Nielewesheni hili jambo Rais Samia kuzungumza na wanawake wa Tanzania siku ya Demokrasia duniani

Nielewesheni hili jambo Rais Samia kuzungumza na wanawake wa Tanzania siku ya Demokrasia duniani

Behaviourist

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2016
Posts
39,926
Reaction score
95,626
September 15 ni siku ya kimataifa ya demokrasia duniani ambapo nchi mbalimbali duniani hupata fursa ya kujadili demokrasia ya nchi zao na wadau husika wa demokrasia katika nchi hizo kama vile vyama vya upinzani.

Sasa sielewi mantiki ya Rais Samia Suluhu Hassan kuitumia hiyo siku ya leo kuzungumza na wanawake wa Tanzania (mara ya pili) na sio wadau wa demokrasia (vyama vya siasa).

Katika hali ya kawaida nilikuwa nategemea Rais akutane na wadau wa demokrasia kama vile vyama vya upinzani kisha wajadili hatima ya demokrasia ya nchi yetu lakini yeye anakutana na wanawake na tena hii ni mara ya pili.Kwangu mimi jambo hili haliingii akilini.

Au siku ya wanawake Duniani (March 08) ndiyo atakutana na wadau wa demokrasia (hususani vyama vya siasa) kujadili masuala ya kidemokrasia?

Sielewi mantiki ya kuwakimbia wapinzani wake wa kisiasa ambao ndiyo wadau wakubwa wa demokrasia hapa nchini.Nielewesheni

Ukiangalia picha ya pili hapo chini Tanzania tumezidi kushuka katika marks za demokrasia duniani ambapo sasa hivi tumeshuka kutoka marks 40/100 hadi kufika marks 34/100.

Yaani kama ni mtihani wa darasani maana yake ni kwamba umepata marks 34 kati ya mia.Hii si kupata F?

Hii maana yake ni kwamba bado kidogo tunaingia kwenye “not free countries” kwa sababu ya kuminya haki za kisiasa na za kiraia halafu Rais siku ya demokrasia duniani kama ya leo anaenda kukutana na wanawake badala ya kukutana na wadau wa demokrasia.

Mn4yH.jpg

Acxcay.jpg

E4D5i.jpg
 
Kwani Tanzania kuna chama chochote cha demokrasia? Kipi Chadema hiki ambacho mwenyekiti Taifa hataki ushindani na akina Sumaye na Zitto Kabwe wakitaka kugombea na ambacho hakina ukomo wa uenyekiti Taifa?
 
Rais pia anatumia demokrasia kuzungumza na kundi lolote analotaka. Kitendo cha kutaka kumpangia ni kuminya demokrasia yake
 
Rais hakosei anajua kila kitu au umesahau alishatueleza hivo
 
siku zooote tunasema huyu samia hajielew na hana uwezo wa kuongoza nchi , majanga anayosababisha mnasingizia washauri wake ilimrad mumtoe kwenye udhaifu, ukwel ni kwamba huyu ni mbaguzi na hafai kuongoza hii nchi, na mujue kuwa huyu alikuwa na ndoto za kuwa rais, kuwa yeye hapo si bahat mbaya, kitendo cha mtu kuchukua form ya kutaka kugombea nafas huyo tyr alkuwa na nia ya urais, na alpokosa nafasi haimaanishi kuwa slkuwa kakata tamaa, kwaiyo yeye kufanya maujinga yske yote mujue kuwa afanyi bahat mbaya, maana ndilo kusud lake..ACHENI KUMTETEA
 
Kwa hiyo ni sahihi pia siku ya ukimwi duniani Rais kuongea na vipofu au watu wenye ugonjwa wa utindio wa ubongo?
Ndio ni sahihi kabisa maana atawaasa hao vipofu kujikinga na virusi vya ukimwi na kama.kuna kipofu anao basi aendelee kutumia dawa na kufuata masharti
 
Ndio ni sahihi kabisa maana atawaasa hao vipofu kujikinga na virusi vya ukimwi
Kwani siku ya ukimwi duniani ni siku ya kukusanya vipofu ambao hawana ukimwi na kuwaasa kuwa wajikinge na ukimwi?
na kama.kuna kipofu anao basi aendelee kutumia dawa na kufuata masharti
Soma ninachoandika between lines,hakuna sehemu niliyosema kuwa kuna vipofu wenye ukimwi ambao watahudhuria.
 
HII NDIYO TANZANIA
ALSO YOU CAN SAY[emoji117] TOZONIA AS A NICKNAME.

