.
Taarifa hiyo imetolewa leo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro na kusema matukio hayo yametokea katika maeneo tofauti tofauti ya Jiji la Dar es Salaam na wakati mwingine nje ya mkoa wa Dar es Salaam.
Your browser is not able to display this video.
"Matukio haya yametokea ndani na nje ya Dar es Salaam, kwa kuhamasisha baadhi ya watu akianzisha ma-group mbalimbali na kuweka majina hewa kwenye ma-grouup hayo kwamba wanachangia pesa na baada ya muda mfupi basi utapata kiwango kikubwa cha pesa, jambo ambalo baadaye anakuja kutopatikana kwenye simu na kupotea na pesa ambazo watu wamechangia," amesema Kamanda Muliro
Watanzania sio wa kuwaonea huruma. Haya majanga huwa wanayataka.
Ponze scheme zote zinaishia kwenye haya ila bado kesho wengine wataenda kumchangia mwizi mwingine mamilioni.
Yale makalio chakula cha bwana jela
Watanzania sio wa kuwaonea huruma. Haya majanga huwa wanayataka.
Ponze scheme zote zinaishia kwenye haya ila bado kesho wengine wataenda kumchangia mwizi mwingine mamilioni.
Yale makalio chakula cha bwana jela
Maisha yanaenda Kasi, Kila MTU Kila siku anatafuta namna ya kuishi. WACHINA Kila siku wanakuja na Gunduzi za Kila aina , Gunduzi zao zinawekwa mitandaon , zipo Gunduzi zinazowekwa mitandaoni lakn zinakua restricted kutumika kwenye Nchi zao tu . WABONGO MATAPELI, na vile tuna TCRA ya kudeal...