Nifatilie toka shambani kilimo cha mahindi, maharage na alizeti hatua kwa hatua

Nifatilie toka shambani kilimo cha mahindi, maharage na alizeti hatua kwa hatua

Msimu huu wa kilimo ntakua natoa maelezo ya kitaalamu na picha live toka shambani kwa vitendo kuanzia kuaandaa shamba, kuchagua mbegu, kupanda, kuzuia wadudu na magonjwa, mbolea, kupalilia hadi kuvuna endelea kunifatilia.
Mkuu shusha nondoo
 
Kwa kifupi samadi ni muhimu kwenye shamba lolote uwe unapandia pamoja na mbolea za dukani ama laa! Japo km samadi ni nyingi naya kutosha hakuna haja ya kuongeza gharama za uzalishaji kwa kununua tena mbolea za viwandani.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Mkuu heshima kwako, kwa shamba kama ni kubwa mfano Ekari 50 na kama eneo lililopo hakuna ng'ombe wa kutosha unawekaje mbolea kwa shamba la mfano huo...?
 
Mkuu kuna kulima na kupanda. Watanzania wengi wanapanda mahindi sina haja ya kukuwekea picha. Zunguka mashambani ujionee ukulima uliopitwa na wakati.
Nakwambia wakulima wangelima kisasa umasikini TZ tungeisha uaga.
Kuna mwalimu wa mkenya ambae amewekeza kulima kilimo cha kisasa HUVUNA GUNIA 35 KWA HEKA 1.
Njoo kwetu je wakulima wetu wanafikisha hata gunia 20 kwa heka ? Wakijitahidi 15.
Nimejifunza formula za huyo mkenya, analima tofauti na sisi.
Kwa hio usirudie kusema eti kila mtu anajua kulima mahindi sema kila mtu anajua kupanda mahindi. Kupanda ni simple tu, unachimba shimo unaweka mbegu unasubiri mavuno, hao ndio wakulima wa TZ.
Weka Elimu na mbinu anazotumia
 
Wakuu natoa mrejesho km kawaida. Hapa ndipo yalipofikia mahindi,nilipandia samadi tu bila mbolea yoyote. Wiki ijayo naweka mbolea ya CAN shughuli inakua imeisha. Picha ya kwanza ni jinsi mahindi yalivyokuwa wiki ya pili toka kuota. Na hizo picha zingine ndo yalivyo sasa.Mungu ni mwemaView attachment 2877783View attachment 2877784View attachment 2877789View attachment 2877791View attachment 2877793

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Shamba lako kitakuwa zuri yaani,samadi ikuze mahindi vizuri hivyo?
 
Weka Elimu na mbinu anazotumia
Mnapenda vya bure. Kuna elimu ya bure. Tafiti mtandaoni utaipata, mie nilitafiti sasa wewe unataka energy yangu nure ukawe tajiri. Kwa sasa sintaweka kitu cha manufaa bure hapa ispokuwa porojo. Pirojo nitachangia bure.
 
Back
Top Bottom