SHAHIDI MUDA AKIFIKA TU , UKWELI WOTE UTAFAHAMIKA .....

MUDA NI SHAHIDI MZURI SANA.
 
Kwani siku ya ukimwi duniani ni siku ya kukusanya watu ambao hawana ukimwi na kuwaasa kuwa wajikinge na ukimwi?

Soma ninachoandika between lines,hakuna sehemu niliyosema kuwa kuna vipofu wenye ukimwi ambao watahudhuria.
Rais ana haki kidemokrasia ya kukusanya watu wa aina yoyote ile. Siku ya ukimwi akikusanya wa malaria sawa hakuna sheria iliyosema akae na wenye ukimwi.

Turudi kwenye point rais kuongea na wanawake siku ya demokrasia ni sawa. Wanawake nao wanahitaji ushirikishwaji katika demokrasia. Demokrasia sio ya vyama vya siasa peke yake.

Conclusion rais katumia demokrasia yake kufanya anachoona ni sawa. Kwani hakuna wanawake wana siasa?
 
Rais ana haki kidemokrasia ya kukusanya watu wa aina yoyote ile. Siku ya ukimwi akikusanya wa malaria sawa hakuna sheria iliyosema akae na wenye ukimwi.
Unaweza kunieleza siku ya ukimwi duniani inahusu nini?
Turudi kwenye point rais kuongea na wanawake siku ya demokrasia ni sawa. Wanawake nao wanahitaji ushirikishwaji katika demokrasia.
Kwani wanaume hawahitaji ushirikishwaji katika demokrasia?Halafu hao wanawake ndiyo key partner katika masuala ya demokrasia hapa nchini?
Demokrasia sio ya vyama vya siasa peke yake.
Wapi nimesema kuwa demokrasia ni ya vyama vya siasa peke yake?
Conclusion rais katumia demokrasia yake kufanya anachoona ni sawa.
Rais huwa hatumii demokrasia yake kufanya anachoona ni sawa bali huongoza kwa mujibu wa sheria,katiba,kanuni na desturi.
Kwani hakuna wanawake wana siasa?
Kwani hakuna wanaume wanasiasa?
 
Unaweza kunieleza siku ya ukimwi duniani inahusu nini?

Kwani wanaume hawahitaji ushirikishwaji katika demokrasia?Halafu hao wanawake ndiyo key partner katika masuala ya demokrasia hapa nchini?

Wapi nimesema kuwa demokrasia ni ya vyama vya siasa peke yake?

Rais huwa hatumii demokrasia yake kufanya anachoona ni sawa bali huongoza kwa mujibu wa sheria,katiba,kanuni na desturi.

Kwani hakuna wanaume wanasiasa?
Haina haja ya kuielezea siku ya ukimwi duniani, elezea wewe uliyeileta, kwanini raisi akutane na vyama vya siasa,kwanini unatK kumpangia rais. Kama rais anaongozwa na sheria basi itoshe kusema utaratibu umeamua hivyo akutane na wanawake nyinyi wengine subirini
 
Kwani Tanzania kuna chama chochote cha demokrasia? Kipi Chadema hiki ambacho mwenyekiti Taifa hataki ushindani na akina Sumaye na Zitto Kabwe wakitaka kugombea na ambacho hakina ukomo wa uenyekiti Taifa?
Ndio hapo sasa!
 
Unaweza kunieleza siku ya ukimwi duniani inahusu nini?

Kwani wanaume hawahitaji ushirikishwaji katika demokrasia?Halafu hao wanawake ndiyo key partner katika masuala ya demokrasia hapa nchini?

Wapi nimesema kuwa demokrasia ni ya vyama vya siasa peke yake?

Rais huwa hatumii demokrasia yake kufanya anachoona ni sawa bali huongoza kwa mujibu wa sheria,katiba,kanuni na desturi.

Kwani hakuna wanaume wanasiasa?
Hutaki rais akutane na wanawake mnataka akutane na vyama vya siasa wakati demokrasia sio ya vyama vya siasa peke yao. Afu tuache kuwaonea wivu wanawake wakiwa wanaamua kukutana
 
Kwa hiyo ni sahihi pia siku ya ukimwi duniani Rais kuongea na vipofu au watu wenye ugonjwa wa utindio wa ubongo?
Ndio ni sahihi. Kwani wao Hua hawaumwi ukimwi au hawahitaji elimu kuhusu ukimwi?
 
Back
Top Bottom