Nifanyeje wanangu wawe na akili nyingi darasani

Nifanyeje wanangu wawe na akili nyingi darasani

Kuweka ratiba ya kusoma jioni au usiku angalau nusu saa Tu kila siku. Hata kwa watu ambao hawasomi nao washiriki zoezi hilo inajenga sana esp mtoto akikuwa na hiyo tabia ya kujisomea. Enzi zetu tukiwa wadogo wazazi walikuwa na home library huwezi kukosa cha kusoma. Wewe utashika daftari lako yeye na wengine watashika kitabu chochote. Jiulize nani anafanya hili era hizi? Kama mzazi nunua hata atlas kubwa siku moja moja unakaa na mtoto wako unacheza hata kimchezo Tu unataka mji, mto, mlima etc dogo anatafuta mpaka aupate then unampigia story chache kuhusu hilo eneo au kitu hicho. Hawezi kusahau Kamwe. Ndo zilizotujenga Sisi
 
Watoto huchukua toka kweny wazazi lakini uwezekano wa kubadili hilo kuptia Tiba Lishe tangu wakiwa watoto ingewezekana sio sasa wakiwa washakomaaa.

Utapiga uwaue sasa hv akili yao ni waamue wenyewe. Wapo kwenye stage ambayo n ile kama unataka muachisha madawa ya kulevya mtu mzima lazima aamue na adhamirie kuacha ila asipoamua mwenyewe hawezi kuacha.

Akili ya mtoto inaanza tengenezwaa tangu akiwa tumboni kuptia misosi ya mama na baada ya kuzaliwa miaka mi 3 ya mwanzo.

Tangu anapoanza fungua macho kutambaa kuongeaaa,nk

Tunasema MSINGI wa akli ya watoto wetu ambao sisi wazazi ni vilaza unaanza angali hajitambui.
 
Mtoto wako umeanza mfundisha mambo ya darasani akiwa na miaka mi 4 unategemea upate mtoto mwenye akili... kama mtoto anaweza ita BABA akiwa na 1 year kwann usimfundshe vitu vya darasani akifika 1year anavijua kuvitamka hata.

Wazazi mmekazana wafundisha watoto kusema BABAAAAA MAMAAAAA DADAAAA haya aende akajibu baba na mama buko darasani sasa
 
You are what you eat......Mlishe Vyakula vya protein - Samaki na "KILKI" kwa wingi.

Mazingira...Mumjengee mazingira ya kuwa na akili....Mumfundishe kuwa na akili.
 
Miongoni mwa mambo ya maana katika hii dunia mbaya ya siku za mwisho ni Elimu. Kila mzazi anatamani kama mimi ninavyotamani wanangu wawe vichwa darasani katika masomo yao, lakini wengi, kama mimi pia tunaishia kutamani tu hasa tunapoona watoto wa wengine wakifanya maajabu katika masomo yao.

Kwangu mimi wanangu hawaendi nitakavyo, mimi pamoja na wanangu kusoma shule za binafsi, English mid. Anayejua siri ya watoto kufanya vizuri anipe wandugu.

Nimejitahodi kuwakazania kusoma na kuwasaidia mimi mwenyewe. Tuition za kufa mtu, vitabu nanunua. Wakifeli na fimbo wanapata, wakifaulu zawadi wanapata. Lakini sioni kufanya vizuri kule mimi ninakotaka, inaniuma sana.

NIFANYEJE
Namna pekee ya kumfanya mtu afanye unachokitaka akifanye ni kumfanya atake kufanya unachokitaka akifanye huku akiamini kuwa huo ni uamuzi wake binafsi na si matakwa yako.

Soma kitabu cha Dale Carnegie, itakusaidia sana katika hilo. Nimekuambatanishia na kitabu tajwa.

Na kwamba mwanao ana akili jibu ni ndiyo. Tafiti za Kisaikolojia zinaonesha kuwa watoto wanaofanya vizuri sana kitaaluma, wengine huwaita magenius, siyo kwamba wana akili sana, bali wamebahatika kulelewa na watu ambao waliwaaminisha kuwa wana akili sana, nao wakaishia kuwa vile walivyoaminishwa.
 

