Nifundisheni jinsi ya kuwaingia watu wakubwa VIP!! Sina kazi sina mchongo Nashindwa Kuongea na Maboss

Si uwapigie, ishu serious we unatuma text si dharau hizo.

Hata kama sio VIP kuna wengine ukituma text ati una shida husaidiwi.
Piga jitambulishe vizuri eleza shida yako ...
Baada ya hapo ndo unaweza kua unamkumbusha kwa texts
 
Hapo namba mbili ("Sinaga urafiki nje ya kazi na maboss") inachangia ulipofika. Ni vizuri kuwa na mahusiano (yenye afya) kwa ajili ya networking hasa kwa career growth. Ukijifungia ndio unakuwa huwajui na inakuwia vigumu kuwa approach.
 
Kuna jamaa aliomba namba kwa mwenzake ambaye amemzidi kimaisha akaambiwa hii namba usipige wala kutuma text ya kawaida ila utume text kwa njia ya wasap tuu [emoji23] nikabaki kucheka
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Fanya haya ukutane na huyo unayemtaka akusaidie.
1. Fanya profiling: Huyo muhusika anapenda nini, kwenda wapi, saa ngapi.

2. Circle yake: Ana watu gani, kuanzia wa chini kabisa hadi anaekaa nao mezani

3. Starehe: Hii ni kama hapo namba 1,
Kuwa mzuri ama expert kwenye eneo la target yako na wewe nenda kwa kuanza na circle yake.
Namaanisha kitu kama anapenda kucheza Fifa ama games basi inabidi uive haswa kwa kuwachakaza wale walioko kwenye mzunguko wake, hii itasaidia sifa zako zisambae kwenye ki-eneo na mwishowe ukionana naye ni yeye ndo anakuwa wa kwanza kuchangamka kabla yako.

4. Usiwe desperate kumfuata, muache yeye akufuate kwa value ambayo utakua nayo. Tengeneza value kupitia skills zinazomvutia huyo unayemtaka.

5. Happy hunting.
P.S yeye ndio akufuate.
 
mtegemea cha nduguye hufa masikini
 
Naungana na wewe mkuu, hii njia ya kujikwamua anayotaka kuitumia huyu mwanajukwaa naona kama ni ngumu mno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…