Attachments

Ni genetics kwa asilimia chache sana. Sababu kama ni kweli genetics zingekuwa ndio zina-determine intelligence ya kiumbe kwa 100%. Then it means kuna familia na vizazi ambavyo ni wajinga milele. Kitu ambacho ni kinyume na sheria kuu ya nature, Development and specific adaptability to certain environments. So usiwasikilize waliosema Genetics kama kichocheo kikuu cha akilia za binadamu.

Bali kwa kiasi kikubwa intelligence ya binadamu inachochewa na Malezi na Mazingira. Hivyo kumlea mtoto kwa kukuza curiosity yake ya utoto na kumjibu kila swali lake na kumsukuma ili aendelee kuwa hivyo ni njia mojawapo. Badala ya kumfokea kwa kumuona msumbufu. Kwani kufanya hivyo kutam-discourage na kudumaza uwezo wake milele. Ukilinganisha watoto huona wazazi wao kama miungu na kuamini kila walisemalo.

Hapo utaupa nafasi ubongo wake kukua kwa haraka, wanaita brain-plasticity na ku-strengthen neurotransmitters. Hivyo kuzidisha ufikiri na kasi yake, ikiwemo kuongezeka kwa curiosity. Hapo lazima apasue masomo ya darasani ambayo kwa wakati huo wa miaka 6-7 yatakuwa chini yake sababu tayari ubongo umekomaa kupitiliza. Ni kama vile wewe upewe maswali ya 5+5. Vilevile kumfunza lugha za kigeni kama English au Kifaransa zinasaidia kukuza uwezo wake wa kufikiri na kusolve vitu.

Kama kweli unataka kukuza an absolute thinking machine basi, kwenye kipengele cha mazingira itabidi uwe strickt kupitiliza. Ikiwemo kuangalia marafiki anaocheza nao kila siku ni watoto wa aina gani kutoka familia gani ya watu wa aina gani ili kutomchanganya wako na wao na kupelekea kudumaa kwa ufikiri, curiosity, utambuzi na brain-plasticity inayochochewa na new informations.

Hapo bado hujachelewa kama bado ni wadogo. Kujibu maswali, kujifunza na udadisi isiwe shule tu. Bali maisha yao ya kila siku.
Vilevile fimbo hazisaidii kitu bali hubomoa tu kwa kumpa mtoto uoga na kumuaminisha yeye hawezi kufanya ulichomwambia kwani njia pekee ni kuelewa. Kitu ambacho sio kweli, sababu mara nyingi mzazi na mwalimu ndio wenye makosa yanayosababisha mtoto kutokuelewa.

Na vilevile mazoea ya mzazi na mtoto. Kama mwanao unamlea kama mbwa kazi yako ni kumpa chakula na kumkaririsha kanuni za hisabati. Basi usitegemee huyo mtoto kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri.
Kukaa nae muda mwingi, kucheza nae, kuongea nae kama mtu mzima, na kuwa na mazoea naye kama rafiki ndiyo njia pekee ya kujua akili ya kweli ya mtoto na kujua utaikuza vipi. Matter of fact, watoto wenye uwezo mkubwa wa kufikiri na ufaulu mkubwa darasani, wengi ndivyo walivyolelewa hivyo. Otherwise ni kazi bure.

Dogo langu anapasua 100% kwenye kila mtihani bila hata kutumia nguvu. Na hata mimi nilikuwa nafaulu mitihani bila hata ya kusoma na kukesha usiku kucha kama wale mabaharia wa mabeseni.

Simply sababu uwezo wa kufikiri na uwezo wa kusolve makubwa ulikuwa mkubwa, hivyo viswali vya mitihani ni kama kumuuliza mtu mzima 1+1.

Kuna thread niliandika a few years back inahusu why Africa haina maendeleo, nenda kaicheck. Nimeelezea baadhi ya haya mambo.
Mkuu unajisifu ww ni kipanga sio
 
Back
Top Bottom